Tuesday, October 27, 2015

Jukwaa la Vijana wa ICGLR watembelea Wizara ya Mambo ya Nje

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula (katikati) akizungumza na wawakilishi kutoka Jukwaa la Vijana la Jumuiya ya Nchi za Ukanda wa  Maziwa Makuu (ICGLR Youth Forum) (hawapo pichani) walipofika Wizarani kwa lengo la kumsalimia na kumpongeza kwa kuteuliwa katika nafasi ya Katibu Mkuu. Timu  hiyo ya vijana  kutoka nchi wanachama wa Ukanda wa Maziwa Makuu ipo nchini kama Waangalizi wa Uchaguzi Mkuu wa Tanzania. Wengine katika picha ni Balozi Muburi Muita, Mkuu wa Msafara na Mratibu wa Kitaifa wa ICGLR nchini Kenya pamoja na Bi. Nancy Kaizilege.
Sehemu ya Vijana hao wakimsikiliza Balozi Mulamula (hayupo pichani). Vijana hao wanatoka nchi za Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Angola, Zambia, Sudan Kusini, Sudan, Tanzania na DRC.
Balozi Muburi nae akizungumza wakati wa mkutano kati ya Wawakilishi wa Jukwaa la Vjana wa ICGLR na Balozi Mulamula.
Sehemu nyingine ya vijana wakifuatilia mkutano wao na Balozi Mulamula (hayupo pichani)
Bi. Nancy nae akitoa maelezo mafupi kuhusu dhumuni la ziara ya Vijana hao hapa Wizarani.
Vijana wakifuatilia

Picha ya pamoja. 



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.