Tuesday, October 3, 2017

Naibu Waziri afanya mazungumzo na Balozi wa Iran chini Tanzania


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Dkt. Susan Kolimba akiwa katika mazungumzo na Balozi wa Jamhuri ya Kiislam ya Iran nchini Tanzania Mhe.Mousa Farhang. Mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ofisi za Wizara za Jijini Dar es Salaam yalijikita zaidi katika kujadili masuala mbalimbali yatakayo imarisha zaidi uhusino wa kidiplomasia uliodumu kwa kipindi cha takriban miaka 40 kati ya Mataifa hayo mawili ( Tanzania na Iran). 
Naibu Waziri Mhe. Dkt.Susan Kolimba akimsikiliza Balozi wa Jamhuri ya Kiislam ya Iran Mhe. Mousa Farhang walipokutana kwa mazungumzo Wizarani Jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri Mhe.Dkt. Kolimba na Balozi Mhe.Farhang wakiwa katika picha ya pamoja. Wapili kulia ni Balozi Innocent Shio, Afisa kutoka Wizarani Bw.Hangi Mgaka (wa kwanza kulia) na mjumbe kutoka Ubalozi wa Iran nchini (wa kwanza kushoto)

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.