Wednesday, October 21, 2015

Waziri Membe akutana na Kiongozi wa Timu ya Waangalizi wa Uchaguzi Mkuu kutoka Umoja wa Afrika.

Kiongozi wa timu ya waangalizi wa Uchaguzi Mkuu kutoka Umoja wa Afrika (AU), ambaye pia ni Rais Mstaafu wa Msumbiji Mhe. Armando Emilio Guebuza akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe ambapo Waziri Membe alimueleza kiongozi huyo hali ya utulivu na amani inavyoendelea katika kipindi chote tangu kuanza kwa kampeni kuelekea siku ya uchaguzi mkuu hapo tarehe 25-10-2015.
Mkurugenzi wa Idara ya Afrika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Samwel William Shelukindo(kushoto) pamoja na baadhi ya wajumbe wa timu hiyo ya waangalizi wa Umoja wa Afrika wakifuatilia mazungumzo hayo.
Kiongozi wa timu ya waangalizi wa Uchaguzi Mkuu kutoka Umoja wa Afrika ambaye pia ni Rais Mstaafu wa Msumbiji Mhe. Armando Emilio Guebuza akisisitiza jambo katika mazungumzo hayo.
Msaidizi wa Waziri Bw. Thobias Makoba (katikati) pamoja na Ofisa wa Wizara ya Nje anayeshughulikia masuala ya Afrika Bi. Zuleha Tambwe wakifuatilia mazungumzo hayo.
Mhe. Membe akifurahia jambo na Mhe. Guebuza mara baada ya kumaliza Mazungumzo yao.

          Rais Mstaafu wa Msumbiji na Kiongozi wa timu ya waangalizi wa Uchaguzi Mkuu kutoka Umoja wa Afrika Mhe.    Armando Emilio Guebuza, akiagana na Mheshimiwa                         Membe mara baada ya Mazungumzo hayo.
                               =================
                         PICHA NA: REUBEN MCHOME.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.