Friday, October 27, 2017

Program ya Uendelezaji wa Sekta ya Uchukuzi kwa njia ya Barabara kwa Nchi Wanachama wa Jumuiya Utatu wa COMESA-EAC-SADC yazinduliwa.

Waziri wa Ujenzi, uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Prof. Makame Mbalawa akihutubia katika Mkutano wa Mawaziri wa Uchukuzi na Ujenzi wakati wa uzinduzi rasmi wa Program ya Uendelezaji wa Sekta ya Uchukuzi kwa njia ya Barabara kwa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Utatu wa COMESA-EAC-SADC. Mkutano huo ulifanyika katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Oktoba 2017.
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Balozi Liberat Mfumukeko akihutubia ambapo pamoja na mambo mengine alieleza faida zitakazopatikana kutokana na uzinduzi wa program hiyo na namna Jumuiya ya Afrika Mashariki ilivyojidhatiti kuhakikisha malengo hayo yanafikiwa kwa uhakika.
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Dkt. Leornard Chamuriho (kulia) pamoja na wajumbe kutoka nchi wanachama wakifuatilia mkutano, wa kwanza kushoto ni Balozi wa Rwanda nchini, Mhe. Eugene Kayihura
Sehemu ya wajumbe wa Tanzania wakifuatilia mkutano, wa pili kulia ni Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Bandari, Mhandisi Deusdedit Kakoko.
Sehemu ya wajumbe kutoka nchi wanachama wakifuatilia mkutano.
Meza kuu wakiongoza Mkutano.
Mkutano ukiendelea.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.