Saturday, October 28, 2017

Waziri Mahiga azitaka taasisi kutoa fursa za ajira kwa vijana

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga leo ameongea na vijana kupitia kongamano la Ubalozi Youth Forum lililofanyika katika viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam. Waziri Mahiga katika hotuba yake amewataka vijana kuchangamkia fursa zinazotolewa na Taasisi mbalimbali za Kimataifa na za ndani na makampuni binafsi. Waziri Mahiga amezitaja baadhi ya fursa hizo kuwa ni nafasi za ufadhili wa masomo ya elimu ya juu (scholarship) na mafunzo mbalimbali kama vile ujasiriamali, teknolojia, ajira na biashara.

Kongamano hilo lililenga kuwaelimisha vijana kuhusu fursa mbalimbali zinazopatikana kwenye Taasisi za Kimataifa zilizopo nchini na Makampuni binafsi na kuwahamasisha kuchangamkia fursa hizo. Vilevile kongamano hilo lilihudhuriwa na Wanadiplomasia wanaoziwakilisha nchi mbalimbali nchini Tanzania ambapo, vijana walipata fursa ya kuzungumza nao na kujifunza masuala mbalimbali kutoka kwa Wanadiplomasia hao.

Aidha katika Kongamano hilo vijana walipata fursa ya kuonesha bidhaa na huduma mbalimbali walizo zibuni, pia kuonesha bidhaa walizozalisha kutokana na miradi mbalimbali inayofadhili na Mashirika ya kimataifa. Miongoni mwa bidhaa zilizooneshwa ni mazao ya kilimo yaliyofadhiliwa na Umoja wa Mataifa (UN) chini ya mradi wa"ajira stahiki kwa vijana vijijini" (decent rural employment) ambapo hadi sasa jumla ya vijana 480 wamenufaika na mradi huo.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akifuatilia kongamano la Ubalozi Youth Forum
Sehemu ya Wanadiplomasia kutoa nchi mbalimbali Duniani wanaoziwakilisha nchi zao nchini Tanzania wakifuatila Kongamano


Waziri Mhe.Mahiga akihutubia hadhira ya Ubalozi Youth Forum

Waziri Mhe.Mhiga akiangalia moja ya bidhaa iliyobuniwa na kutengenezwa na kijana kwenye maonesho ya kongamano la Ubalozo Youth Forum yaliyofanyika katika viwanja vya  Leaders Club Jijini Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.