Tuesday, November 26, 2019

MKUTANO WA 39 WA BARAZA LA MAWAZIRI WA EAC KUANZA KESHO JIJINI ARUSHA

 Baadhi ya washiriki wa Mkutano wa 39 wa Baraza la Mawaziri wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakifuatilia mkutano katika ngazi ya Makatibu Wakuu uliomalizika leo Jijini Arusha
 Makatibu Wakuu Jumuiya ya Afrika Mashariki wakijadili jambo wakati wa Mkutano wao. Kushoto ni Katibu Mkuu, Wizara ya Afrika Mashariki - Uganda, Bibi. Edith Mwanje, akifuatiwa na Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki - Tanzania, Dkt. Faraji Mnyepe. Wengine ni Katibu Mkuu, Wizara ya Biashara, Viwanda na Masula ya EAC - Sudani Kusini, Bw. Mou Mou Athian Kuol, akifuatiwa na Meja Generali, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa - Uganda, Balozi Charles Karamba. Wengine pichani ni Katibu Mwandamizi, Wizara ya Afrika Mashariki na - Kenya, Dkt. Margaret Mwakima na katibu Mkuu, Office ya Rais Inayohusu masula ya Afrika Mashariki - Burundi, Balozi Jean Rigi. 



Makatibu Wakuu Jumuiya ya Afrika Mashariki wakifuatilia mkutano wao (Ngazi ya Makatibu Wakuu) uliomalizika leo jijini Arusha
Mkurugenzi wa Idara ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Stephen Mbundi akiwasilisha mada kwa Makatibu wakuu (hawapo pichani) wakati wa mkutano wa Makatibu wakuu wa EAC Jijini Arusha

   

Mkutano wa 39 wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki unatarajiwa kwanza kesho tarehe 27 Novemba 2019  jijini Arusha.

Kuanza kwa mkutano huo kunafuatia kukamilika kwa Mkutano wa ngazi ya Makatibu Wakuu wa nchi wanachama wa Jumuiya hiyo ulioanza tarehe 25 na kumalizika tarehe 26 Novemba 2019.

Mkutano wa Makatibu Wakuu  pamoja na mambo mengine, umejadili masuala mbalimbali ya utekelezaji ya jumuiya ya Afrika Mashariki na kutoa mapendekezo kwa mkutano wa ngazi ya Mawaziri wa Wizara za Kisekta zinazohusiana na Jumuiya hiyo utakaoanza  tarehe 27 Novemba 2019.

Mkutano huu wa 39 wa Baraza la Mawaziri wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki umeandaliwa kwa lengo la kujadili na kukubabaliana na agenda zitakazowasilishwa kwenye Mkutano wa 21 wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya hiyo utakaofanyika Februari, 2020.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.