Tuesday, October 27, 2015

Mkataba wa Makubaliano kuhusu Misaada ya Kibinadamu kwa Wakimbizi huko Kigoma wasainiwa

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula kwa pamoja na Bw. Anton Breve, Naibu Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Madaktari wasio na Mipaka wakisaini Mkataba wa Makubaliano kuhusu Misaada ya Kibinadamu kwa Wakimbizi waliopo Kigoma. Uwekaji saini huo umefanyika Wizarani tarehe 27 Oktoba, 2015.
Balozi Mulamula na Bw. Breve wakibadilishana Mkataba huo wa Makubaliano mara baada ya kusainiwa
Balozi Mulamula akiwa kwenye mazungumzo na Bw. Breve kabla ya kusaini Mkataba wa Makubaliano kuhusu Misaada ya Kibinadamu kwa Wakimbizi waliopo Mkoani Kigom.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Baraka Luvanda (kushoto)  kwa pamoja na Maafisa katika Kitengo hicho Bw. Gerald Mbwafu (katikati) na Bw. Elisha Suku (kulia) wakifuatilia mazungumzo kati ya Balozi Mulamula na Bw. Breve (hawapo pichani). 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.