Sunday, March 26, 2023

SAUDI ARABIA YAANZA RASMI SAFARI ZA NDEGE MOJA KWA MOJA HADI TANZANIA

Shirika la Ndege la Saudi Arabia limeanza rasmi safari za ndege za moja kwa moja kutoka Saudia Arabia hadi Tanzania. 

Akiongea katika hafla ya mapokezi ya Ndege ya Shirika la Ndege la Saudia Jijini Dar es Salaam, Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa (Mb) amesema kuanzishwa kwa safari za moja kwa moja kutoka Saudia hadi Tanzania ni moja ya matunda ya ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan aliyofanya nchini Saudi Arabia Mwezi, Juni 2022. 

“Kuanzishwa kwa safari hizi, kutachangia kuimarisha mazingira ya kibiashara na uwekezaji yatakayopelekea uhitaji wa usafiri wa anga wa moja kwa moja kutoka Tanzania kwenda Saudi Arabia,” Alisema Prof. Mbarawa

Prof. Mbarawa aliongeza kuwa kwa mujibu wa takwimu za Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) za mwaka 2022, idadi ya abiria wa kimataifa nchini imeongezeka kwa asilimia 55 kutoka abiria 1,694,085 katika mwaka 2021 hadi kufikia abiria 2,618,119 mwaka 2022. 

“Awali abiria walilazimika kupitia mataifa mengine ili kufika Saudi Arabia, uzoefu unaonyesha kuwa walitumia takribani saa kumi ili kukamilisha safari zao. Hivyo, kwa kutumia Shirika hili, abiria wataweza kusafiri kwenda Jeddah moja kwa moja na watatumia saa Nne na dakika arobaini,” aliongeza Prof. Mbarawa.

Akizungumza katika hafla hiyo, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb.) alisema kuanzishwa kwa safari za moja kwa moja kutoka Saudia Arabia hadi Tanzania ni matokea ya uhusiano na ushirikiano mzuri uliopo kati ya mataaifa hayo.

“Tunategemea kupitia safari hizi tutakuza na kuimarisha biashara, uwekezaji, viwanda na utalii nchini……..kwa sasa Urari wa biashara kati ya Tanzania na Saudia Arabia umefikia Dola za Kimarekani 18,000,0000,” alisema Balozi Mbarouk. Tanzania imekuwa ikiuza bidhaa mbalimbali nchini Saudi Arabia hususan nyama, matunda na maua.

Naye Kaimu Balozi wa Saudi Arabia nchini, Bw. Fahad Alharbi alisema Saudi Arabia imefurahi kuanzishwa kwa safari hiyo ya kihistoria na yote hiyo imewezekana kutokana na uhusiano mzuri ilionao na Serikali ya Tanzania.

“leo tumeshuhudia uzinduzi rasmi wa safari za ndege za moja kwa moja kutoka Saudi Arabia hadi Tanzania. Ni Imani yangu kuwa safari hizi zitachangia kuimarisha biashara na uwekezaji, utalii pamoja na usafirishaji kwa kiasi kikubwa," alisema Bw.  Alharbi. Shirika la Ndege la Saudi Arabia litafanya safari zake kuja nchini mara nne kwa wiki. 

Februari, 2023 Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia Mhe. Ali Mwadini na Meneja Mkuu wa Masoko, Kanda ya Kati wa Shirika la Ndege la Saudi Arabia Bw. Abdulrahman Alabdulwahab walikutana na kujadili maandalizi ya uzinduzi wa safari za ndege za moja kwa moja kati ya Tanzania na Saudi Arabia.

Pamoja na mambo mengine, viongozi hao pia walijadili mikakati ya kutangaza vivutio vya utalii vya Tanzania ili kuongeza idadi ya watalii na kurahisisha usafirishaji wa bidhaa za Tanzania hususan nyama na matunda.

Hafla ya uzinduzi wa safari za ndege za moja kwa moja kutoka Saudi Arabia hadi Tanzania zilihudhuriwa pia na Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia Mhe. Ali Mwadini, Balozi wa Comoro Nchini Tanzania, Mhe. Dkt. Ahmada El Badaoui Mohamed pamoja na viongozi wengine wa Serikali.

Ndege ya Shirika la Ndege la Saudi Arabia ikiwasili rasmi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam 

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa safari za ndege za moja kwa moja kutoka Saudi Arabia hadi Tanzania

Wageni wakipokelewa baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam

Picha ya pamoja 


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,akiwasilisha salamu za Wizara katika hafla ya mapokezi ya Ndege ya Shirika la Ndege la Saudia Jijini Dar es Salaam
Kaimu Balozi wa Saudi Arabia nchini, Bw. Fahad Alharbi akitoa salamu za Saudi Arabia katika hafla ya mapokezi ya Ndege ya Shirika la Ndege la Saudia Jijini Dar es Salaam 






Friday, March 24, 2023

TANZANIA – KOREA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA KUKUZA BIASHARA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) ameeleza kuwa Serikali na wadau inaendelea kuweka jitihada katika kuboresha mazingira ya biashara baina ya Tanzania na Jamhuri ya Korea ili kuendelea kuinua kiwango cha biashara na uwekezaji baina ya nchi hizi mbili. 

Waziri Dkt. Tax ameeleza hayo alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini Mhe. Kim, Sun Pyo mapema leo tarehe 24 Machi 2023 jijini Dodoma. 

Dkt. Tax amemuhakikishia Balozi Kim kuwa Serikali ya Tanzania itaendelea kushirikiana na kufanya kazi kwa karibu na Jamhuri ya Korea ili kuwezesha biashara baina ya pande hizo mbili inaendelea kushamiri zaidi tofauti na ilivyo sasa. Dkt. Tax ameeleza baadhi ya hatua zinazochukuliwa na Serikali ya Tanzania ni pamoja na kuendelea kutekeleza na kubuni programu zinazolenga kuongeza mwingiliano wa watu (people to people exchange) kati ya Tanzania na Jamhuri ya Korea. 

Kwa mujibu wa takwimu za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) za mwaka 2020, Korea iliagiza bidhaa zenye thamani ya shilingi za Tanzania bilioni 340.3 kutoka Tanzania, huku Tanzania ikiagiza bidhaa zenye thamani ya shilingi bilioni 290.3 kutoka Jamhuri ya Korea.

Kwa upande wake Balozi Kim, Sun Pyo ameeleza kuwa Jamhuri ya Korea inaendelea kuwahamasisha watu wake kuchangamkia fursa mbalimbali za biashara zinazopatikana nchini ikiwemo katika sekta ya kilimo, viwanda, ujenzi wa miundombinu, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano na Utalii. 

Takwimu kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) zinaonyesha kuwa katika kipindi cha miaka saba (2015-2022), Korea imewekeza nchini dola za Kimarekani milioni 18.01 katika sekta mbalimbali zikiwemo za kilimo, ujenzi na usafirishaji na uchukuzi. Uwekezaji huo unakadiriwa kuzalisha fursa za ajira zipatazo 531. 

Mbali na hayo Waziri Tax ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Korea kwa kuendelea kushirikiana na Tanzania katika utekelezaji wa miradi na programu mbalimbali zinazolenga kuboresha hali ya maisha ya watu ikiwemo elimu, afya, kuendeleza uchumi wa buluu, kilimo, Teknolojia ya Habari na ujenzi wa miundombinu. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) na Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini Mhe. Kim, Sun Pyo wakiwa katika picha ya pamoja walipokutana kwa mazungumzo jijini Dodoma
 Mazungumzo yakiendelea.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo na Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini Mhe. Kim, Sun Pyo yaliyofanyika jijini Dodoma
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax akimsikiliza Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini Mhe. Kim, Sun Pyo walipokuwa kwenye mazungumzo jijini Dodoma
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) na Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini Mhe. Kim, Sun Pyo wakiwa katika picha ya pamoja walipokutana kwa mazungumzo jijini Dodoma

Thursday, March 23, 2023

DKT. TAX AKUTANA NA BALOZI WA SWEDEN NA MWAKILISHI MKAZI WA ICRC

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) amekutana na Balozi wa Ufalme wa Sweden nchini, Mhe. Charlotta Ozaki Macias na Mwakilishi Mkazi wa Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu Duniani (ICRC) Bw. Bart Vermeiren  ofisini kwake jijini Dodoma.

Akizungumza na Balozi wa Sweden nchini, Dkt. Tax amemuhakikishia Balozi huyo kuwa Tanzania itaendelea kudumisha uhusiano wa kihistoria na kidiplomasia baina ya nchi hizo mbili na kusimamia miradi ya ushirikiano kwa maendeleo na ustawi wa watu wake.

Pia ameishukuru Serikali ya Sweden kwa kuendelea kushirikiana na Tanzania katika sekta za elimu; afya; Uwekezaji na biashara; Teknolojia ya Habari, Usafirishaji na  Miundombinu; Nishati; Madini; Utafiti; maboresho kwenye mifumo ya ukusanyaji wa kodi; uchangiaji wa bajeti kuu ya Serikali; Misuti; Demokrasia, Haki za binadamu, Usawa wa jinsia; Utunzaji wa mazingira; na Mabadiliko ya Tabia Nchi.

Naye Balozi Charlotta Macias ameeleza kuwa wakati huu ambapo Tanzania na Sweden inaadhimisha miaka 60 tangu kuanzishwa rasmi kwa ushirikiano wa kidiplomasia ingependa kushirikiana na Tanzania katika shughuli mbalimbali zilizoandaliwa katika kuadhimisha kumbukumbu hiyo.

Aidha, amefafanua kuwa miongoni mwa shughuli za maadhimisho hayo ni; Kukutana na Wahitimu wa kitanzania waliosoma nchini Sweden katika ngazi mbalimbali ambapo watajadili shughuli wanazozifanya na malengo yao ya baadae.

Vilevile akafafanua kuwa shughuli kama hizo za maadhimisho zitakuwa zikifanyika na ofisi za Ubalozi wa Tanzania nchini Sweden ambapo hivi karibuni kuliitishwa mkutano mkubwa wa Watanzania wanaoishi nchini Sweden ambao kwa upande wa Serikali ya Tanzania uliwakilishwa na uongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na kwamba hiyo ni moja ya jitihada zinazofanywa na serikali zetu katika kuimarisha ushirikiano.

Pia, akaeleza kuwa Sweden itaungana na nchi nyingine za Nordic kuadhimisha wiki ya Nordic itakayofanyika tarehe 29 Mei 2023 hadi tarehe 1 Juni 2023 katika maadhimisho yanayotarajiwa kuwakutanisha Mabalozi wanaowakilisha nchi za Nordic nchini, nchi marafiki wa Nordic na viongozi mbalimbali wa Serikali ya Tanzania.

Pamoja na ushirikiano uliopo kati ya Sweden na Tanzania katika miradi ya maendeleo, kampuni za kutoka nchini Sweden zimewekeza nchini katika sekta mbalimbali ambazo ni pamoja na kampuni ya Ericsson, Tigo, Scania na kampuni za uchimbaji wa madini.

Katika hatua nyingine, Dkt. Tax amekutana na Mwakilishi Mkazi wa Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu (ICRC) Bw. Bart Vermeiren aliyefika ofisini kwake kujitambulisha. 

Katika mazungumzo yao Dkt. Tax amemuhakikishia Bw. Vermeiren kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana na ICRC katika kuhakikisha kuwa Tanzania wanakuwa na uelewa wa pamoja kuhusu kuanzishwa kwa kamati ya kitaifa ya ICRC.

“Karibu sana Tanzania, nikuhakikishie kuwa Tanzania itaendelea kufanya kazi na ICRC Tanzania, ili wadau wapate uelewa wa pamoja na hivyo kurahisisha kuanzishwa kwa kamati ya Kitaifa,” alisema Dkt. Tax.

Naye Bw. Bart Vermeiren amemhakikishia Mhe. Wazirii kuwa ICRC Tanzania itaendelea kufanya kazi na Tanzania na kumuahidi kuwa Kamati hiyo iko tayari kushirikiana na Tanzania ili kufanikisha azma ya Tanzania kuanzisha kamati ya kitaifa katika eneo la kujenga uwezo katika Sheria za Kimatifa za msaada wa kibinadamu.

Ameipongeza Tanzania kwa kuendelea kuwa nchi ya amani katika ukanda wake. Pia amewapongeza wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma kwa kushinda mashindano ya Sheria za Kimataifa za Msaada wa Kibinadamu kwa bara la Afrika.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb) akisalimiana na Mwakilishi Mkazi wa Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu Duniani (ICRC) Bw. Bart Vermeiren walipokutana kwa mazungumzo jijini Dodoma
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb) akisalimiana na Balozi wa Ufalme wa Sweden nchini Mhe. Charlotta Ozaki Macias walipokutana kwa mazungumzo jijini Dodoma.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax akiwa katika mazungumzo na Mwakilishi Mkazi wa Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu Duniani (ICRC) Bw. Bart Vermeiren yaliyofanyika jijini Dodoma
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax akielezea jambo wakati wa mazungumzo na Balozi wa Ufalme wa Sweden nchini Mhe. Charlotta Ozaki Macias yaliyofanyika jijini Dodoma
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax na Mwakilishi Mkazi wa Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu Duniani (ICRC) Bw. Bart Vermeiren wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watendaji wa Wizara na ICRC.
Mazungumzo baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax na Balozi wa Ufalme wa Sweden nchini Mhe. Charlotta Ozaki Macias yakiendelea. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax na Balozi wa Ufalme wa Sweden nchini Mhe. Charlotta Ozaki Macias wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watendaji wa Wizara na Ubalozi. 

NORWAY YAIHAKIKISHIA TANZANIA USHIRIKIANO KATIKA SEKTA YA KILIMO

Serikali ya Norway imeihakikishia Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ushirikiano katika sekta za kilimo, usalama wa chakula, nishati, biashara na uwekezaji na mabadiliko ya tabianchi.

Ahadi hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Norway anayeshughulikia Maendeleo ya Kimataifa Mhe. Bjørg Sandkjær alipokutana kwa mazungumzo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

Balozi Mbarouk alisema kuwa Norway imekuwa mdau mkubwa wa Tanzania katika sekta ya afya na imekuwa ikisaidia katika masuala mbalimbali katika sekta hiyo.

“Katika hii ziara Mhe. Naibu Waziri anatagemea kufanya ziara ya kutembelea hospitali ya Kiluteri ya Hydom ambayo imekuwa ikifadhiliwa na Serikali ya Norway……… madhumuni ya zaira hiyo ni kuangalia ni kwa namna gani Norway inaweza kuongeza ushirikiano na kuisaidia hospitali hiyo,” alisema Balozi Mbarouk.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Norway anayeshughulikia Maendeleo ya Kimataifa Mhe. Bjørg Sandkjær amesema kuwa ameitembela Tanzania kutokana na ushirikiano imara uliopo baina yake na Serikali ya Norway uliodumu kwa muda mrefu na ulianza kama ushirikiano wa maendeleo. 

“Lengo la ziara yangu hapa Tanzania ni kuangalia ushirikiano katika sekta ya afya kwa sababu Norway imekuwa ikifadhili sekta, Mashirika ya Umoja wa Mataifa, mifuko ya kimataifa, wadau wengine wanaohusika katika sekta ya afya pamoja na asasi za kiraia zinazofanya kazi na Serikali ya Tanzania katika kuboresha huduma za afya,” alisema Mhe. Sandkjær. 

Hivyo nitaitembelea Hospitali ya Kilutheri ya Haydom ili kujionea shughuli zinavyofanyika na kuangalia zaidi maeneo ya ushirikiano katika sekta hiyo.

Tanzania na Norway zimekuwa zikishirikiana katika sekta za afya, elimu, uvuvi, nishati jadidifu, kilimo, ushafirishaji na utalii pamoja na masuala ya bahari. 

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akimsikiliza Naibu Waziri wa Norway anayeshughulikia Maendeleo ya Kimataifa Mhe. Bjørg Sandkjær walipokutana kwa mazungumzo na katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Balozi wa Norway nchini, Mhe. Elisabeth Jacobsen (kushoto) akieleza jambo wakati wa kikao cha Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk na Naibu Waziri wa Norway anayeshughulikia Maendeleo ya Kimataifa Mhe. Bjørg Sandkjær katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Kikao cha Balozi wa Norway nchini, Mhe. Elisabeth Jacobsen akieleza jambo wakati wa kikao cha Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk na Naibu Waziri wa Norway anayeshughulikia Maendeleo ya Kimataifa Mhe. Bjørg Sandkjær kikiendelea katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Kikao cha Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk na Naibu Waziri wa Norway anayeshughulikia Maendeleo ya Kimataifa Mhe. Bjørg Sandkjær kikiendelea katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk, Naibu Waziri wa Norway anayeshughulikia Maendeleo ya Kimataifa Mhe. Bjørg Sandkjær katika picha ya pamoja na Balozi wa Norway nchini, Mhe. Elisabeth Jacobsen 



Wednesday, March 22, 2023

DKT. TAX AKUTANA NA BALOZI WA MAREKANI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) amekutana na kuzungumza na Balozi wa Marekani nchini, Mhe. Michael Battle katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

Pamoja na mambo mengine, viongozi hao wamejadili kuhusu maandalizi ya ziara ya Makamu wa Rais wa Marekani nchini, Mhe. Kamala Harris, masuala ya ushirikiano kati ya Tanzania na Marekani na jinsi ya kufanya kazi kwa pamoja katika kuendeleza uhusiano wa kidiplomasia uliopo baina ya mataifa hayo mawili.

Dkt. Tax ameishukuru Serikali ya Marekani kwa kushirikiano na Serikali ya Tanzania wakati wote tangu kuanzishwa kwa uhusiano wa kidiplomasia kati ya mataifa hayo na umekuwa na maslahi mapana kwa wananchi wa pande zote mbili.

Naye Balozi wa Marekani Nchini, Mhe. Battle ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa kuendelea kudumisha uhusiano wake na Serikali ya Marekani.

Katika tukio jingine, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb.) amekutana kwa mazungumzo na Balozi wa Urusi nchini Mhe. Mhe. Andrey Avetisyan katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Balozi Mbarouk ameipongeza Urusi kwa fursa za masomo zinazotolewa na nchi hiyo kwa watanzania na kuomba fursa zaidi za ushirikiano katika sekta za kilimo, madini, afya na uhandisi.

Naye Balozi wa Urusi Mhe. Andrey Avetisyan amesema Serikali ya Urusi inategemea kuongeza idadi ya ufadhili wa nafasi za masomo kutoka idadi ya nafasi 90 hadi 120 ili kutoa nafadi zaidi kwa watanzania kunufaika na fursa za elimu zinazopatikana nchini Urusi.

Urusi imekuwa ikishirikiana na Tanzania katika nyanja mbalimbali hususan sekta za elimu, afya, utalii na utamaduni, mafuta na gesi, ulinzi na usalama, madini, kilimo na uhandisi.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akisalimiana na Balozi wa Marekani nchini, Mhe. Michael Battle katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akizungumza na Balozi wa Marekani nchini, Mhe. Michael Battle katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga (kushoto) pamoja na Maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje wakifuatilia majadiliano ya Mhe. Waziri Dkt. Tax na Balozi wa Marekani nchini 

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akimkaribisha Balozi wa Urusi nchini Mhe.  Andrey Avetisyan katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Balozi wa Urusi nchini, Mhe. Andrey Avetisyan akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akimueleza jambo Balozi wa Urusi nchini, Mhe. Andrey Avetisyan katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam



Monday, March 20, 2023

TANZANIA YAKABIDHI RASMI MSAADA NCHINI MALAWI



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Malawi, Mhe. Nancy Tembo mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kamuzu Jijini Lilongwe. Dkt. Tax alikuwa nchini Malawi kukabidhi msaada wa kibinadamu kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kufuatia kimbunga Freddy kilichoikumba Nchi hiyo tarehe 13 Machi 2023.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akimsikiliza Balozi wa Tanzania Nchini Malawi, Mhe. Humphrey Polepole wakati wa hafla fupi ya kukabidhi msaada wa kibinadamu kwa Serikali ya Malawi iliyofanyika Ikulu Jijini Lilongwe, Malawi leo tarehe 20 Machi 2023

Rais wa Malawi Mhe. Dkt. Lazarus Chakwera akipokea ujumbe maalum kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax. Dkt. Tax alikuwa nchini Malawi kukabidhi msaada wa kibinadamu kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan

Rais wa Malawi Mhe. Dkt. Lazarus Chakwera akiagana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax baada ya kuwasilisha msaada wa kibinadamu kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa Serikali ya Malawi

Rais wa Malawi Mhe. Dkt. Lazarus Chakwera katika picha ya pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax na Waziri wa Mambo ya Nje wa Malawi, Mhe. Nancy Tembo pamoja na viongozi waandamizi wa Serikali ya Malawina na ujumbe wa Tanzania


 


NCHI ZA SADC ZAWEKA MIKAKATI YA KUJIKWAMUA KIUCHUMI




Waziri wa Mtangamano wa Kikanda wa DRC na Mwenyekiti wa Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC, Mhe. Didier Mazenga Mukanzu akisoma hotuba yake wakati wa Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (kushoto) pamoja na Mawaziri wenzake wakiwa wamesimama kwa ajili ya kuimba nyimbo za Taifa wakati wa hafla ya ufunguzi ya Mkutano wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC)
Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Anthony Mavunde akichangia jambo wakati wa Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC

Waheshimiwa Mawaziri na wajumbe wengine wa Mkutano wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) wakifuatilia hotuba wakati wa ufunguzi wa mkutano huo.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akitenda jambo na Msaidizi wake, Bw. Seif Kamtunda.

Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya je na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga akifuatilia hotuba za viongozi wakati wa Mkutano wa Baraza la Mawaziri
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akitenda jambo na Kaimu Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushurikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Talha Waziri.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akimsikiliza Waziri wa Zambia wakati waliposhiriki hafla ya ufunguzi ya Mkutano wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC)


Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Anthony Mavunde akiongea na mmoja wa Mawaziri walioshiriki Mkutano wa Baraza la Mawaziri
Kikundi cha Utamaduni kikiwaburudisha wageni wakati wa hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC)
uliofanyika Kinshasa, DRC

Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Anthony Mavunde akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wa Tanzaia ulioshiriki Mkutano wa Baraza la Mawaziri

Waheshimiwa Mawaziri wakiwa katika picha ya pamoja nje ya Ukumbi uliofanyika Mkutano wa Baraza la Mawaziri