Tuesday, November 19, 2019

USHIRIKIANO KATI YA TANZANIA NA SHIRIKA LA AALCO KUENDELEA KUIMARIKA

Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda akizungumza wakati hafla ya Maadhimisho ya Miaka 63 ya kuanzishwa kwa  Shirika la Mashauriano ya Kisheria ya Nchi za Asia na Afrika (AALCO) yaliyofanyika jijini New Delhi tarehe 15 Novemba 2019.
Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda [kushoto] akiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu wa Shirika la Mashauriano ya Masuala ya Kisheria ya Nchi za Asia na Afrika [AALCO], Prof. Kennedy Gastron wakati wa hafla ya maadhimisho ya miaka 63 ya kuanzishwa kwa shirika hilo, Jijini New Delhi tarehe 15 Novemba 2019
Mhe. Balozi Luvanda akiwa  katika meza moja na viongozi mbalimbali wakati wa maadhimisho ya miaka 63 tangu kuanzishwa kwa Shiriko la AALCO
Wageni waalikwa wakiwa kwenye maadhimisho
Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda akiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi pamoja na Maafisa Ubalozi  wa nchi wanachama wa AALCO  walioshiriki hafla ya  maadhimisho ya miaka 63 ya kuanzishwa kwa shirika hilo, Jijini New Delhi tarehe 15 Novemba 2019.
=======================================================

Ushirikiano kati ya Tanzania na Shirika la Mashauriano ya masuala ya Kisheria ya Nchi za Asia na Afrika (AALCO) kuendelea kuimarika

Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Balozi Baraka Luvanda amemwakilisha Mhe. Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Katiba na Sheria na Rais wa sasa wa Shirika la Mashauriano ya Kisheria ya Nchi za Asia na Afrika (Asia-Africa Legal Consultative Organization-AALCO) kwenye sherehe ya miaka 63 ya kuanzishwa kwake. Sherehe hiyo imefanyika Jijini New Delhi tarehe 15 Novemba 2019 na kuhudhuriwa na nchi wanachama wageni waalikwa, wenyeji na mashirika ya kimataifa yaliyopo New Delhi.

Akisoma hotuba kwa niaba ya Mhe. Mahiga, Balozi Luvanda alielezea uhusiano wa kihistoria uliopo kati ya Tanzania na AALCO na kueleza kuwa utaendelea kudumishwa kwa manufaa ya pamoja.

AALCO ilianzishwa tarehe 15 Novemba 1956 kwa lengo la kuwa chombo cha ushauri na ushirikiano katika masuala ya sheria za kimataifa kwa nchi za Asia na Afrika. Toka kuanzishwa kwake AALCO imewezesha nchi wanachama kushirikiana na kubadilishana uzoefu katika masuala mbalimbali ya sheria za kimataifa na imechangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya sheria za kimataifa.

Ushirikiano kati ya Tanzania na shirika hilo ulianza tangu mwaka 1965 ambapo Tanzania ilishiriki katika Mkutano Mkuu wa Mwaka wa AALCO kama nchi Mwangalizi na baadaye mnamo mwaka 1973 kama nchi mwanachama rasmi. 

Mpaka sasa Tanzania imeshaandaa Mikutano mikubwa 3 ya Mwaka ambapo Mkutano wa 25 wa AALCO ulifanyika mwaka 1986 jijini Arusha, Mkutano wa 49 ulifanyika Jijini Dar es Salaam mwaka 2010 na Mkutano wa 58 ulifanyika hivi karibuni, jijini Dar es Salaam tarehe 21 hadi 25 Octoba 2019.

Monday, November 18, 2019

TANZANIA YAKABIDHI SHEHENA YA KWANZA YA MBEGU ZA KOROSHO NCHINI ZAMBIA


Mhe. Hassan Simba Yahaya Balozi wa Tanzania nchini Zambia akihutubia adhira iliyojitokeza kwenye hafla fupi ya kukabidhi mbegu za korosho jimbo la Mongu, Zambia  tarehe 16 Novemba, 2019
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekabidhi 
shehena ya mbegu za korosho kwa Serikali ya Jamhuri ya 
Zambia katika hafla iliyofanyika mjini Mongu nchini humo. 

Korosho hizo zimekabidhiwa kufuatia ahadi ya Rais wa 
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe 
Magufuli aliyoitoa kwa Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. 
Edgar Lungu kwenye uzinduzi wa Kituo cha Pamoja cha 
Huduma Mpakani (OSBP) Tunduma tarehe 5 Oktoba, 2019.

Katika tukio hilo Serikali ya Tanzania iliwakilishwa na Mhe. 
Hassan Simba Yahaya Balozi wa Tanzania nchini Zambia, na

 kwa upande wa Zambia, Serikali aliwakilishwa na Waziri wa 

Jimbo la Mongu Mhe. Richard Kapita, Watendaji kutoka 

Serikalini na viongozi wa Kimila.

Akizungumza katika hafla hiyo Mhe. Kapita kwa naiba ya
 Serikali ya Jamhuri ya Zambia ametoa shukurani za pekee
 kwa Mhe. Rais Magufuli kwa  upendo aliouonesha
 kwa Zambia na kwa upekee kabisa kwa wananchi wa jimbo
 la Mongu.
 Aliongezea kusema wananchi wa Mongu 
wanamatumaini makubwa kuwa, mbegu hizo zitawapa 
chachu ya kuzalisha korosho kwa wingi na kunufaika 
kiuchumi kama ambavyo imekuwa kwa wananchi wa
 Tanzania
Mhe. Hassan Simba Yahaya Balozi wa Tanzania nchini Zambia (kushoto) na Waziri wa Jimbo la Mongu Mhe. Richard Kapita (kulia) wakijadili jambo muda mfupi kabla ya kuanza kwa hafla ya kukabidhi na kupokea korosho iliyofanyika Mongu, Zambia 
Waziri wa Jimbo la Mongu, Zambia  Mhe. Richard Kapita 

akihutubia hadhira iliyojitokeza kwenye hafla ya 

mapokezi ya mbegu za korosho
Mhe. Hassan Simba Yahaya Balozi wa Tanzania nchini Zambia, na Mhe. Mukela Manyindo Waziri Mkuu wa Jimbo la Mongu (katika ngazi ya kimila) wakikata utepe kuashiria mapokezi ya mbegu za korosho katika hafla iliyofanyika Mongu, Zambia 
Picha ya pamoja baada ya hafla ya kukabidhi mbegu za korosho
Mhe. Hassan Simba Yahaya Balozi wa Tanzania nchini Zambia (kushoto) na Afisa kutoka Ofisi za Ubalozi wa Tanzania nchini Zambia wakifuatilia tukio lililokuwa likiendelea wakati wa hafla ya kukabidhi mbegu za korosho
Shemu ya wananchi wa Mongu, Zambia waliojitokeza kwenye hafla ya mapokezi ya mbegu za korosho 



Saturday, November 16, 2019

WAZIRI WA MAMBO YA NJE, PROF. PALAMAGAMBA KABUDI AKUTANA NA WATUMISHI WA WIZARA JIJINI DODOMA


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) leo tarehe 16 Novemba 2019 amezungumza na Watumishi wa Wizara hiyo kwenye Mkutano uliofanyika jijini Dodoma. Katika hotuba yake, Mhe. Prof. Kabudi amewapongeza Watumishi hao kwa kufanikisha majukumu makubwa ya kitaifa ikiwemo Mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) uiofanyika nchini mwezi Agosti 2019 pamoja na Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Afrika na Nchi za Nordic uliofanyika nchini mwezi Novemba 2019. Pia aliwaasa kuendelea kufanya kazi kwa bidii, kujenga Umoja na mshikamano pamoja na kuwa na nidhamu na kutokata tamaa katika kutekeleza majukumu yao.


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb.) nae akiungumza wakati wa Mkutano kati ya Mhe. Waziri na Watumishi wa Wizara.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe akizungumza jambo wakati wa Mkutano kati ya Waziri na Watumishi wa Wizara.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi akichangia hoja wakati wa mkutano kati ya Waziri na Watumishi wa Wizara

Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Bw. Issa Ng'imba akitoa neno kwa Watumishi wakati wa mkutano kati yao na Mhe. Waziri

Sehemu ya Wakurugenzi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwasikiliza viongozi wa Wizara wakati wa Mkutano kati ya Waziri na Watumishi

Sehemu nyingine ya Wakurugenzi

Wakurugenzi wakifuatilia hotuba

Watumishi wa Wizara wakinukuu mazungumzo kati yao na Mhe. Waziri

Mkutano ukiendelea

Wakurugenzi wengine wakifuatilia mkutano

Watumishi wa Wizara wakiwa kwenye mkutano kati yao na Mhe. Waziri

Sehemu nyingine ya Watumishi wa Wizara kwenye mkutano

Pichani ni Watumishi wa Wizara wakisikiliza kwa makini hotuba ya Mhe. Waziri (hayupo pichani) alipozungumza nao

Sehemu nyingine ya Watumishi

Balozi Mteule, Bw. Jestus Nyamanga akiwa amesimama ili kupokea pongezi kutoka kwa Mhe. Prof. Kabudi (hayupo pichani) kwa niaba ya Watumishi wa Wizara kufuatia kuteuliwa kwake kwenye wadhifa wa Balozi hivi karibuni

Mtumishi mpya wa Wizara akijitambulisha

Mhe. Waziri Kabudi na meza kuu wakiwaongoza Watumishi wa Wizara (hawapo pichani) kuimba wimbo wa ….Tuna imani na Mhe. Rais

Watumishi wa Wizara wakiimba wimbo huo kwa furaha


Friday, November 15, 2019

TAKUKURU yakabidhiwa jalada la kufanyia uchunguzi upotevu wa fedha katika Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia


Na Mwandishi wetu,

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imeikabidhi TAKUKURU  jalada la kulifanyia uchunguzi upotevu wa fedha katika Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Mnyepe amekabidhi jalada hilo kwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Brigedia Jenerali John Mbungo katika ofisi ndogo za Wizara jijiji Dar es Salaam.

Hatua hiyo imekuja kutokana na jitihada za Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli za kupambana na kuzuia rushwa pamoja na matumizi mabaya ya fedha za uma.

Uchunguzi huo unafanyika baada ya kubainika upotevu/matumizi mabaya ya fedha katika Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia.

Kuhusu kiwango cha fedha kilichopotea Katibu Mkuu, Dkt. Mnyepe, amesema kitajulikana mara baada ya Takukuru kukamilisha uchunguzi huo wa jalada walililokabidhiwa.



Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, 
Dkt. Faraji Mnyepe akimkabidhi Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Brigedia Jenerali John Mbungo jalada la upotevu wa fedha katika Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia leo jijini Dar es Salaam

Wednesday, November 13, 2019

DOUBLE TROIKA YA SADC YAKUTANA KUJADILI HALI YA AMANI NA USALAMA DRC

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akifungua mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje pamoja na Mawaziri wa Ulinzi na vyombo vya ulinzi na usalama (double Troika) ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) Jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kushoto wake ni Katibu Mtendaji wa SADC, Dkt. Stergomena Tax na anayefuatia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Faraji Mnyepe.

Baadhi ya wajumbe wa Double Troika wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) wakiwa katika mkutano Jijini Dar es Salaam



Baadhi ya wajumbe wa Double Troika wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) wakiwa katika mkutano Jijini Dar es Salaam



Mawaziri wa mambo ya Nje, Mawaziri wa Ulinzi wa SADC wakutana kujadili hali ya Usalama na Amani DRC 

Mawaziri wa Mambo ya nchi za Nje pamoja na Mawaziri wa Ulinzi na vyombo vya ulinzi  vya Jumuiya ya Maendeleo  Kusini mwa Afrika (SADC) ijulikanao kama DOUBLE TROIKA wamekutana kwa dharura kujadili hali ya kisasa na amani katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ili kuweka mikakati ya kuendelea kuimarisha amani katika nchi hiyo.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano huo wa dharura wa DOUBLE TROIKA inayojumuisha Troika ya siasa na Troika ya Ulinzi na Usalama, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi amesema kuwa lengo la mkutano huo wa dharura ni kuweka mikakati itakayosaidia kuimarisha amani nchini Congo DRC na kumaliza migogoro inayotishia ustawi wa nchi hiyo iliyodumu kwa miongo mingi.


Aidha, Waziri Kabudi amebainisha kuwa mkutano huo utasaidia nchi za SADC zenye vikosi vya ulinzi na usalama nchini DRC yaani Tanzania, malawai na Afrika Kusini kuimarisha amani na DRC kwa kufanya tathmini na kukubaliana hatua za kuchukua ili vita na migogoro ya mara kwa mara inayoibuka Nchini Congo DRC ifikie tamati na amani ya kudumu ipatikane.

“Mkutano huu wa leo ni wa Troika ya Siasa na Troika ya ulinzi na usalama ambapo kupitia mkutano huu tunaamini kuwa tutafanya tathimini ya hali ya amani DRC na kukubaliana ni hatua gani za kuchukua,” amesema Prof. Kabudi

Katika hatua nyingine Prof. kabudi ameongeza kuwa ndani ya mwaka huu amani na demokrasia vimezidi kuimarika katika nchi wanachama wa SADC, kutokana na baadhi ya nchi wanachama kuendesha chaguzi za kidemokrasia zilizomalizika kwa amani katika nchi za Msumbiji na Botswana. 

Aidha Prof. Kabudi amesema Tanzania na Nchi 16 wanachama wa SADC bado zinaendelea kupaza sauti kwa jumuiya za kimataifa na nchi ambazo zimeiwekea vikwazo Zimbabwe kuviondoa mara moja kutokana na vikwazo hivyo kutokuwa na uhalali jambo linalosababisha mateso kwa raia wan chi hiyo hususani akina mama na watoto .

"Katika hili la Zimbabwe lazima sisi kama SADC tushikamane na kusafiri pamoja ili tufike kwa umoja wetu" Amesema Prof. kabudi.

Awali akitoa hutuba katika mkutano huo, Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya maendeleo kusini mwa Afrika(SADC), Stergomena Tax amesema kuwa ana matumaini makubwa na mkutano huo unaofanyika jijini Dar es salaam utatathimini na kutoa mapendekezo ya muda mfupi na mrefu kuhusu hali ya usalama, amani na siasa katika nchi ya Congo DRC  na ukanda wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika ili kuhakikisha ukanda huo unakuwa salama na amani

Ameongeza kuwa amani na usalama ni nyenzo mojawapo muhimu katika maendeleo ya kiuchumi na hivyo kupata maendeleo yanayohitajika kwa ajili ya mataifa ya Afrika.




VACANCY ANNOUNCEMENT


PRESS RELEASE

Vacancy announcement at the Secretariat of the Organisation for the Prohibition of Chemical Weapons (OPCW)

The Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation has received Vacancy Notice from the Secretariat of the Organisation of Chemical Weapons (OPCW) inviting qualified Tanzanians to apply for the post of Legal Adviser (Director) (D-2) available at the Secretariat.

Candidates are strongly advised to submit their applications for the vacancy online through the Organisation’s website: www.opcw.org.

The deadline for application is 18th November 2019.

Issued by:
Government Communication Unit,
Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation, Dodoma.
13th November 2019.


Tuesday, November 12, 2019

RAIS MAGUFULI: ENDELEENI NA MRADI WA KUWEKA KUMBUKUMBU SAHIHI ZA VIONGOZI

Na Mwandishi Wetu
Taasisi ya Uongozi yatakiwa kuhakikisha kuwa inaendelea na maradi wa kuweka kumbukumbu sahihi za viongozi na taifa kwa kuandika vitabu na machapisho mbalimbali yanayowahusu viongozi nchini Tanzania na barani Afrika kwa ujumla.

Wito huo umetolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli leo jijini Dar es Salaam wakati alipokuwa akizindua kitabu cha maisha ya binafsi ya Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Mhe. Benjamini William Mkapa kiitwacho 'My Life, My Purpose'.

"Napenda kutumia fursa hii, kumpongeza Rais Mstaafu, Mzee Mkapa kwa kuandika kitabu hiki na kwa mchango wake mkubwa alioutoa na anaoendelea kuutoa kwa taifa letu pia naipongeza Taasisi ya Uongozi kwa kuratibu zoezi zima la uandishi wa kitabu hiki kwa kuwa na mambo mengi mazuri" Alisema Rais Magufuli.

Mhe. Rais aliongeza kuwa kama alivyoeleza Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi, Prof. Joseph Semboja kuwa jukumu la taasisi hii ni kuwaanda, kuwaimarisha na kuwaendeleza vingozi….bila shaka kuratibu na kuchapisha machapisho mbalimbali ni sehemu ya jukumu hilo hasa barani Afrika.

"Wito wangu kwenu Taasisi ya Uongozi muangalie jinsi ya kutafsiri kitabu hiki kwa lugha ya Kiswahili…..naomba kusisitiza viongozi wastaafu wengine waandike vitabu ili kutoa chachu kwa vijana wetu ambao watakuwa viongozi wa baadae kujifunza mambo mbalimbali, tusiishie tu kwa viongozi wastaafu katika ngazi ya Urais bali hata viongozi wengine," Amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli ameongeza kuwa nitafurahi kusoma kitabu cha Maalim Seif, …….nitafurahi kusoma kitabu cha mzee Warioba…… nitafurahi kusoma kitabu cha Spika Job Ndugai kuwa nae amezaliwa kongwa.

Uzinduzi wa kitabu cha maisha binafsi ya Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Mhe. William Benjamin Mkapa kijulikanacho kwa jina la "My Life, My Purpose" ulihudhuriwa na Rais wa Mstaafu wa awamu ya pili, Mhe. Ali Hassan Mwinyi, Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Mhe. Benjamini William Mkapa na Rais wa awamu ya Nne Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na Rais wa Zanzibar, Rais wa Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein.

Mbali na kuzindua kitabu hicho, pia leo ilikuwa ni siku muhimu kwa Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu, kwani leo alikuwa akisheherekea kumbukizi ya siku yake ya kuzaliwa akiwa ametimiza miaka 81 ya kuzaliwa.

Viongozi mbalimbali waandamizi wa Serikali waliohudhuria uzinduzi wa kitabu hicho ni pamoja na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Katibu Mkuu Kiongozi John Kijazi, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai na Balozi wa Finland Nchini Tanzania Riita Swan  

Wengine ni Waziri Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Sinde Warioba, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba Kabudi, Waziri wa Elimu na Sayansi, Prof. Joyce Ndalichako,  Mabalozi, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Bw. Amon Mpanju, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Paul Makonda, viongozi wa vyombo vya ulinzi na Usalama, wakuu wa mikoa, viongozi wa dini, wakuu wa taasisi mbalimbali na asasi za kiraia.

Awali akimkaribisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Rais Mstaafu Mhe. Benjamin Mkapa alimpongeza Rais Magufuli kwa jitihada zake za kuhakikisha kuwa taifa linajitegemea hasa katika maendeleo.

"Kujitegemea ni muhimu sana kama nchi, na ni muhimu kwa heshima ya taifa letu" amesema Rais Mkapa.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli wa pili kushoto akiwa ameshika kitabu cha My Life, My Purpose katika picha ya pamoja na Rais mstaafu wa awamu ya pili, Mhe. Ali Hassan Mwinyi, Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Mhe. William Benjamin Mkapa na Rais wa awamu ya Nne Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na Rais wa Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein. 
Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Mhe. William Benjamin Mkapa akimkabidhi nakala ya kitabu cha 'My Life, My Purpose' Rais John Pombe Joseph Magufuli mara baada ya uzinduzi wa kitabu hicho. Rais mstaafu wa awamu ya pili, Mhe. Ali Hassan Mwinyi na Rais mstaafu wa awamu ya Nne Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akizindua rasmi kitabu cha 'My Life, My Purpose' wengine ni Rais mstaafu wa Awamu ya pili, Mhe. Ali Hassan Mwinyi, Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Mhe. William Benjamin Mkapa na Rais Mstaafu wa awamu ya Nne Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akitoa hotuba yake wakati wa uzinduzi wa kitabu cha 'My Life, My Purpose' chenye historia ya maisha binafsi ya Rais Mstaafu Mhe. Benjamin Mkapa
Balozi wa Finland Nchini Tanzania Riita Swan akitoa hotuba yake wakati wa uzinduzi wa kitabu cha 'My Life, My Purpose' chenye historia ya maisha binafsi ya Rais Mstaafu Mhe. Benjamin Mkapa
Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Mhe. William Benjamin Mkapa akimkaribisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli wakati alipowasili ukumbini kwa ajili ya uzinduzi wa kitabu cha 'My Life, My Purpose'. Kushoto ni Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, akiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba Kabudi, Waziri wa Elimu na Sayansi, Prof. Joyce Ndalichako,  Mabalozi, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Bw. Amon Mpanju. Wengine kushoto ni Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa pamoja na Mke wa Rais Mkapa, mama Anna Mkapa.