Tuesday, March 7, 2023

DKT. TAX AKUTANA KWA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA UINGEREZA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb) amekutana kwa mazungumzo na Balozi wa Uingereza nchini, Mhe. David Concar katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

Pamoja na mambo mengine, viongozi hao wamejadili namna ya kuboresha uhusiano baina ya  Tanzania na Uingereza na jinsi ya kufanya kazi kwa pamoja katika kudumisha na kuendeleza uhusiano huo.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb) akizungumza na Balozi wa Uingereza nchini Mhe. David Concar katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Balozi wa Uingereza nchini Mhe. David Concar akifafanua jambo kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax) walipokutana kwa mazungumzo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax katika picha ya pamoja na Balozi wa Uingereza nchini Mhe. David Concar katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam






No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.