Wednesday, December 25, 2019

WATALII ZAIDI YA 450 KUTOKA ISRAEL WAKO NCHNI KUTEMBELEA VIVUTIO VYA UTALII




Watalii kutoka nchini Israel walipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) watalii hao wako nchini kwa ajili ya kutembelea vivutio vya utalii nchini wakati huu wa Siku Kuu za Krismasi na Mwaka mpya.
Watalii kutoka nchini Israel wakiingia ndani ya uwanja wa  Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) baada ya kuwasili nchini kwa ajili ya kutembelea vivutio vya utalii wakati wa mapumziko ya mwisho wa mwaka na Siku Kuu za Krismasi na Mwaka mpya

Watalii kutoka nchini Israel wakielekea sehemu maalum iliyoandaliwa kwa ajili ya mapokezi yao baada ya kuwasili nchini kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) watalii hao wako nchini kwa ajili ya kutembelea vivutio vya utalii nchini wakati wa mapumziko ya mwisho wa Mwaka na Siku Kuu za Krismasi na Mwaka mpya wa 2020.

Watalii kutoka nchini Israel wakiwa ndani ya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) baada ya kuwasili nchini  kwa ajili ya kutembelea vivutio vya utalii wakati wa Siku Kuu za Krismasi na Mwaka mpya wa 2020.


Kikundi cha ngoma cha Kimasai kikiwa ndani ya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro kwa ajili ya kutumbuiza wakati wa hafla ya kuwapokea  Watalii kutoka nchini Israel waliowasili nchini  kwa ajili ya kutembelea vivutio vya utali.

Mwenyekiti wa Bodi ya Utalii nchini (TTB) Jaji Mst. Mhe. Thomas Mihayo (wa pili kulia) akiwa na Mkurugrenzi Mtendaji wa TTB Bi Devota Mdachi wa (kwanza kushoto) wakiwa na baadhi ya watalii kutoka nchini Israel mara baada ya kuwapokea katika Uwanja wa KIA walipowasili nchini kwa ajili ya kutembelea vivutio vya utalii.


Watalii zaidi ya 450 kutoka Israel wamewasili nchini kwa ajili ya kutembelea vivutio vya kitalii vilivyoko kaskazini mwa Tanzania. Watalii hao wamekuja nchini kwa kutumia ndege binafsi na za kawaida.
 
Kundi la kwanza la watalii 150 liliwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kilimanjaro (KIA) tarehe 21 Desemba 2019 na kupokelewa na Bodi ya Utalii nchini (TTB) na baadaye kuelekea katika vivutio vya utalii vilivyoko mkoani Arusha.

Kundi la pili na la tatu lililokuwa na watalii 313 limewasili nchini kupitia Uwanja wa Ndege KIA  tarehe 24 Desemba 2019.

Watalii hao wako nchini kwa ajili ya kusherehekea sikukuu za Krismasi na Mwaka mpya wanatembelea Hifadhi za Taifa za Serengeti, Tarangire, Ziwa Manyara, Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorogoro na Bonde la Eyasi.

Ubalozi wa Tanzania nchini Israel umetoa viza zaidi ya 500 kwa Waisrael ambao wamepanga kuwasili nchini kwa kutumia Mashirika ya Ndege ya Ethiopia, Uturuki na Uswisi katika kipindi hiki cha siku kuu za mwisho wa mwaka  huku ukiendelea kuratibu ziara nyingine ya watalii zaidi ya 800 ambao mchakato wa safari yao upo katika hatua za mwisho.

Ujio wa watalii hao unatokana na jitihada za kuvutia watalii zinazofanywa na Ofisi ya Ubalozi nchini Israel kwa kushirikiana na makampuni ya wakala wa utalii ya ndani na nje ya nchi ili kuunga mkono harakati za Serikali za kukuza pato la taifa kupitia utalii na hivyo kuiletea nchi maendeleo.

       

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.