Friday, October 20, 2017

Ujumbe wa Mfalme wa Oman watembelea eneo la EPZA-Bagamoyo

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Mhandisi Evarist Ndikilo akimtambulisha Mkurugenzi wa Mamlaka ya Ukanda Maalum wa Uwekezaji (EPZA) kwa Waziri wa Mafuta na Gesi wa Oman mara baada ya kuwasili katika eneo la mradi wa Bandari ya Bagamoyo na kupokelewa na uongozi wa Mkoa wa Pwani, tarehe 19 Novemba 2017.

Ujumbe wa viongozi wa Serikali ya Tanzania ukiwa umeongozwa na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Mhandisi Stella Manyanya (wa sita kutoka kushoto) na Ujumbe wa Mfalme wa Oman wakiwa katika picha ya pamoja kwenye jiwe la msingi la Mradi huo. kutoka kulia Balozi wa Oman nchini Mhe. Ali Abdullah Al-Mahruqi, Balozi wa Tanzania nchini Oman, Mhe. Abdallah Kilima.

Mhe. Ndikilo akipokea zawadi kutoka kwa Mhe. Dkt. Mohammed.

Ujumbe wa Mfalme ukipokea maelezo ya Mradi wa Bandari ya Bagamoyo ambao utahusisha Maendeleo ya Maeneo Maalum ya Kiuchumi (SEZ) kutoka kwa Mhe. Ndikilo, viongozi pamoja na wataalam wengine alioambatana nao. 

Mwakilishi kutoka Mfuko wa Oman ambao pia ni mbia katika Ujenzi wa Bandari hiyo akitoa maelezo kwa viongozi. Wabia wengine katika ujenzi wa mradi huo ni pamoja na  Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Watu wa China.

===================================
Wakati huo huo Ujumbe wa Mfalme wa Oman ulipata fursa ya kutembelea eneo la kihistoria la Kaole Wilayani Bagamoyo, ambapo waliweza kusikia mengi kuhusiana na historia ya eneo hilo na kujionea maeneo mbalimbali yanayohusisha historia ya Tanzania na Oman.
Mhe. Dkt. Mohammed akinywa Maji katika kisima ambacho maji yake huwa hayakauki na hivyo iliaminika kuwa ukinywa maji hayo unaongeza siku zako za uhai.
Waandishi wa habari wakifanya mahojiano na Mhe. Dkt. Mohammed mara baada ya kumaliza ziara yake katika eneo la kihistoria la Kaole.

=======================================
Katika nafasi nyingine Wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam sambamba na wanafuzi kutoka katika shule mbalimbali za Mkoa huo walipata nafasi ya kutembelea Meli ya Mfalme wa Oman "Fulk Al salaam." kama wanavyoonekana katika picha.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.