Thursday, December 19, 2019

WAZIRI KABUDI AKUTANA, KUFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA UFARANSA NCHINI


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania, Mhe. Frederic Clavier.

Mazungumzo hayo yamefanyika leo jijini Dar es Salaam ambapo Waziri Kabudi amemueleza Mhe. Balozi Clavier kuwa, uhusiano baina ya Tanzania na Ufaransa ni wa muda mrefu ambapo hadi sasa Tanzania imekuwa na mahusiano imara na taifa hilo.

Aidha, pamoja na mambo mengine, mazungumzo yao yalijikita katika kuongeza ushirikiano baina ya Tanzania na Ufaransa, kuongeza ushirikino wa maendeleo, kuimarisha uwekezaji, biashara pamoja na kuimarisha masuala ya ulinzi na usalama.



Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania, Mhe. Frederic Clavier akimuelezea jambo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) wakati balozi huyo alipokutana na Mhe. Waziri leo katika ofisi ndogo za wizara Jijini Dar es Salaam
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akimuelezea jambo Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania, Mhe. Frederic Clavier wakati alipokutana na balozi huyo leo katika ofisi ndogo za wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akimsisitiza jambo Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania, Mhe. Frederic Clavier wakati alipokutana na balozi huyo leo katika ofisi ndogo za wizara Jijini Dar es Salaam

Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania, Mhe. Frederic Clavier akimfafanulia jambo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) wakati balozi huyo alipokutana na Mhe. Waziri leo katika ofisi ndogo za wizara Jijini Dar es Salaam



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akipokea zawadi kutoka kwa Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania, Mhe. Frederic Clavier






No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.