Sunday, October 18, 2015

Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wamuaga Rais Kikwete





Picha zote za juu zikimuonesha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Viongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje wakati alipowasili kwenye Kituo cha Kimataifa cha cha Mikutano cha Julius Nyerere ambapo Wizara ya Mambo ya Nje ilifanya hafla ya kumuaga Mhe. Rais.

Rais Kikwete akifunua kitambaa ambapo nyuma yake kuna picha ya Jengo la Ofisi ya Wizara ya Mambo ya Nje linalokusudiwa kuanza kujengwa hivi karibuni. Rais Kikwete alifunua kitambaa hicho kuashiria kuanza ujenzi wa jengo hilo.


Rais Kikwete akipiga makofi kuonesha furaha yake kuwa Wizara ya Mambo ya Nje itapata ofisi za kisasa hivi karibuni

Rais Kikwete akiongozwa kuelekea ukumbi ulioandaliwa kwa ajili ya kufanya hafla ya kumuaga. Wanaomuongoza ni Waziri wa Mambo ya Nje na Uhirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe wa kulia kwa Rais Kikwete na Katibu Mkuu, Balozi Liberata Mulamula.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Bi. Mindi Kasiga akitoa neno la kuwakaribisha wageni waalikwa akiwemo Rais Kikwete katika hafla ya kumuaga.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Balozi Liberata Mulamula akitoa utambulisho wa wageni waalikwa wakiwemoWaheshimiwa Mabalozi waliostaafu.

Balozi Mstaafu akisalimia wajumbe baada ya kutambulishwa

Watumishi wa Wizara wakiwemo Wakuu wa Idara/Vitengo, Waheshimiwa Mabalozi wanaowakilisha Tanzania nje ya nchi wakiwa wameketi kwa ajili ya kushuhudia matukio ya hafla ya kumuaga Rais Kikwete.

Sehemu ya watumishi wa Wizara waliohudhuria hafla ya kumuaga Rais Kikwete

Watumishi wa Wizara katika hafla ya kumuaga Rais Kikwete

Mtumishi wa Wizara akisoma utenzi wa kumsifu na kumpongeza Rais Kikwete namna alivyoongoza Taifa la Tanzania kwa umahiri mkubwa katika kipindi chake cha miaka 10 ambacho kinakamilika Oktoba 2015.

Waziri wa Mambo ya Nje, Mhe. Bernard K.Membe akisoma hotuba yake katika hafla hiyo. Hotuba ya Waziri Membe iligusia mafaniki ambayo Serikali ya awamu ya nne imeyapata katika kipindi cha miaka 10 ikiwa ni pamoja na kuvutia wawekezaji wakubwa, kuongeza uwakilishi nje ya nchi,kujenga ofisi za kibalozi na utatuzi wa migogoro.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Waziri Membe wakionesha Tuzo aliyotunukiwa Rais Kikwte na Wizara ya Mambo ya Nje.



Picha za juu zinaonesha zawadi mbalimbali ambazo Rais Kikwete amekabidhiwa wakati wa hafla hiyo

Rais Kikwete akiongea na watumishi wa Wizara na wageni waalikwa. Katika mazungumzo yake Rais Kikwete alisisitiza umuhimu wa watumishi wa Wizara kudumuisha na kuimarisha mahusiano mazuri na nchi zote duniani. Alisema katika kipindi cha uongozi wake mafanikio makubwa ya kidiplomasia yamepatikana hivyo ni vyema watumishi wa Wizara wakayaendeleza kwa kiwango cha juu zaidi.

Picha ya pamoja kati ya Mhe. Rais Kikwete, Mhe. Waziri Membe, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje,Wakuu wa Idara/Vitengo na Waheshimiwa Mabalozi wa Tanzania nje ya nchi


Mhasibu Mkuu wa Wizara, Bw. Paul Kabale akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya  watumishi wa Kitengo cha Fedha na Uhasibu



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.