Saturday, November 30, 2019

Tanzania na Nambia zaweka Mikakati ya Kujiimarisha Kiuchumi




Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Wilbroad Kayombo akifanya utambulisho wa viongozi wa Tanzania wanaoshiriki mkutano wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Namibia unaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC).
Waliokaa mstari wa mbele ni Makatibu Wakuu na Naibu Katibu Wakuu wanaoshiriki mkutano wa JPC ambao walikuwa wanatambulishwa na Bw. Kayombo.
Viongozi katika Meza Kuu. Kutoka kulia ni Balozi wa Namibia nchini Tanzania, Mhe. Theresia Samaria; Katibu Mkuu wa Wizara ya Uhusiano na Ushirikiano wa Kimataifa ya Namibia, Balozi Selma Ashipala-Musavyi, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji K. Mnyepe na Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Prof. Joseph Buchweishaija.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji K. Mnyepe ambaye ni Mwenyekiti Mwenza wa Mkutano wa JPC ngazi ya Makatibu Wakuu akisoma hotuba ya ufunguzi ya Mkutano wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Namibia.
Dkt. Mnyepe akiendelea kusoma hotuba, huku wajumbe wakimsikiliza.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Uhusiano na Ushirikiano wa Kimataifa ya Namibia, Balozi Selma Ashipala-Musavyi ambaye ni Mwenyekiti mwenza akisoma hotuba ya ufunguzi katika mkutano huo.
Wajumbe wanaoshiriki kikao cha JPC wakifuatilia hotuba za viongzo zilizokuwa zinawasilishwa.
Makatibu Wakuu wa Wizara za Mambo ya Nje za Tanzania na Namibia, Dkt. Faraji K. Mnyepe na Balozi Selma Ashipala-Musavyi wakipongezana baada ya kuwasilisha hotuba za ufunguzi katika Mkutano wa JPC kati ya Tanzania na Namibia.
Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Elizabeth Rwetunga akiongoza wajumbe wa mkutano kupitia rasimu ya taarifa ya masuala waliyoyajadili na kukubaliana.
Watumishi kutoka Taasisi za Serikali wakifuatilia Mkutano wa JPC.

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Wilbroad Kayombo akiongea na vyombo vya habari kuhusu mkutano wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Namibia. 
Makatibu Wakuu wa Wizara za Mambo ya Nje za Tanzania na Namibia, Dkt. Faraji K. Mnyepe (mwenye suti) na Balozi Selma Ashipala-Musavyi wakiongea na waandishi wa habari kuhusu JPC kati ya Tanzania na Namibia.


Viongozi wa Tanzania na Namibia wakiwa katika picha ya pamoja.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.