Monday, March 20, 2023

TANZANIA YAKABIDHI RASMI MSAADA NCHINI MALAWI



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Malawi, Mhe. Nancy Tembo mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kamuzu Jijini Lilongwe. Dkt. Tax alikuwa nchini Malawi kukabidhi msaada wa kibinadamu kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kufuatia kimbunga Freddy kilichoikumba Nchi hiyo tarehe 13 Machi 2023.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akimsikiliza Balozi wa Tanzania Nchini Malawi, Mhe. Humphrey Polepole wakati wa hafla fupi ya kukabidhi msaada wa kibinadamu kwa Serikali ya Malawi iliyofanyika Ikulu Jijini Lilongwe, Malawi leo tarehe 20 Machi 2023

Rais wa Malawi Mhe. Dkt. Lazarus Chakwera akipokea ujumbe maalum kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax. Dkt. Tax alikuwa nchini Malawi kukabidhi msaada wa kibinadamu kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan

Rais wa Malawi Mhe. Dkt. Lazarus Chakwera akiagana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax baada ya kuwasilisha msaada wa kibinadamu kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa Serikali ya Malawi

Rais wa Malawi Mhe. Dkt. Lazarus Chakwera katika picha ya pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax na Waziri wa Mambo ya Nje wa Malawi, Mhe. Nancy Tembo pamoja na viongozi waandamizi wa Serikali ya Malawina na ujumbe wa Tanzania


 


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.