Wednesday, November 14, 2012

Congratulatory message on the occassion of the Belgium National Day


Jakaya Kikwete - Doug Pitt Named Goodwill Ambassador Of Tanzania Hosted by President Kikwete


PRESS RELEASE

H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to His Majesty King Albert II, King of the Belgians following the occasion of the National Day of the Kingdom of Belgium on 15th November, 2012.
The message reads as follows;

“His Majesty King Albert II,
 King of the Belgians,
 Brussels,
 BELGIUM.

Your Majesty,

On behalf of the Government and the people of the United Republic of Tanzania, and on my own behalf, it gives me great pleasure to congratulate you most sincerely on the occasion of the National Day of the Kingdom of Belgium.

              Belgium and Tanzania have over the years enjoyed good bilateral relations. The celebration of your country’s National Day offers me yet another opportunity to reaffirm our commitment to continue working closely with you in further consolidating and strengthening the ties of friendship, cooperation and partnership between the Kingdom of Belgium and the United Republic of Tanzania.

            Please accept, Your Majesty, my best wishes for your personal good health and prosperity for the people of Belgium”.


ISSUED BY: MINISTRY OF FOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL CO-OPERATION,
DAR ES SALAAM.
14TH NOVEMBER, 2012.


Katibu Mkuu akutana na Mjumbe Maalum kutoka Argentina

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John M. Haule, akipokea Ujumbe Maalum kutoka Serikali ya Argentina kwa niaba ya Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kutoka kwa Balozi Bibiana Jones. Balozi Jones ni Mkurugenzi wa Idara ya Afrika anayeshughulikia nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Argentina.

Bw. Haule akizungumza na Balozi Jones mara baada ya kupokea Ujumbe Maalum.

Balozi Jones akifafanua jambo kwa Bw. Haule wakati wa mazungumzo yao.

Katibu Mkuu, Bw. Haule akiendelea na mazungumzo na Balozi Jones kuhusu ushirikiano baina ya Tanzania na Argentina. Mwingine katika picha ni Balozi Dora Msechu, Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Katibu Mkuu akimsikiliza Balozi Jones wakati wa mazungumzo yao huku Balozi Msechu na Bi. Upendo Mwasha, Afisa katika Idara ya Ulaya na Amerika wakishuhudia.

Saturday, November 10, 2012

Ushirikiano kati ya Tanzania na China wazidi kuimarika: Wizara ya Mambo ya Nje na Tume ya Mipango zajadili miradi na Serikali ya China

Kaimu Katibu Mkuu katika Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bw. Longinus Rutasitara (katikati) akifafanua jambo wakati wa mkutano na Wajumbe kutoka Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China na wadau wengine (hawapo pichani) kujadili misaada ya Serikali ya China katika kuisadia Tanzania kutekeleza miradi mikubwa katika sekta kama vile Kilimo, Miundombinu na Umeme. Wengine katika picha ni Maafisa Waandamizi kutoka Tume hiyo.

Balozi Mbelwa Kairuki (kulia), Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akitoa mchango wake wakati wa majadiliano na ujumbe kutoka Serikali ya China kuhusu kuisaidia Tanzania kutekeleza miradi yake mikubwa. Wengine katika picha ni Bw. Lin Zhiyong (katikati) Mwakilishi Mkuu katika masuala ya Uchumi na Biashara wa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China hapa nchini na Bi. Fang Wang, Afisa kutoka Ofisi hiyo.

Bw. Lin Zhiyong akitoa maoni yake wakati wa majadiliano hayo.

Balozi Kairuki na wajumbe kutoka China wakimsikiliza Kaimu Katibu Mtendaji, Bw. Rutasitara (hayupo pichani) wakati wa majadiliano. Wengine katika picha ni Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Tume ya Mipango walioshiriki mkutano huo.

Bw. Rutasitara na Maafisa wengine wakimsikiliza Bw. Li wakati wa majadiliano hayo.

Thursday, November 8, 2012

Ushirikiano kati ya Tanzania na China wazidi kukua; Rais Kikwete azinduzia bomba la gesi asilia



Rais Kikwete azindua Ujenzi wa Bomba la Gesi Asilia kutoka Mkoani Mtwara hadi Dar es Salaam


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizindua rasmi ujenzi wa bomba la gesi asilia linalotoka Mkoani Mtwara hadi Dar es Salaam katika maeneo ya Kinyerezi, leo jijini Dar es Salaam.  Akishuhudia uzinduzi huo (kushoto) ni Makamu wa Rais, Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal.  


Rais Kikwete, Makamu wa Rais Dkt. Bilal na viongozi wengine wakimsikiliza Mhe. Profesa Sospeter Muhongo (Mb), Waziri wa Nishati na Madini ambaye alikuwa akielezea kuhusu miundombinu ya bomba la gesi la asilia. 


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wa kampuni inayojenga bomba la gesi asilia kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam, Benki ya Exim ya China na viongozi waandamizi wa Serikali akiwemo Balozi Dkt. Philip S. Marmo (wa pili kulia - mstari wa mbele), Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini China.  Rais Kikwete aliwakaribisha Ikulu kwa mazungumzo baada ya uzinduzi rasmi wa ujenzi wa bomba hilo maeneo ya Kinyerezi, jijini Dar es Salaam.



Picha zote kwa hisani ya      www.issamichuzi.blogspot.com







Wednesday, November 7, 2012

Rais Kikwete ametuma salamu za pongezi kwa Rais Obama


Jakaya Kikwete - Doug Pitt Named Goodwill Ambassador Of Tanzania Hosted by President Kikwete 



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ameeleza furaha na shangwe yake kufuatia ushindi wa jana, Jumanne, Novemba 6, 2012 wa Rais Barack Obama wa Marekani katika Uchaguzi Mkuu wa nchi hiyo.




Katika salamu zake za pongezi kwa kiongozi huyo wa Marekani ambaye amechaguliwa tena na wananchi wa nchi hiyo kwa kipindi cha pili, Rais Kikwete amesema mapema leo, Jumatano, Novemba 7, 2012:


Obama
Rais Barack Obama akisheherekea ushindi wake
dhidi ya mpinzani wake, Bw. Mitt Romney, na kuwa
Rais wa Marekani kwa kipindi cha pili.

“Nimepokea kwa furaha na shangwe habari za kuchaguliwa tena kwako kuwa Rais wa Marekani kwa kipindi cha pili. Kwa niaba ya Serikali na Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na kwa hakika, kwa niaba yangu mwenyewe, napenda kukutumia wewe na kupitia kwako Chama cha Democratic pongezi nyingi kwa ushindi wako wa maana sana.”




Ameongeza Rais kikwete katika salamu zake hizo: “Kuchaguliwa kwako tena kuendelea kuongoza nchi yako muhimu na wananchi wake, ni ishara ya wazi ya uaminifu na imani ambayo wananchi wa Marekani wanayo katika uongozi wako wa mfano.”

Amesisitiza Rais Kikwete: “Wakati unajiandaa kuchukua tena uongozi wa nchi hiyo katika kipindi chako kipya, napenda kukuhakikishia msimamo wangu binafsi na ule wa Serikali yangu kuwa tutaendelea kufanya kazi kwa karibu kabisa na wewe na Serikali yako ya kutukuka, ili kuendeleza uhusiano bora ulioko kati ya nchi zetu mbili ndugu.”



Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.

7 Novemba, 2012

Tuesday, November 6, 2012

Rais Kikwete akagua miradi 19 katika wiki moja






THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
              press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425


PRESIDENT’S OFFICE,
      THE STATE HOUSE,
              P.O. BOX 9120,  
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais akagua miradi 19 katika wiki moja
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amerejea Dar es Salaam mchana wa leo, Jumanne, baada ya kumaliza ziara ya siku tisa katika mikoa minne ambako amekagua, kuanzisha ama kuzindua miradi 19 ya maendeleo na kutembea kiasi cha kilomita 2,770.
Rais Kikwete amewasili Dar es Salaam akitokea Dodoma ambako amefanya ziara ya kikazi ya siku mbili baada ya kumaliza ziara katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Manyara na Singida.
          Katika Mkoa wa Kilimanjaro ambako Rais Kikwete alianzia ziara yake Oktoba 28, mwaka huu, miongoni mwa mambo mengine alikagua nyumba za wahanga wa maporomoko ya mwaka 2006 kwenye kijiji cha Goha na akafungua Kiwanda cha Kusindika Tangawizi kilichoko Mamba Miamba, Wilaya ya Same, na akafungua Shule ya Sekondari ya Kata ya Asha Rose Mingiro iliyoko mjini Mwanga.
Miradi mingine aliyoifungua Rais Kikwete katika Mkoa wa Kilimanjaro ni uzinduzi wa barabara za Rombo Mkuu-Tarakea na Kwasadallah-Masama na akafungua Ofisi ya Mkaguzi Mkuu na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (NAO) mjini Moshi.
Katika Mkoa wa Arusha, Rais Kikwete alizindua Hospitali ya Wilaya ya Arusha ya Olturumet, akazindua Mradi Mkubwa wa Uboreshaji wa Miji kwa kufungua barabara za Jiji la Arusha, akazindua Jiji la Arusha, akafungua rasmi Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela na akatembelea Kiwanda cha Nguo cha A-Z.
Kabla ya kuondoka Mkoani Arusha, Rais Kikwete alifungua Shule ya Msingi ya Sokoine na kuzindua ukarabati mkubwa wa Barabara ya Minjingu-Arusha.
Mkoani Manyara, Rais Kikwete alifungua rasmi Barabara ya Singida-Minjingu-Arusha, akazindua mradi mkubwa wa maji wa Mji wa Babati na akaweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa Barabara ya Babati-Bonga.
Mkoani Singida, Rais Kikwete alizindua mradi mkubwa wa maji wa Mwankoko kwa ajili ya Mji wa Singida, akaweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa Barabara ya Manyoni-itigi-Chaya na akafungua Barabara ya Issuna-Manyoni.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
6 Novemba, 2012


Monday, November 5, 2012

Sherehe za Mwenge za Kuadhimisha Miaka 100 ya ANC



Mhe. Balozi Radhia Msuya, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Afrika Kusini akisema machache wakati wa Sherehe za Mwenge za kuadhimisha Miaka 100 ya Chama Cha African National Congress (ANC) zilizofanyika hivi karibuni tarehe 30 Oktoba, 2012 kwenye Ofisi za Ubalozi wa Tanzania mjini Pretoria, Afrika Kusini.


 
Wanachama wa ANC wakisikiliza hotuba ya Mhe. Balozi Msuya.


Mjumbe wa Chama cha ANC, Bw. Sochayile Khanyile, naye akiongea machache wakati wa Sherehe hizo.


Wanajeshi wakiwa wamejipanga kabla ya Sherehe rasmi za kuwasha Mwenge kuanza.  Kushoto ni Bw. Robert Kahendaguza, Mtawala Mkuu kwenye Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchi Afrika Kusini.


Mhe. Balozi Radhia Msuya, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Afrika Kusini, akiwasha Mwenge, ikiwa ni ishara ya kuadhimisha Sherehe za Kitaifa za Kutimiza Miaka Mia Moja ya kuanzishwa kwa Chama Cha ANC cha Afrika Kusini.  

Sherehe hizo zilianza katika vitongoji na miji kadhaa nchini Afrika Kusini tangu mwezi Januari 2012, ambapo viongozi mbalimbali wa Kitaifa walihudhuria, wakiwemo Mhe. Rais Jacob Zuma ambaye alikuwa mgeni rasmi, Rais mstaafu Mhe. Benjamin W. Mkapa, pamoja na marais na viongozi wa nchi mbali mbali.

Wakati huo huo, matamasha mbali mbali, mijadala, maonyesho na mbio za Mwenge zimekuwa zikiendelea nchini Afrika Kusini katika muendelezo wa Maadhimisho hayo ya Miaka 100 ya Chama Tawala.   Aidha, tarehe 31 Oktoba, 2012 Mbio za Mwenge za Maadhimisho hayo zilifanyika katika Balozi zaidi ya kumi za nchi marafiki, ikiwa ni sehemu ya kutoa ushirikiano katika harakati za Ukombozi wa Afrika Kusini. Nchi hizo zinaijumuisha Tanzania, Zimbabwe, Botswana, Namibia, Zambia, Angola, Palestina, Urusi, China, Cuba na nyingine nyingi. 

Saturday, November 3, 2012

President Kikwete sends a sympathy message to H.E. President Barack Obama of the United States of America


Jakaya Kikwete - Doug Pitt Named Goodwill Ambassador Of Tanzania Hosted by President Kikwete


H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, the President of the United Republic of Tanzania, has sent a sympathy message to H.E. Barack Obama, the President of the United States of America following the devastations from hurricane Sandy.

The message reads as follows: -

 “H.E. Barak Obama,
  President of the United States of America,

  Washington, DC

  USA.

Your Excellency,

I have learnt with deep sorrow and profound dismay about the sad news of the devastating hurricane Sandy which killed more than forty people, injuring many and leaving others homeless.

In the wake of this terrible tragedy, I would like on behalf of the Government and people of the United Republic of Tanzania and indeed on my own behalf to convey our most heartfelt condolences to Your Excellency, and through you, to the bereaved families, the government and people of the United States of America.

While wishing the affected families strength and fortitude during this moment of distress please accept, Your Excellency, the assurances of my highest consideration”.


ISSUED BY: MINISTRY OF FOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL CO-OPERATION, DAR ES SALAAM.
3RD NOVEMBER, 2012




Naibu Waziri ashiriki Mkutano wa IOR na kukutana na baadhi ya Mawaziri kwa mazungumzo

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Mahadhi Juma Maalim (kushoto) akiwa katika mazungumzo na Mhe. Pierrot Jocelyn Rajaonarivelo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Madagascar. Mhe. Maalim na Mhe. Rajaonarivelo wapo nchini India kuhudhuria Mkutano wa Mawaziri kutoka Nchi Zinazopakana na Bahari ya Hindi (Indian Ocean Rim-IOR)

Mhe. Maalim akisalimiana na Mhe. Abu-Bakr Al-Qirbi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Yemen wakati wa Mkutano wa Mawaziri kutoka Nchi Zinazopakana na Bahari ya Hindi unaoendelea nchini India

Mhe. Maalim akipata picha ya kumbukumbu  na Mhe. Jean-Paul Adam, Waziri wa Mambo ya Nje wa Shelisheli mara baada ya kumaliza mazungumzo yao. Mawaziri hao wapo nchini India kuhudhuria Mkutano wa Nchi zinazopakana na Bahari ya Hindi.

Mhe. Maalim (katikati) katika picha ya pamoja na  Mhe. Jean-Paul Adam (wa pili kutoka kushoto), Waziri wa Mambo ya  Nje wa Shelisheli na Mhe John Kijazi (wa pili kutoka kulia), Balozi wa Tanzania nchini India  na wajumbe wengine wanaoshiriki Mkutano wa Mawaziri wa Nchi zinazopakana na Bahari ya Hindi.

Thursday, November 1, 2012

Naibu Waziri atembelea Ubalozi wa Tanzania nchini India

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Mahadhi Juma Maalim (Mb.), akisaini Kitabu cha Wageni  alipotembelea Ubalozi wa Tanzania nchini India. Anayeshuhudia pembeni ni Mhe. John Kijazi, Balozi wa Tanzania nchini humo. Mhe. Maalim yupo nchini India kuhudhuria Mkutano wa Mawaziri wa Nchi zinazopakana na Bahari ya Hindi (Indian Ocean Rim).

Mhe. Maalim akimsikiliza Balozi Kijazi wakati akimkaribisha  kuzungumza na Watumishi wa Ubalozini. Wengine katika picha ni baadhi ya Watumishi wa Ubalozi huo.

Mhe. Maalim (mwenye tai ya bluu) akiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Balozi Kijazi  (kulia kwake) na Watumishi wa Ubalozi wa Tanzania uliopo New Delhi nchini India mara baada ya kuwatembelea na kuzungumza nao.

Wednesday, October 31, 2012

Hon. Membe meets Consul General of India to Zanzibar


Hon. Bernard K. Membe (MP), Minister for Foreign Affairs and International Co-operation today met with Consul General of India to Zanzibar, Mr. Pawan Kumar, who had paid a courtesy visit to the Minister's Office in Dar es Salaam.


Hon. Membe in discussion with Mr. Kumar during their meeting today at this Office.


Hon. Membe meets Consul General of India to Zanzibar

By TAGIE DAISY MWAKAWAGO

The Minister for Foreign Affairs and International Co-operation, Hon. Bernard K. Membe (MP), today met with Consul General of India to Zanzibar, Mr. Pawan Kumar in his office at the Ministry in Dar es Salaam.
Mr. Kumar paid a courtesy visit to the Minister and discussed successful areas of cooperation between Zanzibar and India in particular, solar energy project. 
During their discussion, the Consul General said his Government sponsored six women from Zanzibar and provided practical training in solar power equipment installation in India for six months.
He said that since their return back to Zanzibar, the women have managed to connect electricity to 100 villages.
Mr. Kumar also highlighted new similar solar project his Government has earmarked to embark in Matemwe Village, in the Northern part of Unguja. 
“We are working on setting up training program at the doorstep in Zanzibar instead of training technician all the way to India,” said the Consul General.
On his part, Hon. Membe welcomed and congratulated the Consul General, in particular for his Government’s assistance to Zanzibar in solar energy project. 
“We have had rich traditional history with India in sectors such as  health, information and communication technology,” said Hon. Membe.
Hon. Membe said that he was happy that the solar energy project has taken its course in Zanzibar, serving hundreds of households in the rural areas. 
He further hoped that India’s cooperation through solar energy projects will continue to blossom in both parts of the Union.    

Tuesday, October 30, 2012

Membe: Hakuna mtu kusema Ziwa lote ni lake



Waziri Membe akiwa Katumbasongwe

Mhe. Bernard K. Membe (Mb), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiongea na wazee waishio Katumbasongwe, kando ya Ziwa Nyasa ndani ya Wilayani Kyela, Mkoani Mbeya.


Wakazi wa Katumbasongwe walimiminika kwa wingi kumsikiliza Mhe. Membe.


Wazee wa Katumbasongwe wakinyoosha mikono kujitambulisha umri wao wakati wa Mkutano wao na Waziri Membe uliofanyika jana Wilayani Kyela, Mkoani Mbeya.  Wazee walio weka mikono juu wana umri kati ya miaka 60 hadi 85. Waziri Membe alikuwa Mkoani humo kwa ziara ya siku mbili ambapo alitembelea maeneo na makazi ya wananchi waishio ufukweni mwa Ziwa Nyasa.



Waziri Membe akiwa Matema


Waziri Membe akiongea na wakazi wa Matema, Wilayani Kyela ambapo aliwasihi waendelee na shughuli zao za kujiletea maendeleo.  Aidha, Mhe. Membe alisema Serikali inajitahidi kadri iwezavyo kutafuta suluhisho la mgogoro wa mpaka wa Ziwa Nyasa kati ya Tanzania na Malawi. 

Wakazi wa Matema, waishio katika ufukwe wa Ziwa Nyasa, Wilayani Kyela wakimsikiliza Waziri Membe alipowatembelea jana.


Waziri Membe (hayupo pichani) pia alipata fursa ya kuongea na wazee wa Matema ikiwa ni sehemu ya mwisho wa ziara yake ya siku mbili Mkoani Mbeya.  Katika mazungumzo yake na wazee hao, Waziri Membe aliwaeleza kuwa ziara hii ni sehemu ya kukusanya ushahidi muhimu kutokana na maelezo ya historia watakazochangia hususan tangu enzi ya ukoloni kuhusu Ziwa Nyasa.



Membe: Hakuna mtu kusema Ziwa lote ni lake
 
Na TAGIE DAISY MWAKAWAGO,
Mbeya
30 Oktoba, 2012

“Hakuna mtu kusema Ziwa lote ni lake,” alisema Waziri Bernard K. Membe (Mb), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na kuongeza kuwa lazima kuwe na dhamana inayoonesha mipaka, kanuni na sheria ili kuondoa wingu la shaka yoyote hususan kwa Taifa lolote na wananchi wake. 
Aidha, Waziri Membe aliongeza kuwa Serikali ina jukumu la kumaliza mgogoro wa mpaka wa Ziwa Nyasa kati yake na Malawi, na jitihada muhimu zinafanyika ili kuumaliza kwa amani na utulivu.
Waziri Membe aliyasema hayo jana mjini Mbeya alipokuwa akizungumza na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mbeya, ambayo hiko chini ya Uenyekiti wa Mhe. Abbas Kandoro, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya.
Akiainisha jitihada hizo, Mhe. Membe alisema kuwa Kamati ya Taifa inayojumuisha timu ya wanasheria na wataalamu wa mipaka imeundwa kwa madhumuni ya kutatua mgogoro huo na timu ya Malawi.  Pia kuna timu ya Kikosi Kazi chini ya Waziri Membe, ambayo jukumu lake ni kukusanya nyaraka na kumbukumbu muhimu za mgogoro huo tangu miaka ya 1890 hadi leo.
Kwa mujibu wa maelezo ya Waziri, baada ya Kikosi Kazi kumaliza kazi yake, kitawasilisha rasmi nyaraka kwa Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete na kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ili hatua muhimu za Serikali zifanyiwe kazi.
Aidha, Mhe. Waziri alisema kuwa kuna umuhimu wa kutumia vyombo vingine ili kusaidia kutatua tatizo hili kama vile Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), Baraza la Uongozi wa Wakuu wa Afrika la SADC (Leadership Forum - SADC), Umoja wa Afrika (AU) na ikiwezekana kuipeleka kesi kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ).
Kwa upande wake, Mhe. Kandoro alisema kuwa hali Mkoani Mbeya ni tulivu na kwamba maisha yanaendelea vizuri.  Alikanusha kuhusu taarifa zisizo za kweli zilizotangazwa kwenye mitandao kwamba mabomu yamerushwa Mkoani Mbeya hususan kwenye maeneo ya mpaka wa Ziwa Nyasa. 
Aidha, Mkuu wa Mkoa aligusia ukamatwaji wa wavuvi na mitumbwi kutoka Malawi ambayo ilikuja ufukweni mwa Tanzania, na kusisitiza kuwa hatua muhimu zilichukuliwa kwa kuzingatia na kuheshimu ujirani mwema.  
Katika ziara yake, Waziri Membe pia alitembelea Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Bibi Margareth Malenga, ambapo alipata taarifa kuhusu hali ya ulinzi na usalama katika mipaka ya Ziwa Nyasa, pamoja na mahusiano kati ya Wilaya ya Kyela na Wilaya ya Karonga nchini Malawi. Wilaya ya Kyela iko mpakani mwa Wilaya ya Karonga nchini Malawi.
Akisoma taarifa ya Wilaya yake, Bibi Malenga alisema “hali ya mipaka ni tulivu na kueleza kuwa hivi karibuni, mnamo tarehe 11 Oktoba, 2012 walipata ugeni wa Mhe. Mganda Chiume, Waziri wa Mambo ya Nje wa Malawi na ujumbe wake akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Karonga nchini humo.”  
Kwa mujibu wa Bibi Malenga, lengo la ziara ya Waziri Chiume lilikuwa ni kukagua mpaka wa Ziwa Nyasa kwa upande wao lakini waliona ni vizuri waje Wilayani Kyela kuona hali ya mahusiano ilivyo baina ya wananchi wa upande wa Kyela na wale wa Karonga.   
Akiendelea na ziara yake, Waziri Membe pia alipata fursa ya kuongea na wazee alipotembelea maeneo ya Katumbasongwe na Matema yaliyopo katika ufukwe wa Ziwa Nyasa. 
“Tumekuja hapa kupata ushahidi wenu wa kihistoria tangu enzi ya ukoloni ambao utazisaidia Kamati zilizoteuliwa kutatua mgogoro huu ili ziweze kukusanya kumbukumbu na kufanya kazi ipasavyo,” alisema Waziri Membe. 
Aidha, Waziri Membe aliwahakikishia amani na utulivu wananchi wa Kyela, na kusema kuwa “Serikali inajitahidi kadri iwezavyo kutatua mgogoro huu kwa njia ya kidiplomasia na hata kama ikiwezekana kwenda ICJ.”
Kabla ya kumaliza ziara yake ya siku mbili jana Mkoani Mbeya, Mhe. Membe alitembelea Kasumulu ambapo mpaka wa Mto Songwe hupo, ikiwa ni pamoja na Katumbasongwe na Matema kwenye ufukwe wa Ziwa Nyasa ambapo alizungumza kwa kina na wakazi waishio ufukweni mwa Ziwa hilo.

Mwisho.




Membe: We are committed to settle the Lake Nyasa dispute


 Hon. Membe in Katumbasongwe

Hon. Bernard K. Membe (MP), Minister for Foreign Affairs and International Co-operation is talking to residents of Katumbasongwe, offshore of the Lake Nyasa, in Kyela District - Mbeya Region.  Hon. Membe assured them peace, security and wanted them to continue with their daily activites.


Residents of Katumbasongwe are doing their daily activities near offshore of the Lake Nyasa.

Residents of Katumbasongwe are busy doing their daily activities such as washing dishes and bathing kids.  Witnessing the activities is Journalist and Owner of Jamhuri Newspaper, Mr. Jakton Manyerere (2nd left).


Hon. Membe witnessing some of daily activities of Katumbasongwe residents.  Minister Membe was in Mbeya Region for a two-day tour around the Kyela District and offshore areas near the Lake Nyasa which ended yesterday.



 .....while in Matema


Hon. Membe assured residents of Matema peace and security, asking them to continue with their daily activites. Matema is located in the offshore of Lake Nyasa in Kyela District. During his meeting, Hon. Membe said the Government will to continue its efforts in resolving diplomatically the dispute of Lake Nyasa between Tanzania and Malawi.  


The Matema residents listening to Hon. Membe (not in the photos) explanation of the dispute of Lake Nyasa between Tanzania and Malawi.  Both countries have been in dispute over the Lake Nyasa, whereas Malawi claims ownership of the whole Lake of the area under dispute and Tanzania claims the 50 percent share ownership of the same.
 

   
Daily activities in Matema near the offshore of the Lake Nyasa in Mbeya Region.




  
Fishermen arriving in Matema with their boat, whereas children are playing and bathing on the Lake Nyasa.



Photos by Tagie Daisy Mwakawago