Friday, November 22, 2019

Tanzania yashiriki Mkutano kuhusu Madini ya Almasi nchini India

Tanzania inashiriki katika Mkutano wa  Mwaka kwa Nchi Wanachama wa KIMBERLEY PROCESSING SCHEME, unaofanyika Jijini New Delhi nchini India. Ujumbe wa Tanzania  katika mkutano huo  unaongozwa na  Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Stanslaus Nyongo. Mkutano huo unahusu nchi wazalishaji wa Madini ya  Almasi  na udhibiti wa biashara ya almasi  duniani. Ushiriki  wa Tanzania katika mkutano huo unalenga  katika  kupata uzoefu  kutoka nchi nyingine zinazofanya vizuri katika biashara ya Madini hayo ghali duniani.
Mkutano ukiendelea

Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Stanslaus Nyongo akiwa na Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka H. Luvanda alipotembelea Ubalozi huo tarehe 20 Novemba 2019 na kufanya mazungumzo na  Balozi  Luvanda.

Mhe. Nyongo na Balozi Luvanda wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Watumishi wa Ubalozi wa Tanzania nchini India.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.