Monday, November 18, 2019

TANZANIA YAKABIDHI SHEHENA YA KWANZA YA MBEGU ZA KOROSHO NCHINI ZAMBIA


Mhe. Hassan Simba Yahaya Balozi wa Tanzania nchini Zambia akihutubia adhira iliyojitokeza kwenye hafla fupi ya kukabidhi mbegu za korosho jimbo la Mongu, Zambia  tarehe 16 Novemba, 2019
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekabidhi 
shehena ya mbegu za korosho kwa Serikali ya Jamhuri ya 
Zambia katika hafla iliyofanyika mjini Mongu nchini humo. 

Korosho hizo zimekabidhiwa kufuatia ahadi ya Rais wa 
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe 
Magufuli aliyoitoa kwa Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. 
Edgar Lungu kwenye uzinduzi wa Kituo cha Pamoja cha 
Huduma Mpakani (OSBP) Tunduma tarehe 5 Oktoba, 2019.

Katika tukio hilo Serikali ya Tanzania iliwakilishwa na Mhe. 
Hassan Simba Yahaya Balozi wa Tanzania nchini Zambia, na

 kwa upande wa Zambia, Serikali aliwakilishwa na Waziri wa 

Jimbo la Mongu Mhe. Richard Kapita, Watendaji kutoka 

Serikalini na viongozi wa Kimila.

Akizungumza katika hafla hiyo Mhe. Kapita kwa naiba ya
 Serikali ya Jamhuri ya Zambia ametoa shukurani za pekee
 kwa Mhe. Rais Magufuli kwa  upendo aliouonesha
 kwa Zambia na kwa upekee kabisa kwa wananchi wa jimbo
 la Mongu.
 Aliongezea kusema wananchi wa Mongu 
wanamatumaini makubwa kuwa, mbegu hizo zitawapa 
chachu ya kuzalisha korosho kwa wingi na kunufaika 
kiuchumi kama ambavyo imekuwa kwa wananchi wa
 Tanzania
Mhe. Hassan Simba Yahaya Balozi wa Tanzania nchini Zambia (kushoto) na Waziri wa Jimbo la Mongu Mhe. Richard Kapita (kulia) wakijadili jambo muda mfupi kabla ya kuanza kwa hafla ya kukabidhi na kupokea korosho iliyofanyika Mongu, Zambia 
Waziri wa Jimbo la Mongu, Zambia  Mhe. Richard Kapita 

akihutubia hadhira iliyojitokeza kwenye hafla ya 

mapokezi ya mbegu za korosho
Mhe. Hassan Simba Yahaya Balozi wa Tanzania nchini Zambia, na Mhe. Mukela Manyindo Waziri Mkuu wa Jimbo la Mongu (katika ngazi ya kimila) wakikata utepe kuashiria mapokezi ya mbegu za korosho katika hafla iliyofanyika Mongu, Zambia 
Picha ya pamoja baada ya hafla ya kukabidhi mbegu za korosho
Mhe. Hassan Simba Yahaya Balozi wa Tanzania nchini Zambia (kushoto) na Afisa kutoka Ofisi za Ubalozi wa Tanzania nchini Zambia wakifuatilia tukio lililokuwa likiendelea wakati wa hafla ya kukabidhi mbegu za korosho
Shemu ya wananchi wa Mongu, Zambia waliojitokeza kwenye hafla ya mapokezi ya mbegu za korosho 



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.