Saturday, October 10, 2015

Rais Kikwete azindua Kiwanda cha Saruji kikubwa Afrika Mashariki na Kati.

Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Kiwanda cha Saruji kikubwa Afrika Mashariki na Kati cha Dangote Industries Limited kilichopo katika Kijiji cha Mgao Mkoani Mtwara, Tanzania. Kulia kwa Rais ni Mmiliki wa Kiwanda hicho, Alhaji Aliko Dangote na kushoto ni Mwakilishi wa Serikali ya Nigeria, Mallam Nasir Ahmad El-Rufai, Gavana wa Jimbo la Kaduna. Wengine ni Mke wa Rais Mama Salma Kikwete pamoja na wafanyibiashara kutoka nchini Nigeria nao wakishuhudia uzinduzi huo uliofanyika tarehe 10 Oktoba 2015.
Mheshimiwa Rais Dkt. Jakaya Kikwete akiweka saini kwenye kitabu cha wageni, muda mfupi baada ya kuzindua kiwanda hicho.
Mmiliki wa Kiwanda hicho, Alhaj Aliko Dangote, akifafanua jambo kwa Mheshimiwa Rais juu ya namna kiwanda hicho kinavyofanya kazi ya uzalishaji  wa saruji
Mheshimiwa Rais akipewa maelezo na mmoja wa wataalamu ya namna kiwanda hicho kinavyofanya uzalishaji wa saruji. 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete, akizungumza na Wafanyibiashara wa Tanzania na Nigeria pamoja na Wananchi waliojitokeza katika kushuhudia ufunguzi wa Kiwanda hicho cha pili kwa ukubwa Barani Afrika na cha kwanza kwa Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya Mheshimiwa Rais Kikwete kuzindua kiwanda hicho.
Moja ya sehemu ya muonekano wa kiwanda hicho cha Dangote Industries Limited Tanzania. 
Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete akizungumza jambo na mmiliki wa Kiwanda hicho, AlhajI Aliko Dangote.
Picha ya Pamoja.
=====================================
PICHA NA: Reuben Mchome.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.