Sunday, September 27, 2015

Rais Kikwete atangaza agenda ya Wanawake kwenye Mkutano wa Umoja wa Mataifa



Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitoa hotuba yake huku wajumbe wengine wakisikiliza wakiwemo Mhe. Sofia Simba (Mb.), Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto(wa pili kulia). 

Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Mama Getrude Mongela aliyeongoza mkutano mkubwa wa wanawake miaka 20 iliyopita Jijini Beijing China. 




Tanzania yatangaza hatua tano za kuendeleza haki za wanawake na usawa wa kijinsia
·      Yaahidi kufanya mabadiliko makubwa ya kisera na kisheria
·      Miongoni mwa Sheria zitakazohusika ni Sheria ya Ndoa na Sheria ya Urithi
·      Ni katika utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu  - SDG’s
Tanzania imeahidi kuchukua hatua tano muhimu za kutetetea na kuendelea haki za wanawake kati ya sasa na mwaka 2030, ikiwa ni pamoja na kufanya mabadiliko makubwa ya kufuta sheria zinazokandamiza wanawake na kutunga sheria za kuleta usawa wa kijinsia, yote katika utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG) mapya kwa manufaa ya wanawake wa Tanzania.
Miongoni mwa hatua hizo itakuwa ni pamoja na kufuta ama kufanya mabadiliko ambayo yanaendeleza vitendo vya kiutamaduni ambavyo kwavyo vinaendeleza ubaguzi wa wanawake kama vile Sheria ya Ndoa, Sheria ya Urithi na kutunga Sheria ya Kukomesha Ukatili dhidi ya wanawake.
Msimamo huo wa Tanzania umeelezwa Jumapili, Septemba 27, 2015 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete alipozungumza katika Mkutano wa Usawa wa Jinsia na Uwezeshaji wa Akinamama: Dhamira ya Kuchukua Hatua uliohudhuriwa na wakuu wa nchi mbali mbali duniani kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa (UN) mjini New York, Marekani.
Rais Kikwete ameuambia mkutano huo ulioitishwa  kwa pamoja na Jamhuri ya Watu wa China, Denmark, Mexico na Kenya kuwa hatua ya pili ambayo Tanzania inakusudia kuchukua ni kuridhia makubaliano yote ya kimataifa kuhusu haki za akinamama hasa Makubaliano ya Kimataifa Juu ya Kukomesha Aina Zote za Ubaguzi Dhidi ya Wanawake – Convention on the Elimination of All Forms of Discrimination Against Women (CEDAW).
Hatua nyingine ambazo Rais Kikwete amesema kuwa Tanzania itachukua katika miaka 15 ijayo ili kuhakikisha usawa wa kijinsia nchini ni zifuatazo:
·      Kuendeleza na kuunga mkono upatikanaji wa raslimali fedha zinazolenga kuongeza usawa wa kijinsia kwa mujibu wa Ajenda ya Kugharimia Maendeleo ya Addis Ababa, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha zinatolewa pesa za kutekeleza mipango ya kitaifa na ya Serikali za mitaa za kukomesha ukatili dhidi ya wanawake.
·      Kuhakikisha utekelezaji wa uwakilishi wa uongozi wa asilimia 50-50 kati ya wanawake na wanaume katika nafasi zote za maamuzi kwenye ngazi zote.
·      Kupatikana na kutumiwa kwa data na habari za ukweli katika utunzi wa sera na utoaji maamuzi ya kukomesha ubaguzi wa kijinsia.
·      Kutunga na utekelezaji mfumo wa uwajibikaji na ufuatiliaji wa haki za kijinsia na haki za akinamama zilizokubaliwa kitaifa na kwenye ngazi ya Serikali za mitaa.
Rais Kikwete pia amewaambia wajumbe wa mkutano huo kuhusu hatua za kisera na kisheria ambazo zimechukuliwa na Tanzania katika miaka ya karibuni kujenga usawa wa kijinsia, ikiwa ni pamoja na Sheria ya Ardhi ya mwaka 1999 na marekebisho yake ya mwaka 2004 ambayo yanawapa akinamama nafasi na haki ya kupata, kushikilia, kutumia na kumiliki ardhi.
Hatua nyingine ni kuwapa wanawake nafasi za maamuzi na uongozi katika nyanja za kisiasa na maisha ya umma. Katika kutekeleza hilo, idadi ya wabunge wanawake imeongezeka kutoka asilimia 21.5 ya wabunge wote mwaka 2005 hadi kufikia asilimia 34.5 mwaka huu, mawaziri wanawake wameongezeka kutoka sita mwaka 2005 hadi kufikia 26 mwaka huu na idadi ya majaji wanawake imeongezeka kutoka wanane mwaka 2005 hadi kufikia 41 mwaka huu.
Rais Kikwete amesema kuwa hatua nyingine zilizochukuliwa na Serikali ni kupunguza vifo vya wanawake wakati uzazi, kutunga Sheria dhidi ya ukatili wa kijinsia na ukatili dhidi ya wanawake na watoto; kuanzishwa kwa uandaaji wa Bajeti inayotilia maanani mahitaji ya wanawake na kuongeza uwezekaji wa kiuchumi wa akinamama kupitia kuanzishwa kwa Benki ya Wanawake Tanzania (TWB) yenye kulenga kutoa mikopo ya masharti nafuu kwa akinamama wafanyao biashara ndogo ndogo na za kati.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

28 Septemba, 2015

Foreign Permanent Secretary Discusses Climate Change with The Elders


Ambassador Liberata Mulamula and the group of Elders and other envitees in a group photos after discussions on Climate Change held at the W Hotel in New York City.
Sitted with Ambassador Mulamula is Gro Harlem Brundtland, First woman Prime Minister of Norway also chair of the breakfast  meeting. 

African countries are urged to take the leading role and owning the process of mitigating climate change since it affects them the most. The message was given by Ambassador Liberata Mulamula, Foreign Affairs Permanent Secretary while discussing preparedness level of African countries in dealing with global issue of climate change at the breakfast with The Elders in New York. 

The meeting which was held at the margins of the 70th Session of the United Nations General Assembly was aimed at triggering conversation from African countries and Island States on the action to be taken into consideration at the Conference on Climate Change to be held at Paris end of 2015. 

"Tanzania expects to see agreements that have taken into consideration elements of mitigation, adoptation as well as financing" Said Mulamula. 

She added that African countries who are mostly afftected by the climate change should own the process, preparing tirelessly as well as giving education to its population on the importance of protecting the environment.

The Elders is an independent group of global leaders who work together for peace and human rights. They were brought together in 2007 by Nelson Mandela. 

Also in attendance at the Elders Breakfast was the H.E. Hailemariam Desalegn, Prime Minister of Ethiopia (third from left).
Ambassador Liberata Mulamula with one of The Elders - Graca Machel of Mozambique.

Ambassador Mulamula, Graca Machel, Mindi Kasiga and Noel Kaganda after The Elders Breakfast on Climate Change.

Saturday, September 26, 2015

JK katika Mkutano wa 70 wa Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani, Leo

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano wa 70 wa Umoja wa Maiataifa akiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na ushurikiano wa Kimataifa Mhe Bernard Membe, Waziri wa Waziri wa Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto Mhe Sophia Simba, Waziri wa Fedha Zanzibar Mhe Yussuf Mzee na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje, Balozi  Liberata Mulamula 
Rais Kikwete akiwa na Waziri Mkuu wa Denmark Mhe. Lars Loekke Rasmussen 

 Rais Kikwete akiwa na Rais mstaafu wa Finland Mama Tarja Halonen

Rais Kikwete na ujumbe wa Tanzania Waziri wa Mambo ya Nje na ushurikiano wa Kimataifa Mhe Bernard Membe, Waziri wa Waziri wa Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto Mhe Sophia Simba, Waziri wa Fedha Zanzibar Mhe Yussuf Mzee,  Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje, Balozi  Liberata Mulamula na Balozi Tuvako Manongi, Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa.
Rais Kikwete na Waziri Mkuu wa Bahamas Mhe Perry Christie. Hapo Mhe Rais alimfahamisha Waziri Mkuu huyo kwamba yey anamaliza muda wake na Waziri Mkuu akaeleza matumaini yake kwamba atakayemrithi ataendelea kuimarisha uhusisno wa Tanzania na Bahamas na nchi za Caribbean.  
Rais Kikwete akiwa na Rais Filipe Jacinto Nyusi wa Mzumbiji na mawaziri wao wa nchi za nje
Rais Kikwete na Ujumbe wake wakimlaki Baba Mtakatifu Francis alipowasili kuhutubia Umoja wa Mataifa kwa mara ya kwanza. Picha kwa hisani ya Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa.
Baba Mtakatifu Francis akihutubia Umoja wa Mataifa kwa mara ya kwanza.

Friday, September 25, 2015

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Taarifa kuhusu Mahujaji kutoka Tanzania waliofariki na kujeruhiwa huko Saudi Arabia

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa imepokea kwa mshtuko na masikitiko makubwa taarifa za kufariki kwa Mahujaji zaidi ya 700 na wengine zaidi ya 800 kujeruhiwa wakati wakishiriki ibada ya Hijja iliyofanyika Makkah, Saudi Arabia tarehe 24 Septemba, 2015.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Ubalozi wa Tanzania, Saudi Arabia
Mahujaji hao walifariki na kujeruhiwa kutokana na msongamano mkubwa wa watu uliotokea kwenye eneo la Mina.

Aidha, taarifa hizo zinaeleza kuwa hadi sasa Mahujaji wapatao watano (5) kutoka Tanzania wamefariki dunia na wengine kujeruhiwa. Majina ya Watanzania waliofariki na kutambuliwa ni Bi. Mwanaisha Hassan Juma, Mkungwe Suleiman Hemedi na Sefu Saidi Kitimla. Mtu mwingine aliyefariki ni Raia wa Kenya anayeishi nchini ambaye ametambulika kwa jina la Bi. Fatuma Mohammed Jama.

Ubalozi unaendelea na jitihada za kupata jina la Mtanzania mwingine aliyefariki kwenye tukio hilo. Aidha, Serikali ya Saudia imetangaza kuwa itatoa taarifa kamili ikiwemo idadi ya watu waliofariki na majeruhi na nchi wanazotoka mara itakapokamilika.

Pia Ubalozi wetu kwa kushirikiana na Taasisi zinazoshughulikia masuala ya Hijja za Tanzania ikiwemo BAKWATA pamoja na Mamlaka za Serikali ya Saudi Arabia unaendelea kufuatilia kwa karibu ili kujua endapo kuna vifo na majeruhi wengine kutoka Tanzania.

Hivyo basi, Wananchi wanaombwa kuwa watulivu katika kipindi hiki kigumu wakati Serikali ikiendelea kufuatilia.

-Mwisho-
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali kwa Umma,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,
Dar es Salaam
25 Septemba, 2015

PRESS RELEASE

H.R.H Salman bin Abdulaziz Al Saud, King of  Saudi Arabia

PRESS RELEASE

H.E. Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a condolence message to H.R.H. Salman bin Abdulaziz Al Saud, King of the Kingdom of Saudi Arabia following a tragic death of more than 700 pilgrims which occurred in Makkah  on 24th September, 2015.

 The massage reads as follows:

“His Royal Highness Salman bin Abdulaziz Al Saud,
King of Saudi Arabia and Custodian of the Two Holy Mosques,
RIYADH,
SAUDI ARABIA.

Your Royal Highness,

I am deeply saddened by the news about the death of more than 700 pilgrims and injured of others more than 800 on Thursday 24th September, 2015 in a stampede outside the holy city of Makkah when they were completing their rituals.

On behalf of the Government and the people of the United Republic of Tanzania, I wish to convey to you and through you to the people of the Royal Kingdom of Saudi Arabia and all the bereaved pilgrims’ families, our heartfelt condolences and sympathies.

My family and the people of the United Republic of Tanzania are praying that the departed soul be rested in paradise, and for patience and solace to all pilgrims’ families around the world.

May Almighty Allah grant quick recovery to all injured people.

Please accept, Your Royal Highness and dear colleague, the assurance of my highest consideration”.


Issued by: The Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation, Dar es Salaam



25th September, 2015.

Thursday, September 24, 2015

Tanzania yapongezwa kwa uongozi bora wa Kikundi Kazi cha Mawaziri Jumuiya ya Madola

Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola ukiendelea pembezoni mwa Mkutano wa 70 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Jijini New York, Marekani.

Sekretarieti ya Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola wamesifu kazi iliyofanywa na Tanzania kama Mwenyekiti wa Kikundi Kazi cha Mawaziri wa Mambo ya Nje wa jumuiya hiyo ya kusimamia na kuimarisha misingi imara ya jumuiya katika kipindi cha miaka miwili iliyopita. 

Hayo yamesemwa na Dkt. Josephine Ojiambo Makamu Katibu Mkuu wa Sekretarieti hiyo, kwenye taarifa fupi ya utekelezaji wa kazi za Jumuiya kwenye Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola uliofanyika Septemba 24, pembezoni mwa Mkutano wa 70 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa uongozi wa Mhe. Bernard Membe (Mb.), ambaye ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Tanzania umeibua mbinu za kisasa za kutatua matatizo ya nchi wanachama zilizokuwa na changamoto ya kuheshimu misingi na taratibu za Jumuiya ya Madola. 

Waziri Membe ambaye anamaliza muda wake wa uongozi kwenye kikundi kazi hicho mwaka huu, amesema mafanikio hayo yametokana na ushirikiano mzuri aliokuwa anaupata kutoka kwa Sekretarieti inayoongozwa na Kamalesh Sharma, ambao ndio waratibu wa shuguli za Kikundi Kazi cha Mawaziri. Vilevile ushirikiano aliopewa na Makamu Mwenyekiti wa Kikundi hicho Mhe. Murray McCully, Waziri wa Mambo ya Nje wa New Zealand pamoja na wajumbe wengine wa Kikundi hicho maalum kimewezesha kazi za kuratibu kazi za Jumuiya hiyo kuwa na mafanikio makubwa. 

Masuala mengine yaliyojadiliwa kwenye mkutano wa Mawaziri ni utekelezaji wa maamuzi ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya hiyo kuhusu uimarishwaji wa mifumo ya tehama na  nyenzo mbalimbali za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi kwenye nchi wanachama uliofanyika mwaka 2013  Jijini Colombo, nchini Sri Lanka. 

Kwenye mkutano huo pia Mhe. George William Vella, Waziri wa Mambo ya Nje wa Malta alitoa taarifa fupi kuhusu maandalizi ya Mkutano wa mwaka huu wa wakuu wa nchi na serikali wa Jumuiya hiyo utakaofanyika Novemba 2015, nchini Malta. 

(Pichani juu na chini) Mhe. Bernard Membe (Mb.), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akifuatilia Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola

Wednesday, September 23, 2015

Mkurugenzi wa Mashariki ya Kati azungumza na Balozi wa UAE nchini

Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Balozi Abdallah Kilima (kulia) akimsikiliza Balozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), Mhe. Abdulla Ibrahim Ghanim Alsuwaidi (kushoto) alipokuja kujitambulisha na kumpongeza kwa kuteuliwa kuwa Mkurugenzi  na Balozi mpya katika Idara hiyo ya Mashariki ya Kati. Katika mazungumzo yao waligusia masuala ya kuboresha mahusiano kati ya Tanzania na Nchi za Umoja wa Falme za Kiarabu.  
Afisa Mambo ya Nje, Bw. Hangi Mgaka akisikiliza mazungumzo kati ya Balozi Kilima na Balozi Abdulla Ibrahim Ghanim Alsuwaidi (hawapo pichani).
Balozi Kilima (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Alsuwaidi

Tuesday, September 22, 2015

Katibu Mkuu akutana kwa mazungumzo na Naibu Mwangalizi Mkuu wa Uchaguzi kutoka EU

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula akimsikiliza  Naibu Mwangalizi Mkuu wa Uchaguzi kutoka Jumuiya ya Ulaya (EU), Bi.Tania Marques alipokuja Wizarani kwa ajili ya mazungumzo kuhusu mipango ya Timu ya Waangalizi kutoka Jumuiya ya Ulaya wakati wa uchaguzi mkuu.
Maafisa Mambo ya Nje wakifuatilia mazungumzo hayo kwa makini. Kushoto ni Bw.Gerald Ngwafu na Bi. Mona Mahecha
Balozi Mulamula (kulia) akizungumza na Bi.Marques
Balozi wa Umoja nchini, Mhe. Filiberto Sebregondi (wa kwanza kushoto) naye akichangia jambo wakati wa mazungumzo hayo.
Mazungumzo yakiendelea