Wednesday, September 7, 2022

NORWAY KUONGEZA BAJETI YA KUTEKELEZA MIRADI MBALIMBALI NCHINI


Waziri wa Norway anayeshughulikia masuala ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa na nchi za Nordic Mhe. Anne Beathe Tvinnereim amesema Serikali ya Norway imeongeza bajeti ya kufadhili miradi mbalimbali ya kijamii na maendeleo nchini. 

Waziri Tvinnereim aliyeambatana na ujumbe wake amesema hayo alipozungumza na wakazi wa kijiji cha Chihembe kilichopo Mvumi-Chamwino jijini Dodoma. 

Akizungumza (Jumatano, Septemba 7, 20220) na Wananchi ambao ni wanufaika wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), Waziri Tvinnereim ametaja baadhi ya maeneo ambayo bajeti hiyo itaelekezwa kuwa ni kukabiliana na madiliko ya Tabia Nchi, kuongeza uzalishaji wa mazao ya chakula na mpango wa kunusuru kaya maskini nchini kupitia TASAF.

“Natambua na kupongeza kazi kubwa inayofanywa na Serikali ya Tanzania katika kuboresha maisha ya wananchi wake, hata hivyo Serikali ya Norway inatambua changamoto zinazoikabili dununi kwa sasa, kama vile vita vinaovyoendelea kati ya Urusi-Ukraine na COVID19 ambazo zimepelekea ongezeko la bei ya bidhaa muhimu ikiwemo chakula, mafuta na gesi kwa nchi nyingi duniani ikiwemo Tanzania, hivyo tumeona ni vyema tukaongeza bajeti ya kusaidia miradi na programu mbalimbali za kiuchumi na kijamii zinazotekelezwa Tanzania ili kuwawezesha wananchi huhimili gharama za maisha”

Kuhusu kusaidia kubabiliana na mabadiliko ya Tabia Nchi Waziri Tvinnereim, amesema Norway imesukumwa kusaidia eneo hilo kwa kutambua kuwa asilimia kubwa ya pato la Tanzania linachangiwa na sekta ya kilimo na wananchi wake wengi wamejiajiri katika sekta hiyo huku wakitegemea mvua kuendesha shughuli hizo. 

Ameongeza kuwa ni vyema kuhakikisha uzalishaji katika sekta ya kilimo hauathiriwi na hali ya hewa kwa kukabiliana na Mabadiko ya Tabia Nchi. 

Akiwa ziarani jijini Dodoma Waziri Tvinnereim amefanya shughuli mbalimbali ikiwemo kutembelea miradi inayotelezwa na TASAF katika eneo la Mvumi, wilayani Chamwino, sambamba na kutembelea wanufaika wa mpango wa kunusuru kaya maskini na kuzungumza na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Dkt. Selemani Jafo na Uongozi wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI). 

Waziri Tvinnereim na ujumbe wake ambaye pia ameambatana Balozi wa Tanzania nchini Sweden Mhe. Grace Martini yuko nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tatu.
Waziri wa Norway anayeshughulikia masuala ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa na nchi za Nordic Mhe. Anne Beathe Tvinnereim akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watendaji wa Serikali walipotembelea mradi wa bwawa uliotekelezwa na TASAF katika eneo la Mvumi jijini Dodoma
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Dkt. Selemani Jafo na Waziri wa Norway anayeshughulikia masuala ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa na nchi za Nordic Mhe. Anne Beathe Tvinnereim na ujumbe wake wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watendaji wa Serikali alipomtembelea ofisini kwake jijini Dodoma
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule na Waziri wa Norway anayeshughulikia masuala ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa na nchi za Nordic Mhe. Anne Beathe Tvinnereim na ujumbe wake wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watendaji wa Serikali alipomtembelea ofisini kwake jijini Dodoma.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule akiwa na Waziri wa Norway anayeshughulikia masuala ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa na nchi za Nordic Mhe. Anne Beathe Tvinnereim alipomtembelea ofisini kwake jijini Dodoma.
Waziri wa Norway anayeshughulikia masuala ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa na nchi za Nordic Mhe. Anne Beathe Tvinnereim akifurahia jambo na Bi. Agness Mkunya mkazi wa Mvumi jijini Dodoma alipomtembelea nyumbani kwake.
Waziri wa Norway anayeshughulikia masuala ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa na nchi za Nordic Mhe. Anne Beathe Tvinnereim akiwa katika mitaa ya Mvumi jijini Dodoma alipotembelea miradi inayo tekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF)
Waziri wa Norway anayeshughulikia masuala ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa na nchi za Nordic Mhe. Anne Beathe Tvinnereim akizungumza na wananchi wa kijiji cha Chihembe-Mvumi jijini Dodoma.
Waziri wa Norway anayeshughulikia masuala ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa na nchi za Nordic Mhe. Anne Beathe Tvinnereim akisalimiana na Bi. Agness Mkunya mkazi wa Mvumi jijini Dodoma alipomtembelea nyumbani kwake.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Dkt. Selemani Jafo akisalimiana na Waziri wa Norway anayeshughulikia masuala ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa na nchi za Nordic Mhe. Anne Beathe Tvinnereim alipowasili ofisini kwake jijini Dodoma

WAZIRI MULAMULA AKUTANA NA MABALOZI WA UTURUKI, ETHIOPIA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) kwa nyakati tofauti amekutana kwa mazungumzo na Balozi wa Uturuki nchini, Mhe. Dkt. Mehment Gulluoglu na Balozi wa Ethiopia nchini, Mhe. Shibru Mamo Kedida tarehe 7 Septemba 2022 katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam. 

Akiongea na Dkt. Gulluoglu Waziri Mulamula amesema  Tanzania itaendelea kushirikiana na Uturuki katika masuala ya biashara, masoko, kilimo, uwekezaji, utalii, madini na uchumi wa bluu.

Naye Balozi wa Uturuki nchini, Mhe. Dkt. Mehment Gulluoglu ameeleza kuwa katika kipindi chake cha uwakilishi anafanya jitihada za makusudi kuhakikisha Mkutano wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Uturuki unafanyika ili kuongeza nguvu ya utekelezaji katika maeneo ya ushirikiano yaliyokubaliwa.

Katika tukio jingine, Waziri Mulamula amemhakikishia Balozi wa Ethiopia nchini, Mhe. Kedida kuwa Tanzania itaendeleza ushirikiano wa muda mrefu na wa kihistoria ulioasisiwa na waasisi wa mataifa yao ili kufikia malengo ya utekelezaji wa diplomasia ya uchumi.

Ameongeza kuwa Tanzania itaendelea kuzingatia utekelezaji wa makubaliano mbalimbali yanayofikiwa katika Umoja wa Afrika hususan umuhimu wa mto Nile na manufaa yake katika sekta za kilimo na huduma nyingine za kijamii.

Naye Mhe. Kedida amemueleza Waziri Mulamula kuwa Ethiopia itaendeleza jitihada za kukuza ushirikiano katika maeneo mbalimbali ikiwemo kusimamia makubaliano yaliyoanzishwa kati ya Tanzania na Ethiopia hususan ushirikiano kati ya Shirika la Utangazaji la Tanzania na Shirika la Utangazaji la Ethiopia pamoja na ushirikiano kati ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Chuo Kikuu cha Ethiopia.

=======================================

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Balozi wa Uturuki nchini, Mhe. Dkt. Mehment Gulluoglu tarehe 07 Septemba 2022 katika ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam.

Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Swahiba Mndeme na maafisa kutoka Wizara hiyo wakifuatilia mazungumzo.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akisalimiana na Balozi wa Uturuki nchini, Mhe. Dkt. Mehment Gulluoglu katika ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam.

Picha ya pamoja
==================================

Wakati huohuo Waziri Mulamula alikutana kwa mazungumzo na Balozi wa Ethiopia nchini, Mhe. Shibru Mamo Kedida.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Balozi wa Ethiopia nchini, Mhe.Shibru Mamo Kedida katika ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam.

Watumishi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia mazungumzo.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiteta jambo na Mhe. Kedida katika ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam.





BALOZI SOKOINE AKUTANA NA MKUU WA IDARA YA UHAMIAJI WA SAUDI ARABIA

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine amekutana kwa mazungumzo na Mkuu wa Idara ya Uhamiaji wa Ufalme wa Saudi Arabia Luteni Generali Suliman Al-Yahya katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

Pamoja na Mambo mengine, viongozi hao wamejadili masuala mbalimbali ya kukuza ushirikiano baina ya pande hizo mbili ambapo Saudi Arabia imeonyesha utayari wa kujadiliana na Serikali ya Tanzania kuhusu masuala ya upatikanaji wa viza za kuingia nchini Saudi Arabia.

Kwa upande wake, Balozi Sokoine ameishukuru Serikali ya Saudi Arabia kwa ushirikiano wake kwa Tanzania katika nyanja mbalimbali.

Balozi Sokoine ametumia mazungumzo hayo kuelezea utayari wa Tanzania kuingia makubaliano ya kuanzishwa Tume ya Kudumu ya Pamoja (JPC) kati ya nchi hizi mbili katika kusimamia utekelezaji wa masuala mbalimbali ya ushirikiano.

Ujumbe wa Saudi Arabia ukiongozwa na Mkuu wa Idara ya Uhamiaji, Luteni Generali Suliman Al-Yahya ukijitambulisha wakati wa kikao baina yake na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Kikao baina ya Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine na Mkuu wa Idara ya Uhamiaji wa Ufalme wa Saudi Arabia Luteni Generali Suliman Al-Yahya kikiendelea katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine amekutana kwa mazungumzo na Mkuu wa Idara ya Uhamiaji wa Ufalme wa Saudi Arabia Luteni Generali Suliman Al-Yahya kikiendelea katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Mkuu wa Idara ya Uhamiaji wa Ufalme wa Saudi Arabia Luteni Generali Suliman Al-Yahya akieleza jambo wakati wa kikao chake na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Mkuu wa Idara ya Uhamiaji wa Ufalme wa Saudi Arabia Luteni Generali Suliman Al-Yahya akipokea zawadi ya picha kutoka kwa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine  

Ujumbe wa Tanzania ukiwa katika picha ya pamoja na Ujumbe wa Saudi Arabia


BAKITA YATOA VITABU 1,650 VYA KISWAHILI KWA UBALOZI WA TANZANIA UJERUMANI

Katika jitihada za kukuza na kueneza lugha ya Kiswahili Duniani Baraza la Kiswahili Tanzania (BAKITA) limetoa vitabu 1,650 vya Kiswahili  vitakavyotumiwa na vyuo, vituo na taasisi zinazojishughulisha na ufundishaji wa lugha ya Kiswahili nchini  Ujerumani.

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano ya vitabu hivyo, iliyofanyika jijini Dar es Salaam,  Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine ameipongeza BAKITA kwa kuunga mkono jitihada za Serikali ya katika kubidhaisha lugha ya Kiswahili katika ukanda wa Kimataifa.

“Naamini kuwa BAKITA itaendelea kufungua mlango kwa ajili ya maombi ya vitabu vya kufundishia lugha ya Kiswahili katika nchi rafiki na nchi nyingine zote duniani ambazo zitaonesha nia ya kufundisha raia wake lugha adhimu ya Kiswahili, alisema Balozi Sokoine

Alisema kuwa juhudi hizo ni muhimu sana wakati huu kwa kuwa Shirika la UNESCO liliipitisha tarehe 7 Julai ya kila mwaka kuwa siku ya Kiswahili duniani, huku SADC, EAC na AU pia zilipitisha lugha ya Kiswahili kuwa miongoni mwa lugha rasmi zinazotumika katika utendaji kazi wa mitangamano hii na kuongeza kuwa kwa sasa ni dhahiri kuwa lugha ya kiswahili itakuwa kwa kasi na mahitaji ya vitabu na zana nyingine za kufundishia yataongezeka pia

"Kitendo hiki ni muhimu sana hasa ikizingatiwa kuwa  UNESCO iliipitisha tarehe 7 Julai ya kila mwaka kuwa siku ya Kiswahili duniani, SADC, EAC na AU nazo zilipitisha lugha ya Kiswahili kuwa miongoni mwa lugha rasmi za kazi, ni dhahiri kuwa lugha hii sasa itakuwa kwa kasi na hivyo, mahitaji ya vitabu na zana nyingine za kufundishia yataongezeka,” amesema Balozi Sokoine.

Naye Naibu katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Saidi Yakubu amesema uchapishwaji wa vitabu hivyo utasaidia kukuza lugha ya kiswahili nchini Ujeremani pamoja na mataifa mengine ya jirani.

Akizungumza katika hafla hiyo Katibu Mtendaji wa BAKITA Bi. Consolata Mushi ameahidi kuwa wataendelea kushirikiana na Serikali katika kuendelea kubidhaisha lugha ya Kiswahili kimataifa zaidi.

“BAKITA katika kutekeleza majukumu yake ya kisheria na mkakati wa taifa wa kubidhaisha Kiswahili itaendelea kusambaza vitabu katika balozi mbalimbali za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zikiwemo Urusi, Uholanzi, Afrika Kusini, Burundi, Namibia, Korea Kusini, Nigeria na Mauritius,” amesema Bi. Mushi

Ameongeza kuwa BAKITA imetoa vitabu hivyo ikishirikiana na wachapishaji wa vitabu kutoka kampuni mbalimbali kwa lengo la kubidhaisha lugha ya Kiswahili na kutangaza soko jipya la vitabu katika nchi za Ulaya ikilenga kuwasaidia walimu wanaofundisha Kiswahili ambao ni Wadachi wenye nasaba na Waswahili pamoja na Diaspora wa Tanzania ambao wameanza kufundisha Kiswahili.

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine pamoja na Naibu katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Saidi Yakubu wakimsikiliza Katibu Mtendaji wa (BAKITA), Bi. Consolata Mushi alipokuwa akitoa maelezo kuhusu ukumbi unaotumika kwa tafsiri za lugha mbalimbali katika taasisi hiyo

Katibu Mtendaji wa (BAKITA), Bi. Consolata Mushi akitoa hotuba yake wakati wa hafla ya makabidhiano ya nakala 1,650 za vitabu vitakavyotumiwa na vyuo, vituo na taasisi zinazojishughulisha na lugha ya Kiswahili Ujerumani 

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine (katikati) akiwasilisha hotuba yake wakati wa hafla ya makabidhiano ya nakala 1,650 za vitabu vitakavyotumiwa na vyuo, vituo na taasisi zinazojishughulisha na lugha ya Kiswahili Ujerumani 

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine akiangalia moja kati ya Vitabu vilivyotolewa na BAKITA kwa Ubalozi wa Tanzania nchini Ujerumani. Wengine ni Naibu katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Saidi Yakubu (kulia) pamoja na Katibu Mtendaji wa (BAKITA), Bi. Consolata Mushi (kushoto)

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine akipokea boksi la Vitabu vilivyotolewa na BAKITA kwa Ubalozi wa Tanzania nchini Ujerumani kutoka kwa Naibu katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Saidi Yakubu pamoja na Katibu Mtendaji wa (BAKITA), Bi. Consolata Mushi

Meza Kuu katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa BAKITA


TANZANIA, NORWAY KUSHIRIKIANA KUIMARISHA UCHUMI

Serikali za Tanzania na Norway zimesisitiza kuendelea kuimarisha ushirikiano baina ya nchi hizo ili kukuza uchumi.

Msisitizo huo umetolewa wakati wa mazungumzo ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb.) na Waziri wa Norway anayeshughulikia masuala ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa na nchi za Nordic, Mhe. Anne Beathe Tvinnereim walipokutana tarehe 06 Septemba 2022 katika ofisi ndogo za wizara Jijini Dar es Salaam.

Nchi hizo zinashirikiana katika masuala ya elimu, afya, kilimo, uwekezaji, miundombinu, nishati, madini, tehama, utafiti, maboresho kwenye mifumo ya ukusanyaji wa kodi, uchangiaji wa bajeti kuu ya Serikali, misitu, demokrasia, haki za binadamu, usawa wa jinsia, utunzaji wa mazingira na ukuzaji wa sekta ya biashara.

Balozi Mulamula alieleza kuwa Tanzania inathamini ushirikiano uliopo baina yake na Norway kwa kusimamia miradi ya maendeleo iliyo kwenye makubaliano na kuongeza maeneo mapya ya ushirikiano kwa lengo la kujenga uchumi wa Wananchi.

“Norway ni mshirika wa maendeleo wa Tanzania wa muda mrefu na imesaidia kujenga uwezo katika maeneo mbalimbali ya kiutendaji ikiwemo uboreshaji wa mazingira wezeshi ya uwekezaji na biashara, usimamizi wa mfumo wa ulipaji kodi,” alisema Balozi Mulamuala.

Kadhalika, Serikali ya Norway imeongeza muda wa miaka mitano ya utekelezaji wa makubaliano ya majadiliano ya kisiasa yaliyoingiwa kati yake na Tanzania yanaendelea ili kuimarisha ushirikiano katika maeneo ya kipaumbele ya Serikali ya awamu ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Kwa upande wake Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Dkt. Doroth Gwajima alieleza kuwa Tanzania ipo tayari kushirikiana na Norway katika utekelezaji wa pendekezo la mpango wa miaka mitano wa kujenga usawa na uwezo kwa wanawake, vijana na makundi maalum unaotegemewa kuinua uchumi na kuwawezesha kuajiriwa na kujiajiri katika kazi rasmi. 

Mpango huo pia umezingatia umuhimu wa  afya ya uzazi kuwa agenda muhimu ili kuyafikia Malengo ya Mpango wa Maendeleo Endelevu.

Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Antony Mavunde alieleza kuwa kupitia sekta ya kilimo Tanzania inayo nia ya kushirikiana na Norway katika masuala ya kujenga uwezo katika vyuo vya kilimo na taasisi zake ili kuwezesha tafiti za sekta hiyo kwa lengo la kuinua uwezo binafsi wa kuzalisha mbegu za mazao, kusimamia usalama wa chakula nchini, kujenga mabwawa na kuimarisha miradi ya umwagiliaji.

Maeneo mengine ya ushirikiano ni pamoja na upatikanaji wa mbolea kwa gharama nafuu, uimarishaji na ujenzi wa miundominu ya kilimo ili kujenga uwezo wa kuzalisha kwa mwaka mzima badala ya kusubiri msimu wa mvua kama ilivyosasa.

Vilevile Wizara ya Kilimo imeandaa mpango wa miradi ya kilimo kwa Wanawake na Vijana itakayotekelezwa katika mikoa ya Mbeya na Dodoma ambapo mradi huo utatumia jumla ya ekari 69 hivyo, kupitia ushirikiano uliopo Tanzania ina dhamira ya dhati ya kushirikiana na Norway ili kuyafikia malengo ya uzalishaji yaliyowekwa katika kufanya kilimo cha biashara na kulifikia soko la kimataifa.

Naye Mhe. Tvinnereim ameeleza kuwa Norway imejenga uwezo mkubwa katika masuala ya uzalishaji wa mbegu hivyo itaendelea kushirikiana na Tazania katika eneo hilo na maeneo mengine yaliyoelezwa na mawaziri walioshiriki mazungumzo hayo kwa lengo la kuondoa umasikini, kuongeza nafasi za ajira na kujenga uwezo wa kiuchumi kwa wananchi.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Kushoto) akizungumza na ujumbe wa Norway ulioongozwa na Waziri wa Norway anayeshughulikia masuala ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa na nchi za Nordic, Mhe. Anne Beathe Tvinnereim katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Doroth Gwajima (Kushoto) akizungumza na ujumbe wa Norway ulioongozwa na Waziri wa Norway anayeshughulikia masuala ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa na nchi za Nordic, Mhe. Anne Beathe Tvinnereim katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Norway anayeshughulikia masuala ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa na nchi za Nordic, Mhe. Anne Beathe Tvinnereim (Kulia) akizungumza na ujumbe wa Tanzania  ulioongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Antony Mavunde akieleza jambo wakati wa mkutano baina ya  Balozi Mulamula na Waziri wa Norway anayeshughulikia masuala ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa na nchi za Nordic, Mhe. Anne Beathe Tvinnereim katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Waziri wa Norway anayeshughulikia masuala ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa na nchi za Nordic, Mhe. Anne Beathe Tvinnereim akipokea zawadi ya picha ya Mlima Kilimanjaro kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Ujumbe wa Tanzania ukiwa katika picha ya pamoja na Ujumbe wa Norway


Tuesday, September 6, 2022

NAFASI ZA KAZI SHIRIKA LA HALI YA HEWA DUNIANI


 

NAFASI ZA KAZI UMOJA WA AFRIKA

 


WAZIRI WA MAMBO YA NJE NORWAY AWASILI NCHINI KWA ZIARA YA SIKU TATU

Waziri wa Mambo ya Nje wa Norway anayeshughulikia masuala ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa na nchi za Nordic, Mhe. Anne Beathe Tvinnereim amewasili nchini leo kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kuanzia tarehe 6 - 8 Septemba 2022 na kupokelewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula.

Akiwa nchini Mhe. Tvinnereim kwa nyakati tofauti, atakutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais – Muungano na Mazingira, Dkt. Selemani Jaffo na Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Anthony Mavunde.

Aidha, Mhe. Tvinereim pia anataraji kutembelea miradi ya Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini (TASAF)  pamoja na Mji wa Serikali (Mtumba) Jijini Dodoma ili kujionea maendeleo ya miradi  sambamba na mikakati ya Serikali katika kufanikisha miradi hiyo. 

Tanzania na Norway zinashirikiana katika sekta za elimu, afya, kilimo, uwekezaji, miundombinu, nishati, madini, tehama, utafiti, maboresho kwenye mifumo ya ukusanyaji wa kodi, uchangiaji wa bajeti kuu ya Serikali, misitu, demokrasia, haki za binadamu, usawa wa jinsia, utunzaji wa mazingira na ukuzaji wa sekta ya biashara. 

Maeneo mengine mtambuka ya ushirikiano ni pamoja na masuala ya mabadiliko ya tabia nchi, utawala bora, usimamizi wa migogoro, amani na ulinzi.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akimpokea Waziri wa Mambo ya Nje wa Norway anayeshughulikia masuala ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa na nchi za Nordic, Mhe. Anne Beathe Tvinnereim alipowasili nchini leo kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kuanzia tarehe 6 - 8 Septemba 2022
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Norway anayeshughulikia masuala ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa na nchi za Nordic, Mhe. Anne Beathe Tvinnereim leo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam 

Waziri wa Mambo ya Nje wa Norway anayeshughulikia masuala ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa na nchi za Nordic, Mhe. Anne Beathe Tvinnereim akimueleza jambo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula leo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam 



TANZANIA, NORWAY KUSHIRIKIANA KUIMARISHA UCHUMI


Serikali za Tanzania na Norway zimesisitiza kuendelea kuimarisha ushirikiano baina ya nchi hizo ili kukuza uchumi.

Msisitizo huo umetolewa wakati wa mazungumzo ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb.) na Waziri wa Norway anayeshughulikia masuala ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa na nchi za Nordic, Mhe. Anne Beathe Tvinnereim walipokutana tarehe 06 Septemba 2022 katika ofisi ndogo za wizara Jijini Dar es Salaam.

Nchi hizo zinashirikiana katika masuala ya elimu, afya, kilimo, uwekezaji, miundombinu, nishati, madini, tehama, utafiti, maboresho kwenye mifumo ya ukusanyaji wa kodi, uchangiaji wa bajeti kuu ya Serikali, misitu, demokrasia, haki za binadamu, usawa wa jinsia, utunzaji wa mazingira na ukuzaji wa sekta ya biashara.

Balozi Mulamula alieleza kuwa Tanzania inathamini ushirikiano uliopo baina yake na Norway kwa kusimamia miradi ya maendeleo iliyo kwenye makubaliano na kuongeza maeneo mapya ya ushirikiano kwa lengo la kujenga uchumi wa Wananchi.

“Norway ni mshirika wa maendeleo wa Tanzania wa muda mrefu na imesaidia kujenga uwezo katika maeneo mbalimbali ya kiutendaji ikiwemo uboreshaji wa mazingira wezeshi ya uwekezaji na biashara, usimamizi wa mfumo wa ulipaji kodi,” alisema Balozi Mulamuala.

Kadhalika, Serikali ya Norway imeongeza muda wa miaka mitano ya utekelezaji wa makubaliano ya majadiliano ya kisiasa yaliyoingiwa kati yake na Tanzania yanaendelea ili kuimarisha ushirikiano katika maeneo ya kipaumbele ya Serikali ya awamu ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Kwa upande wake Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Dkt. Doroth Gwajima alieleza kuwa Tanzania ipo tayari kushirikiana na Norway katika utekelezaji wa pendekezo la mpango wa miaka mitano wa kujenga usawa na uwezo kwa wanawake, vijana na makundi maalum unaotegemewa kuinua uchumi na kuwawezesha kuajiriwa na kujiajiri katika kazi rasmi. 

Mpango huo pia umezingatia umuhimu wa afya ya uzazi kuwa agenda muhimu ili kuyafikia Malengo ya Mpango wa Maendeleo Endelevu.

Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Antony Mavunde alieleza kuwa kupitia sekta ya kilimo Tanzania inayo nia ya kushirikiana na Norway katika masuala ya kujenga uwezo katika vyuo vya kilimo na taasisi zake ili kuwezesha tafiti za sekta hiyo kwa lengo la kuinua uwezo binafsi wa kuzalisha mbegu za mazao, kusimamia usalama wa chakula nchini, kujenga mabwawa na kuimarisha miradi ya umwagiliaji.

Maeneo mengine ya ushirikiano ni pamoja na upatikanaji wa mbolea kwa gharama nafuu, uimarishaji na ujenzi wa miundominu ya kilimo ili kujenga uwezo wa kuzalisha kwa mwaka mzima badala ya kusubiri msimu wa mvua kama ilivyosasa.

Vilevile Wizara ya Kilimo imeandaa mpango wa miradi ya kilimo kwa Wanawake na Vijana itakayotekelezwa katika mikoa ya Mbeya na Dodoma ambapo mradi huo utatumia jumla ya ekari 69 hivyo, kupitia ushirikiano uliopo Tanzania ina dhamira ya dhati ya kushirikiana na Norway ili kuyafikia malengo ya uzalishaji yaliyowekwa katika kufanya kilimo cha biashara na kulifikia soko la kimataifa.

Naye Mhe. Tvinnereim ameeleza kuwa Norway imejenga uwezo mkubwa katika masuala ya uzalishaji wa mbegu hivyo itaendelea kushirikiana na Tazania katika eneo hilo na maeneo mengine yaliyoelezwa na mawaziri walioshiriki mazungumzo hayo kwa lengo la kuondoa umasikini, kuongeza nafasi za ajira na kujenga uwezo wa kiuchumi kwa wananchi.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Kushoto) akizungumza na ujumbe wa Norway ulioongozwa na Waziri wa Norway anayeshughulikia masuala ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa na nchi za Nordic, Mhe. Anne Beathe Tvinnereim katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Doroth Gwajima (Kushoto) akizungumza na ujumbe wa Norway ulioongozwa na Waziri wa Norway anayeshughulikia masuala ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa na nchi za Nordic, Mhe. Anne Beathe Tvinnereim katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam
Waziri wa Norway anayeshughulikia masuala ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa na nchi za Nordic, Mhe. Anne Beathe Tvinnereim (Kulia) akizungumza na ujumbe wa Tanzania  ulioongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam
Waziri wa Norway anayeshughulikia masuala ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa na nchi za Nordic, Mhe. Anne Beathe Tvinnereim akipokea zawadi ya picha ya Mlima Kilimanjaro kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam





Monday, September 5, 2022

TANZANIA, VENEZUELA ZASAINI HATI ZA MAKUBALIANO YA USHIRIKIANO

Serikali ya Tanzania na Serikali ya Venezuella zimesaini Hati za Makubaliano ya kuanzisha uhusiano wa kisiasa na mkataba wa ushirikiano katika nyanja mbalimbali baina ya nchi hizo. 

Makubaliano hayo yamesainiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb.), pamoja na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Venezuela anayeshughulikia masuala ya Afrika, Mhe. Yuri Pimentel Moura katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

“Tumesaini mikataba miwili ambapo mmoja unalenga kuendeleza majadiliano ya kisiasa (political consultation) lakini pia makubaliano ya kuwa na ushirikiano katika nyanja mbalimbali ikiwemo kichumi, nishati, afya, elimu na kilimo,” amesema Balozi Mulamula.

Kusainiwa kwa mikataba hiyo ni ishara ya kuimarika kwa uhusiano kati ya Tanzania na Venezuela katika sekta za nishati, afya, elimu na kilimo kwa maslahi mapana ya pande zote mbili.

Naye Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Venezuela anayeshughulikia masuala ya Afrika, Mhe. Yuri Pimentel Moura amesema kusainiwa kwa mikataba hiyo miwili ni hatua muhimu ya kudumisha na kuendeleza ushirikiano katika nyanja mbalimbali baina ya Venezuela na Tanzania.

Mhe. Moura amewasili nchini leo akitokea Venezuela na atakuwepo nchini kwa siku mbili kwa ziara ya kikazi. 

Katika tukio jingine, Balozi Mulamula amekutana na kupokea barua za utambulisho kutoka kwa Konseli Mkuu wa Kenya mwenye makazi yake Arusha, Bw. Dennis Mburu katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

Baada ya kupokea barua za utambulisho kutoka kwa Bw. Mburu Balozi Mulamula amemuahidi ushirikiano kutoka Serikalini wakati wote wa utekelezaji wa majukumu yake hapa nchini.

Pamoja na mambo mengine, viongozi hao wamejadili masuala ya biashara na uwekezaji pamoja na utalii.  

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Venezuela anayeshughulikia masuala ya Afrika, Mhe. Yuri Pimentel Moura katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika (kushoto), Balozi Swahiba Mndeme pamoja na Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali Balozi Mindi Kasiga (kulia) wote kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia kikao cha Mhe. Balozi Mulamula na Mhe. Moura katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula pamoja na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Venezuela anayeshughulikia masuala ya Afrika, Mhe. Yuri Pimentel Moura kwa pamoja wakisaini Hati za Makubaliano ya kuanzisha uhusiano wa kisiasa na mkataba wa ushirikiano katika nyanja mbalimbali baina ya nchi hizo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam. Utiaji saini Hati hizo umeshuhudiwa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda wengine ni  Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Balozi Swahiba Mndeme, Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Balozi Mindi Kasiga wote kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki 



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akipokea barua za utambulisho kutoka kwa Konseli Mkuu wa Kenya mwenye makazi yake Arusha, Bw. Dennis Mburu katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam
 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula katika picha ya pamoja na Konseli Mkuu wa Kenya mwenye makazi yake Arusha, Bw. Dennis Mburu. wengine pichani niMkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Balozi Mindi Kasiga na Maafisa waandamizi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki pamoja na Ubalozi wa Kenya nchini katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.