Saturday, December 7, 2019

MHE.WILLIAM RUTO AFUNGUA MKUTANO WA BARAZA LA MAWAZIRI WA ACP

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Kenya Mhe. William Ruto akifungua Mkutano wa 110 wa Baraza la Mawaziri kwa Nchi za Afrika,Caribbean na Pacific (ACP) katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Kenyatta (KICC) unaoendelea Nairobi-Kenya
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwa katika mkutano wa Baraza la Mawaziri wa nchi za Afrika,Caribbean na Pacific (ACP) unaoendelea Katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Kenyatta (KICC) Jijini Nairobi,Kenya

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwa anajadiliana jambo na Balozi anayeiwakilisha Tanzania Nchini Ubelgiji na Jumuiya ya Ulaya (EU) Balozi Jestas Nyamanga wakati wa Mkutano wa 110 wa nchi za Afrika,Caribbean na Pacific (ACP) ukiendelea Katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Kenyatta (KICC) Jijini Nairobi-Kenya.

Balozi wa Tanzania Nchini Kenya Balozi Pindi Chana akiwa anafuatilia mijadala mbalimbali katika mkutano wa 110 wa Baraza la Mawaziri wa nchi za Afrika,Caribbean na Pacific (ACP) unaoendelea Katinka ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Kenyatta (KICC)  Jijini Nairobi - Kenya



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.