Tuesday, October 24, 2017

Waziri Mahiga apokea Nakala za Hati Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa China nchini.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (kulia) akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa China nchini, Mhe.Wang Ke. Makabidhiano hayo yamefanyika leo katika Ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam.


Mhe. Waziri Mahiga akimpongeza Mhe. Wang kwa kuteuliwa kwake kuja kuiwakilisha Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China na kwa kuwa Mwakilishi wa kwanza mwanamke kutoka Taifa hilo nchini. Mhe Wange aliwasili nchini Tarehe 22 Oktoba 2017.  


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz Mlima (kulia) na Mkuu wa Itifaki, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Grace Martin wakifuatilia mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea mara baada ya makabidhiano.

Maafisa wa Ubalozi wa China nchini waliofuatana na Mhe. Wang wakifuatilia mazungumzo.

Mazungumzo yakiendelea.

Wakijadiliana jambo. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Bibi. Justa Nyange

Picha ya pamoja.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.