Wednesday, October 25, 2017

Wizara yamtunuku nishani Balozi Kapya

Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt.Aziz P Mlima (kushoto) akimkabidhi nishani Mhe.Balozi David Kapya kutokana na mchango wake wa kushiriki katika utatuzi wa migogoro  katika sehemu mbalimbali Barani Afrika. Mhe. Balozi Kapya amekabidhiwa nishani hiyo katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es  Salaam.

Katibu Mkuu Balozi Dkt.Aziz P Mlima akimpongeza Balozi David Kapya mara baada yakumtunuku nishani kufuatia mchango wake mkubwa wa kushiriki katika utatuzi wa migogoro

Rais Magufuli apokea Hati za Utambulisho za Mabalozi wapya kutoka nchini Oman, Uholanzi na China

Rais wa Jamhuri wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Oman nchini, Mhe. Ali bin Abdallah bin Salim Al-Mahrooqi mwenye makazi yake Jijini Dar es Salaam. Makabidhiano hayo yamefanyika leo Ikulu Jijini Dar es Salaam. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Mhe. Al-Mahrooqi.
Wakiwa katika mazungumzo ambapo maongezi yao yalijikita katika kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia sambamba na ushirikiano katika masuala ya biashara na uwekezaji ambao ndio msingi mkuu wa kuinua uchumi wa mataifa hayo.
Picha ya pamoja.  
Mkuu wa Itifaki katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Grace Martin akimtambulisha Mhe. Al-Mahrooqi kwa Mhe. Rais Magufuli kabla ya kukabidhi Hati za Utambulisho.
Mhe. Al-Mahrooqi akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Ofisi za Ikulu Jijini Dar es Salaam.


Balozi Al-Mahroooqi akipigiwa Wimbo wa Taifa wa Tanzania na Oman mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam.                     
=========================================================

Wakati huohuo Mhe. Rais Magufuli alipokea Hati za Utambulisho za Balozi wa Uholanzi.


Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Uholanzi nchini, Mhe. Jeroen Verheul mwenye makazi yake Jijini Dar es Salaam. Makabidhiano hayo yamefanyika leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Itifaki, Balozi Grace Martin akimtambulisha Mhe. Verheul kwa Mhe. Rais Magufuli.    
Picha ya pamoja Viongozi na Maafisa wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Ubalozi wa Uholanzi nchini.     
Mhe. Waziri Mahiga akimtambulisha Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bi. Mary Matari kwa Mhe. Verheul.
Mhe. Rais Magufuli akizungumza na Balozi wa Uholanzi nchini mara baada ya kupokea Hati za Utambulisho. 
 
Mhe. Verheul akipigia wimbo wa Taifa wa Tanzania na Uholanzi na bendi ya polisi na baadae aliagana na kiongozi wa bendi hiyo.
====================================================================
Katika nafasi nyingine Mhe. Rais Magufuli alipokea Hati za Utambulisho za Balozi wa China nchini.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati za Utambulisho za Balozi wa China nchini, Mhe. Wang Ke mwenye makazi yake Jijini Dar es Salaam. Makabidhiano hayo yamefanyika leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Balozi Grace Martini akimtambulisha Mhe. Wang kwa Mhe. Rais Magufuli kabla ya kukabidhi Hati hizo.
Picha ya pamoja.
Mhe. Wang akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Mhe. Wangi akiagana na kiongozi wa Bendi ya Polisi mara baada ya kukamilisha hafla ya makabidhiano.

Maadhimisho ya Miaka 72 ya Umoja wa Mataifa yafana

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokelewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga mara baada ya kuwasili kwenye Viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kushiriki maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa. Maadhimisho hayo ambayo hufanyika tarehe 24 Oktoba kila mwaka yalibeba kaulimbiu isemayo "Maendeleo ya Viwanda na Utunzaji wa Mazingira kwa Maendeleo Endelevu".
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz Mlima wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Celestine Mushy wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa, Bw. Alvaro Rodriguez wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea heshima ya wimbo wa Taifa wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa.
Wageni waalikwa wakiwa wamesimama wakati wimbo wa Taifa ukipigwa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride la Heshima lililoandaliwa kwa ajili maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa, Bw. Alvaro Rodriguez wakishuhudia upandishwaji wa Bendera ya Umoja wa Mataifa (Flag Raising) ikiwa ni ishara ya kilele cha maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akitoa hotuba wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza machache wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa, Bw. Alvaro Rodriguez naye akitoa salamu za Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa.
Kikundi cha Burudani cha Wanafunzi kutoka Zanzibar kikitumbuiza wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa
Wanafunzi kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Weruweru wakiimba wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa.
Sehemu ya wageni waalikwa wakifuatilia matukio wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa, Bw. Alvaro Rodriguez akimkabidhi tuzo maalum  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kutambua ushirikiano na mchango wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa.
Mhe. Waziri Mahiga naye akipokea tuzo kutoka kwa Bw. Rodriguez. Kulia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Harrison Mwakyembe.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa yaliyopo nchini
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini.
Maafisa Mambo ya Nje ambao wameshiriki  Maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa wakiwa katika picha ya kumbukumbu
Sehemu nyingine ya Maafisa kutoka Wizara ya  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki walioshiriki  maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa.
Watumishi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakipata picha ya kumbukumbu wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa






Tuesday, October 24, 2017

Waziri Mahiga apokea Nakala za Hati Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa China nchini.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (kulia) akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa China nchini, Mhe.Wang Ke. Makabidhiano hayo yamefanyika leo katika Ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam.


Mhe. Waziri Mahiga akimpongeza Mhe. Wang kwa kuteuliwa kwake kuja kuiwakilisha Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China na kwa kuwa Mwakilishi wa kwanza mwanamke kutoka Taifa hilo nchini. Mhe Wange aliwasili nchini Tarehe 22 Oktoba 2017.  


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz Mlima (kulia) na Mkuu wa Itifaki, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Grace Martin wakifuatilia mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea mara baada ya makabidhiano.

Maafisa wa Ubalozi wa China nchini waliofuatana na Mhe. Wang wakifuatilia mazungumzo.

Mazungumzo yakiendelea.

Wakijadiliana jambo. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Bibi. Justa Nyange

Picha ya pamoja.