Friday, October 20, 2017

Mkutano na waandishi wa habari kuhusu Maadhimisho ya Miaka 72 ya Umoja wa Mataifa.

 Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt Suzan Kolimba (Mb) akiongea kwenye mkutano na waandishi wa habari( Hawako pichani) kuhusu maadhimisho ya Miaka 72  ya Umoja wa Mataifa katika ukumbi wa Kimataifa wa mikutano wa Mwalimu Nyerere (JNICC), tarehe 19 Oktoba,2017, Dar es Salaam, kulia kwake ni Bw. Alvaro Rodriguez Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa Nchini na kushoto ni Balozi Celestine Mushy Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa . Mwaka huu siku hii itaadhimishwa katika viwanja vya Karimjee, Dar es Salaam Oktoba 24,2017 , Maadhimisho hayo yatafikia kilele katika tukio litakalofanyika katika Kisiwa cha Unguja, Zanzibar. Kauli mbiu ya Maadhimisho hayo mwaka huu ni "Maeendeleo ya Viwanda hayana budi kuzingatia Utunzaji Mazingira ili kuleta Maendeleo endelevu".

Baadhi ya maafisa wa Wizara na Umoja wa Mataifa, wakifuatilia mkutano huo, wa kwanza kulia ni Bi. Wendy Bigham - Naibu Mkurugenzi Mkazi wa Sihirika la Chakula Duniani(WFP), Bw. Jestus Nyamanga Mkurugenzi Msaidizi kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa na mwisho ni Bw. Charles Faini Katibu wa Naibu Waziri.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.