Saturday, November 16, 2019

WAZIRI WA MAMBO YA NJE, PROF. PALAMAGAMBA KABUDI AKUTANA NA WATUMISHI WA WIZARA JIJINI DODOMA


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) leo tarehe 16 Novemba 2019 amezungumza na Watumishi wa Wizara hiyo kwenye Mkutano uliofanyika jijini Dodoma. Katika hotuba yake, Mhe. Prof. Kabudi amewapongeza Watumishi hao kwa kufanikisha majukumu makubwa ya kitaifa ikiwemo Mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) uiofanyika nchini mwezi Agosti 2019 pamoja na Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Afrika na Nchi za Nordic uliofanyika nchini mwezi Novemba 2019. Pia aliwaasa kuendelea kufanya kazi kwa bidii, kujenga Umoja na mshikamano pamoja na kuwa na nidhamu na kutokata tamaa katika kutekeleza majukumu yao.


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb.) nae akiungumza wakati wa Mkutano kati ya Mhe. Waziri na Watumishi wa Wizara.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe akizungumza jambo wakati wa Mkutano kati ya Waziri na Watumishi wa Wizara.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi akichangia hoja wakati wa mkutano kati ya Waziri na Watumishi wa Wizara

Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Bw. Issa Ng'imba akitoa neno kwa Watumishi wakati wa mkutano kati yao na Mhe. Waziri

Sehemu ya Wakurugenzi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwasikiliza viongozi wa Wizara wakati wa Mkutano kati ya Waziri na Watumishi

Sehemu nyingine ya Wakurugenzi

Wakurugenzi wakifuatilia hotuba

Watumishi wa Wizara wakinukuu mazungumzo kati yao na Mhe. Waziri

Mkutano ukiendelea

Wakurugenzi wengine wakifuatilia mkutano

Watumishi wa Wizara wakiwa kwenye mkutano kati yao na Mhe. Waziri

Sehemu nyingine ya Watumishi wa Wizara kwenye mkutano

Pichani ni Watumishi wa Wizara wakisikiliza kwa makini hotuba ya Mhe. Waziri (hayupo pichani) alipozungumza nao

Sehemu nyingine ya Watumishi

Balozi Mteule, Bw. Jestus Nyamanga akiwa amesimama ili kupokea pongezi kutoka kwa Mhe. Prof. Kabudi (hayupo pichani) kwa niaba ya Watumishi wa Wizara kufuatia kuteuliwa kwake kwenye wadhifa wa Balozi hivi karibuni

Mtumishi mpya wa Wizara akijitambulisha

Mhe. Waziri Kabudi na meza kuu wakiwaongoza Watumishi wa Wizara (hawapo pichani) kuimba wimbo wa ….Tuna imani na Mhe. Rais

Watumishi wa Wizara wakiimba wimbo huo kwa furaha


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.