Friday, October 30, 2015

BALOZI DORA MSECHU ASHIRIKI KWENYE SHEREHE YA MIAKA 10 YA JUMUIYA YA WATANZANIA JIMBO LA FYN, DENMARK

Balozi Dora Msechu  amekutana na watanzania wanaoishi kwenye Jimbo la Fyn nchini Denmark na kuwapongeza kwa kutimiza miaka 10 ya Umoja wao. na kuwashukuru kwa mchango mkubwa wanaotoa kwenye maendeleo ya nchi yetu. Amewaasa waendeleze mshikamano wao na kuwahakikishia kuwa  milango ya Ubalozi ipo wazi katika kuwahudumia na kushirikiana kwa  karibu na watanzania wote wanaoishi kwenye nchi za Nordic na Baltic.

Sherehe hiyo iliandaliwa na Jumuiya ya Watanzania Jimbo la Fyn kwa kushirikiana na familia ya Bibi Dorthe Nielsen, rafiki mkubwa wa Tanzania na mtoto wa aliyekuwa Mwakilishi wa Heshima wa Tanzania nchini Denmark, marehemu Robert Andersson.





No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.