Friday, November 21, 2014

Waziri Membe azindua Chama cha Urafiki wa Tanzania na China

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akitoa hotuba ya uzinduzi wa  Chama cha Urafiki wa Tanzania na China. Hafla ya uzinduzi huo ilifanyika Jijini Dar es Salaam na kuhuduhuriwa na Mwenyekiti wa Chama hicho ambaye ni Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Dkt. Salim Ahmed Salim, Balozi wa China nchini, Mhe. Lu Yongqing na Viongozi wengine.
Mhe. Membe akihutubia.
Balozi wa China nchini, Mhe. Lu Yongqing akihutubia wakati wa hafla hiyo. 
Mwenyekiti wa Chama hicho Mhe. Salim nae akizungumza wakati wa hafla hiyo
Mhe. Membe kwa kushirikiana na Balozi Lu Yongqing wakizindua Chama hicho kwa mara nyingine.
Waziri Membe, Balozi Lu na Dkt. Salim pamoja na wageni waalikwa wakati wa hafla hiyo.
Waziri Membe pamoja na Wageni waalikwa wakiinua glasi juu kutakiana heri

Waziri Membe akijadiliana jambo na Dkt. Salim
Hafla ikiendelea

WAZIRI MEMBE AWAASA WAHITIMU WA KIU KUTII SHERIA ZA NCHI

 Brass Band ya Jeshi la Magereza ikiwaongoza Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala (KIU), Kampasi ya Dar es Salaam , Rais Mstaafu, Mhe. Ali Hassan Mwinyi, mgeni rasmi, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe, Maafisa, Wahadhiri,Wahitimu pamoja na Wageni Waalikwa kuingia katika Viwanja vya Chuo Kikuu  hicho katika sherehe za Mahafali ya Kumi na Moja ya chuo hicho yaliyofanyika tarehe 21.11.2014.
  Mhe. Membe (mwenye joho la bluu) akiongozana na baadhi ya Wahadhiri kuingia katika viwanja yalikofanyika mahafali ya kumi na moja ya chuo kikuu cha Kimataifa cha Kampala Kampasi Dar es Salaam huko Gongo la Mboto.
 Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala ambaye pia ni Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Mhe. Ally Hassan Mwinyi  (mwenye kofia ya njano) akiwa pamoja na mgeni rasmi  Mhe. Membe (wa pili kutoka kushoto) wakiwa wamesimama kwa heshima ya Wimbo wa Taifa kama ishara ya kuanza kwa mahafali hayo ya kumi na moja.
 Shekhe Dr.Badruh H.Sseguja akifungua kwa sala Mahafali ya Kumi na Moja ya Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam tarehe 21.11.2014
  Mchungaji Ogah Ogbole akifungua kwa sala mahafali ya kumi na moja ya Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam tarehe 21.11.2014
 Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala Profesa Mohamed Ndaula akitoa hotuba ya ufunguzi wa  mahafali hayo ya kumi na moja ya chuo hicho Jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya wahitimu wa fani mbalimbali wa chuo kikuu cha kimataifa cha Kampala Kampasi ya Dar es Salaam wakiwa wamekaa kwa utulivu tayari kabisa kwa ajili ya sherehe za mahafali ya kumi na moja ya chuo hicho ambapo jumla ya wanafunzi 902 walihitimu masomo yao.
 Baadhi ya wakuu wa idara mbalimbali za Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala wakiingia katika viwanja vya chuo hicho Kampasi ya Dar es Salaam tayari kwa mahafali ya kumi na moja ya chuo hicho.
 Mkuu wa chuo kikuu cha kimataifa cha Kampala Mheshimiwa Ally Hassan Mwinyi akiwahutubia wahitimu wa mahafali hayo ya kumi na moja.
   Mgeni rasmi, Mhe. Bernard Membe akiwahutubia wahitimu wa mahafali hayo ya kumi na moja ambapo aliwaasa kwenda kufanya kazi kwa bidii na kutii sheria za nchi.
 Baadhi ya wahitimu wa chuo kikuu cha kimataifa cha Kampala wakinyanyua kofia zao juu mara baada ya kutunukiwa shahada zao katika mahafali yao ya kumi na moja ya chuo hicho.
 Baadhi ya wageni waalikwa waliohudhuria mahafali hayo wakifuatilia hatua kwa hatua kile kinachoendelea katika sherehe hizo.
 Mkuu wa chuo kikuu cha kimataifa cha Kampala akitunuku shahada kwa wahitimu wa mahafali hayo.
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala ambaye pia ni Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa Awamu ya Pili, Mhe. Ally Hassan Mwinyi ( mwenye joho la njano) akiwa pamoja na mgeni rasmi, Mhe. Membe pamoja na meza kuu wakiwa wamesimama kwa heshima ya wimbo wa taifa kama ishara ya kufunga mahafali hayo ya kumi na moja.


 Mgeni rasmi akizungumza na waandishi wa habari baada ya mahafali hayo.

PICHA NA Reuben Mchome
======================================

Membe Mgeni Rasmi Mahafali KIU

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Membe, amesema elimu imekomboa wanawake nchini Tanzania kwa kuwapa uwezo wa kushiriki sawa sawa na wanaume kwenye fursa za kiuchumi, kisiasa na kijamii.

Mhe. Membe, ambaye alikuwa akihutubia kwenye mahafali ya 11 ya Chuo Kikuu cha Kampala (KIU), Jijini Dar es Salaam leo, aliwataka wanawake kutumia kikamilifu fursa za elimu ya juu ili wajitegemee kiuchumi na kuondokana kabisa na unyanyasaji wa kijinsia.

Alielezea kuridhishwa na uwezo ulioonyeshwa na wahitimu wa kike katika chuo hicho. Kati ya wahitimu 902 waliotunukiwa Shahada na Stashahada na Mkuu wa Chuo Kikuu hicho, Rais Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi, 423 ni wanawake.

Mhe. Membe aliwataka wahitimu hao watumie elimu yao vizuri katika kuiendeleza jamii na taifa, kufanya kazi kwa bidii na kutii sheria za nchi.

Tuesday, November 18, 2014

PRESS RELEASE

Sultan of Oman, His Majesty Qaboos bin Said Al Said

PRESS RELEASE

His Excellency Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to His Majesty Qaboos bin Said Al Said, Sultan of the Sultanate of Oman on the occasion of the 44th Anniversary of the Sultanate of Oman National Day.

The message reads as follows;
“His Majesty, Qaboos bin Said,
Sultan of the Sultanate of Oman
MUSCAT,
Your Majesty,

On behalf of the Government and the people of the United Republic of Tanzania, and indeed on my own behalf, I would like to sincerely convey my warm congratulations to you, Your Majesty and through you, to the Government and the people of Oman on celebrating the 44th Anniversary of the National Day.

The Sultanate of Oman and the United Republic of Tanzania have enjoyed cordial and brotherly bilateral relations over the years. As you commemorate this joyous occasion of your National Day, I wish to take this opportunity to reiterate my Government’s desire and commitment to further enhance the traditional bond of friendship and cooperation existing between our two countries for our mutual benefits.

Please accept, Your Majesty, my most sincere congratulations and best wishes for the continued good health and happiness, and for the friendly people of the Sultanate of Oman, further progress and prosperity”.

ISSUED BY: THE MINISTRY OF FOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL COOPERATION, DAR ES SALAAM.
18th NOVEMBER, 2014



Monday, November 17, 2014

Waziri Membe afungua Mkutano wa Kimataifa kuhusu Sayansi ya Jamii

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akitoa hotuba ya ufunguzi wa   Mkutano wa Kimataifa wa siku mbili kuhusu Sauti ya Kwanza ya Sayansi ya Jamii. Mkutano  huo ambao unafanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Mlimani  chini ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam unawashirikisha Wajumbe kutoka  Tanzania, Kenya, Uganda, Ghana, Nigeria na Canada. Katika hotuba yake Mhe. Membe alisisitiza umuhimu wa Wasomi na Wanazuoni kujikita katika Tafiti za Kisayansi ili kuja na majibu yatakayoisaidia nchi kuondokana na umaskini, utunzaji wa mazingira na masuala mengine ya manufaa kwa nchi.
Mhe. Membe akikaribishwa na Prof. Florence Luoga ambaye ni Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo cha Dar es Salaam mara baada ya kuwasili kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Mlimani kwa ajili ya ufunguzi rasmi wa Mkutano wa Kimataifa wa siku mbili kuhusu Sauti ya Kwanza ya Sayansi ya Jamii  ulioandaliwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. 
Mhe. Membe akikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa mkutano huo
JUU NA CHINI: Ni sehemu ya Wajumbe wakifuatilia mkutano huo kuhusu masuala ya Sayansi ya Jamii.
Mhe. Membe akiendelea na hotuba yake ya ufunguzi huku wajumbe wakimsikiliza.
Sehemu ya wajumbe wakifurahia jambo wakati Mhe. Membe (hayupo pichani) akitoa hatuba ya ufunguzi.
Mhe. Membe akisindikizwa kwenda kupiga picha ya pamoja na Maprofesa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam waliokuwepo kwenye mkutano huo
Mhe. Membe (wa tatu kulia waliokaa) katika picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe wa mkutano kuhusu masuala
Waziri Membe akifurahia jambo na mmoja wa Wajumbe wanaoshiriki mkutano huo.
Mhe. Membe akihojiwa na Wanahabari kuhusu mkutano huo.

Picha na Reuben Mchome

Saturday, November 15, 2014

Waziri wa Uchukuzi akutana na Konseli Mkuu wa Tanzania, Dubai

Waziri wa Uchukuzi Mhe. Harrisson Mwakyembe (Mb.), amekutana na kufanya mazungumzo ofisini kwa Bw. Omar Mjenga, Konseli Mkuu wa Tanzania, Dubai.

 Konseli Mkuu amemueleza Mhe. Mwakyembe kuhusu mazungumzo yake pamoja na Mhe. Gaith  Alghaith, Mtendaji Ma wa Shirika la Ndege la FlyDubai, kuhusu mpango wa shirika hilo kuingia makubaliano ya ushirikiano pamoja na shirika la Ndege la Tanzania(Air Tanzania) ambako Flydubai watatoa ndege tano zitakazochukua njia za ndani (domestic routes) na zile za kikanda (regional routes).

Ushirikiano huu utasaidia kufufua njia zote za ATC na kuiwezesha ATC kuanza kupata mapato.
Njia za kikanda ni pamoja na Kinshasa, Lubumbashi, Goma, Kigali, Bunjumbura, Entebe, Nairobi, Sychelles, Moroni, Madagascar, Mauritius, Maputo, Lilongwe, Lusaka, Joharnessburg, na Harare.

Friday, November 14, 2014

Waziri Membe akutana na Mabalozi wa Misri na Sudan nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akisalimiana na Balozi wa Misri hapa nchini, Mhe. Hossam Moharram alipofika Wizarani kwa mazungumzo kuhusu kuimarisha ushirikiano baina ya nchi hizi mbili.
Mhe. Membe akifafanua jambo wakati wa mazungumzo yake na Balozi Moharram. Wengine pichani ni Maafisa kutoka Ubalozi wa Misri.


......Waziri Membe na Balozi wa Sudan

Waziri Membe akisalimiana na Balozi wa Sudan hapa nchini, Mhe. Dkt. Yassir Mohamed Ali alipokutana nae kwa mazungumzo Wizarani.

Picha na Reuben Mchome

Monday, November 10, 2014

Naibu Katibu Mkuu akutana kwa mazungumzo na Mjumbe Maalum wa Marekani Eneo la Maziwa Makuu


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Rajabu Gamaha akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiriano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb)  na Mjumbe Maalum wa Marekani kwenye Ukanda wa Maziwa Makuu, Bw. Russel D. Feingold alipofika Wizarani kwa ajili ya mazungumzo. Katika mazungumzo yao waligusia mchango wa Tanzania katika suala la amani Mashariki mwa  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. 
Mkurugenzi wa Idara  ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Joseph Sokoine akiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, Bw. Innocent Shiyo  wakifuatilia mazungumzo kati ya Naibu Katibu Mkuu na Bw. Russel (hawapo pichani).

Sehemu ya ujumbe uliofutatana na Bw. Russel wakifuatailia mazungumzo.
Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakati wa mazungumzo kati ya Balozi Gamaha na Bw. Russel (hawapo pichani)

Picha na Reuben Mchome

Friday, November 7, 2014

Mhe. Rais awaapisha Balozi Zoka na Balozi Shelukindo


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.  Jakaya Mrisho Kikwete akimuapisha na kumkabidhi vitendea kazi Mhe. Jack Mugendi Zoka kuwa Balozi mpya wa Tanzania nchini Canada, Ikulu Jijini Dar es Salaam leo Novemba 6, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi vitendea kazi Mhe Jack Mugendi Zoka
 Mhe. Rais Kikwete akimuapisha Bw. Samwel William Shelukindo kuwa Balozi na Mshauri wa Rais masuala ya Diplomasia  Ikulu Jijini Dar es salaam. Kabla ya uteuzi huu, Balozi Shelukindo alikuwa Afisa Mambo ya Nje Mwandamizi katika Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia.
Mhe. Rais Kikwete akimkabidhi vitendea kazi Balozi Samwel William Shelukindo.
Picha ya pamoja ya Mhe. Rais na Balozi Shelukindo, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sfue pamoja na Wakurugenzi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Balozi Joseph Sokoine. Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Balozi Mbelwa Kairuki na anayefuata ni Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy.
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue akizungumza jambo na Balozi  Shelukindo baada ya kuapishwa.
Balozi Shelukindo (wa pili kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi wenzake kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.


Picha na Reginald Philip