Tuesday, October 27, 2015

Timu za Waangalizi za AU, SADC na Jumuiya ya Madola waisifu Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Kiongozi wa Timu ya Waangalizi wa Uchaguzi Mkuu wa Tanzania kutoka Umoja wa Afrika (AU), ambaye pia ni Rais Mstaafu wa Msumbiji Mhe. Armando Emilio Guebuza, akitoa ripoti ya timu hiyo mbele ya Waandishi wa Habari na Mabalozi mbalimbali wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini  tarehe 27 Oktoba, 2015 katika Hoteli ya White Sands Jijini Dar es Salaam.
Pamoja na mambo mengine, timu hiyo ya Waangalizi ya Umoja wa Afrika (AU) imeisifu Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kwa kuendesha uchaguzi katika hali ya haki na uwazi bila upendeleo wowote.
Kamishna anayeshughulikia masuala ya Siasa katika Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Dkt. Aisha Abdulahi nae akizungumza wakati wa uwasilishaji ripoti ya Umoja huo kuhusu Uchaguzi Mkuu wa hapa nchini.
Baadhi ya Waheshimiwa Mabalozi  wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini wakimpigia makofi kiongozi wa timu ya Waangalizi ya Afrika Mhe. Armando Guebuza (hayupo pichani).
Kiongozi wa Timu ya Waangalizi wa Uchaguzi Mkuu kutoka  Jumuiya ya Madola, ambaye pia ni Rais Mstaafu wa Nigeria, Mhe. Goodluck Jonathan akitoa ripoti ya timu yake  mbele ya Waandishi wa Habari na Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini tarehe 27Oktoba, 2015 katika Hoteli ya White Sands jijini Dar es Salaam.
Mheshimiwa Goodluck Jonathan ameisifu Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Vyombo vya Dola, Wagombea, Viongozi wa vyama vya siasa pamoja na Watanzania wote kwa ujumla kwa kuendesha uchaguzi katika mazingira ya haki, uwazi na amani.
Mkurugenzi wa Idara ya Afrika, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Samwel Shelukindo (katikati), Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga (kulia) pamoja na Afisa wa Wizara hiyo Bw. Celestine Kakere, wakifuatilia ripoti hizo.
Baadhi ya Waheshimiwa Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini wakifuatilia ripoti ya kiongozi wa timu ya Waangalizi ya Jumuiya ya Madola Mhe. Goodluck Jonathan.
Wajumbe wa timu za Waangalizi wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC)Umoja wa Afrika (AU) na Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola nao wakifuatilia Ripoti ya Mhe. Goodluck Jonathan.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Msumbiji ambaye pia ndiye Kiongozi wa Timu ya Waangalizi wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), Mhe. Oldemiro Baloi naye akitoa taarifa ya timu yake ya uangalizi wa Uchaguzi Mkuu hapa nchini tangu kipindi cha kampeni hadi siku ya uchaguzi.

Baadhi ya Waheshimiwa Mabalozi  wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini wakifuatilia ripoti ya kiongozi wa timu ya waangalizi ya SADC.
Mkutano huo ukiendelea.
Waheshimiwa Mabalozi wakiendelea kufuatili uwasilishwaji wa ripoti hizo za waangalizi wa Kimataifa wa Uchaguzi Mkuu nchini Tanzania.

Mmoja wa Waandishi wa Habari akiuliza swali juu ya ripoti hizo.
Waandishi wa Habari wakiendelea kuwajibika kuchukua kila kinachoelezwa na timu hizo za kimataifa za waangalizi wa Uchaguzi Mkuu unaoendelea hapa nchini.
Mkutano ukiendelea.
===========================
PICHA NA: REUBEN MCHOME.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.