Tuesday, December 3, 2019

Tanzania na Namibia Zajizatiti kukuza Biashara baina yao


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akisalimiana na Waziri wa Uhusiano na Ushirikiano wa Kimataifa wa Namibia, Mhe. Netumbo Nandi-Ndaitwah mara baada ya Mhe. Nandi-Ndaitwah kuwasili katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere kwa ajili ya kushiriki mkutano wa Tume ya Kudumu ya  Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Namibia.
Naibu Waziri Mkuu naWaziri wa Uhusiano na Ushirikiano wa Kimataifa wa Namibia, Mhe. Netumbo Nandi-Ndaitwah akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa AAfrika Mashariki, Dkt. Faraji K. Mnyepe.

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Uhusiano na Ushirikiano wa Kimataifa wa Namibia, Mhe. Netumbo Nandi-Ndaitwah akiangalia picha za matukio ya wapigania uhuru wa nchi za Kusini mwa Afrika ikiwemo Namibia.

Naibu Waziri Mkuu naWaziri wa Uhusiano na Ushirikiano wa Kimataifa wa Namibia, Mhe. Netumbo Nandi-Ndaitwah akiweka saini Kitabu cha Wageni alipowasili Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwasilisha hotuba yake wakati wa kuhitimisha Mkutano wa pili wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Namibia leo jijini Dar es Salaam. Wengine kutoka kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Uhusiano na Ushirikiano wa Kimataifa wa Namibia, Balozi Selma Ashipala-Musavyi, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Uhusiano na Ushirikiano wa Kimataifa wa Namibia, Mhe. Netumbo Nandi-Ndaitwah, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (Mb), Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko, (Mb) pamoja na Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Innocent Bashungwa, (Mb)
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Uhusiano na Ushirikiano wa Kimataifa wa Namibia, Mhe. Netumbo Nandi-Ndaitwah akiwasilisha hotuba yake wakati wa kuhitimisha Mkutano wa pili wa Tume ya Kudumu ya pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Namibia leo jijini Dar es Salaam. Wenginine kutoka kushoto ni  Katibu Mkuu wa Wizara ya Uhusiano na Ushirikiano wa Kimataifa wa Namibia, Balozi Selma Ashipala-Musavyi, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb), Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (Mb), Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko (Mb) pamoja na Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Innocent Bashungwa (Mb)
Baadhi ya Makatibu Wakuu, maafisa waandamizi wa Serikali, maafisa wa Serikali pamoja na waandishi wa habari wakifuatilia ufunguzi wa mkutano wa JPC leo jijini Dar es Salaam
Naibu Waziri Kuu na Waziri wa Uhusiano na Ushirikiano wa Kimataifa wa Namibia, Mhe. Netumbo Nandi-Ndaitwah na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (Mb) wakiweka saini Hati ya Makubaliano ya kushirikiana katika Utamaduni, Sanaa na Michezo kati ya Tanzania na Namibia. 

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Uhusiano na Ushirikiano wa Kimataifa wa Namibia, Mhe. Netumbo Nandi-Ndaitwah na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (Mb) wakibadilishana Hati ya Makubaliano ya kushirikiana katika Utamaduni, Sanaa na Michezo kati ya Tanzania na Namibia.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Uhusiano na Ushirikiano wa Kimataifa wa Namibia, Mhe. Netumbo Nandi-Ndaitwah wakisaini Hati ya Makubaliano ya kushirikiana katika Masuala ya Utalii kati ya Tanzania na Namibia

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Uhusiano na Ushirikiano wa Kimataifa wa Namibia, Mhe. Netumbo Nandi-Ndaitwah wakibadilishana Hati ya Makubaliano ya kushirikiana katika Masuala ya Utalii kati ya Tanzania na Namibia.

Meza kuu katika picha ya pamoja ikiongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb), Balozi wa Namibia nchini Tanzania Mhe. Theresia Samaria Naibu Waziri Mkuu na Waziri Wizara ya Uhusiano na Ushirikiano wa Kimataifa ya Namibia, Mhe. Netumbo Nandi-Ndaitwah, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (Mb), Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko, (Mb) na Waziri wa Viwanda Mhe. Innocent Bashungwa, (Mb) Pamoja na Makatibu Wakuu, na Viongozi waandamizi wa Serikali.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.