Wednesday, October 28, 2015

Rais Kikwete apokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Mabalozi wa Misri, Singapore, Israel na Ufilipino

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (kushoto) akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Ufilipino nchini Tanzania mwenye makazi nchini Kenya,  Mhe. Bayani V. Mangibin. Hafla hiyo imefanyika Ikulu Dar es Salaam tarehe 28 Oktoba, 2015. 
Balozi Mangibin akizaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Ikulu Jijini Dar es Salaam
Balozi Mangibin (kulia) akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberatta Mulamula (kushoto) mara baada ya kuwasilisha Hati za Utambulisho kwa Mhe. Rais Jakaya Kikwete (katikati mwenye tai nyekundu)
Balozi Mangibin (kulia) akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Khatibu Makenga (wa kwanza kushoto) alipokuwa akitambulishwa na Mhe. Rais. 
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga (wa kwanza kushoto) akisalimiana na Balozi Mangibin (kulia).
Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mangibin.
Picha ya pamoja

=========Balozi wa Singapore
Balozi wa Singapore nchini Tanzania, Mhe. Tan Puay Hiang akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Ikulu kwa ajili ya kuwasilisha Hati zake za Utambulisho kwa Mhe. Rais.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (kushoto) akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Singapore mwenye kazi yake nchini Singapore,  Mhe. Tan Puay Hiang (kulia)
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberatta Mulamula (kushoto) akisalimiana na Balozi Tan Puay Hiang (kulia)
Mhe. Rais Kikwete akizungumza na Balozi Hiang mara baada ya kupokea hati zake za utambulisho kama Balozi mpya wa Singapore hapa nchini. Kushoto ni Afisa aliyefuatana na Balozi Hiang.

.......Balozi wa Misri 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi mpya wa Misri hapa nchini, Mhe. Yasser Ahmed Al Eldin Elshawaf. Hafla hiyo imefanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 28 Oktoba, 2015.
Mhe. Rais Kikwete akimkaribisha Balozi Elshawaf.
Mhe. Rais Kikwete akimtambulisha kwa Balozi Elshawaf, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula.
Balozi Elshawaf akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Samwel Shelukindo 
Balozi Elshawaf akisalimiana na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. 
Picha ya pamoja
Mhe. Rais Kikwete akiwa kwenye mazungumzo na Balozi mpya wa Misri hapa nchini Mhe. Elshawaf
Mazungumzo yakiendelea

......Balozi wa Israel

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Balozi mpya wa Israel hapa nchini mwenye Makazi yake nchini Kenya, Mhe. Yahel Vilan mara baada ya kupokea Hati zake za utambulisho. Hafla hiyo imefanyika Ikulu, Dar es Salaam tarehe 28 Oktoba, 2015.
Mhe. Rais Kikwete akimtambulisha kwa Balozi Vilan, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula.
Balozi Vilan akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Elibariki Maleko.
Balozi Vilan akisalimiana na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga
Balozi Vilan akisalimiana na Bw. Batholomeo Jungu, Afisa Mambo ya Nje
Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Vilan
Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Vilan na Balozi Mulamula
Balozi Elshawaf (katikati) akipokea heshima ya wimbo wa taifa mara baada ya kuwasili Ikulu. Kulia ni Mkuu wa Itifaki Balozi Juma Maharage na kushoto Mnikulu.
Bendi ya polisi ikipiga wimbo wa taifa wa Misri kwa heshima ya Balozi Elshawaf
Balozi Elshawaf akisalimiana na Bw. Celestine Kakele, Afisa Mambo ya Nje
Balozi Elshawaf akisalimiana na Kiongozi wa Bendi ya Polisi
Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.