Monday, October 16, 2017

Waziri Mwijage akutana na Balozi wa India nchini


Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage (Mb.) akizungumza na Balozi wa India nchini, Mhe. Sandeep Arya kuhusu kuimarisha ushirikiano kwenye masuala ya biashara, viwanda na uwekezaji kati ya Tanzania na India. Mazungumzo hayo yalifanyika katika Ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Jijini Dar es Salaam tarehe 16 Oktoba, 2017. Mazungumzo hayo yalihudhuriwa pia na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba (Mb.), Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz Mlima pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Bw. Magabilo Murobi (hawapo pichani).

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba (Mb.) (kushoto) akiwa na Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz Mlima (wa pili kushoto) pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Bw. Magabilo Murobi (wa kwanza kulia) wakati wa mazungumzo kati ya Mhe. Mwijage na Balozi wa India nchini (hawapo pichani).
Mhe. Dkt. Kolimba akichangia jambo wakati wa mazungumzo kati ya Waziri Mwijage na Balozi Arya.
Mazungumzo yakiendelea

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.