Wednesday, October 25, 2017

Maadhimisho ya Miaka 72 ya Umoja wa Mataifa yafana

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokelewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga mara baada ya kuwasili kwenye Viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kushiriki maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa. Maadhimisho hayo ambayo hufanyika tarehe 24 Oktoba kila mwaka yalibeba kaulimbiu isemayo "Maendeleo ya Viwanda na Utunzaji wa Mazingira kwa Maendeleo Endelevu".
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz Mlima wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Celestine Mushy wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa, Bw. Alvaro Rodriguez wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea heshima ya wimbo wa Taifa wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa.
Wageni waalikwa wakiwa wamesimama wakati wimbo wa Taifa ukipigwa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride la Heshima lililoandaliwa kwa ajili maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa, Bw. Alvaro Rodriguez wakishuhudia upandishwaji wa Bendera ya Umoja wa Mataifa (Flag Raising) ikiwa ni ishara ya kilele cha maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akitoa hotuba wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza machache wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa, Bw. Alvaro Rodriguez naye akitoa salamu za Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa.
Kikundi cha Burudani cha Wanafunzi kutoka Zanzibar kikitumbuiza wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa
Wanafunzi kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Weruweru wakiimba wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa.
Sehemu ya wageni waalikwa wakifuatilia matukio wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa, Bw. Alvaro Rodriguez akimkabidhi tuzo maalum  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kutambua ushirikiano na mchango wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa.
Mhe. Waziri Mahiga naye akipokea tuzo kutoka kwa Bw. Rodriguez. Kulia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Harrison Mwakyembe.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa yaliyopo nchini
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini.
Maafisa Mambo ya Nje ambao wameshiriki  Maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa wakiwa katika picha ya kumbukumbu
Sehemu nyingine ya Maafisa kutoka Wizara ya  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki walioshiriki  maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa.
Watumishi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakipata picha ya kumbukumbu wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa






No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.