Wednesday, March 8, 2023

TANZANIA, NAMIBIA KUIMARISHA DIPLOMASIA YA UCHUMI




Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Kiongozi wa ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa Tatu wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano (JCC) kati ya Tanzania na Namibia, ngazi ya Maafisa Waandamizi, Balozi Fatma Rajab (kushoto) akihutubia wakati wa hafla ya ufunguzi wa mkutano huo unaofanyika jijini Windhoek, Namibia tarehe 8 hadi 10 Machi 2023.  Kulia, ni Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje wa Namibia, Balozi Penda Naanda.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab (wa pili kutoka kushoto walioketi), Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje wa Namibia, Balozi Penda Naanda (watatu kutoka kushoto walioketi), Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Namibia, Mhe. Dkt. Modestus Kipilimba (wa kwanza koshoto walioketi), Balozi wa Jamhuri ya Namibia nchini Tanzania, Mhe. Lebius Tobius katika picha ya pamoja na Makatibu Wakuu na Maafisa Waandamizi wa Serikali ya Tanzania na Namibia wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Tatu wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano (JCC) kati ya Tanzania na Namibia ngazi ya Maafisa Waandamizi unaofanyika jijini Windhoek, Namibia. 

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Namibia, Mhe. Dkt. Modestus Kipilimba akifatilia hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Tatu wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano (JCC) kati ya Tanzania na Namibia, ngazi ya Maafisa Waandamizi unaofanyika jijini Windhoek, Namibia tarehe 8 hadi 10 Machi 2023

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab (kulia) akihutubua wakati wa hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Tatu wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano (JCC) kati ya Tanzania na Namibia, ngazi ya Maafisa Waandamizi unaofanyika jijini Windhoek, Namibia tarehe 8 hadi 10 Machi 2023, kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Naimi Aziz.

Ujumbe Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Mkutano wa Tatu wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano (JCC) kati ya Tanzania na Namibia ngazi ya Maafisa Waandamizi ukifuatilia hafla ya ufunguzi wa mkutano huo unaofanyika jijini Windhoek, Namibia tarehe 8 hadi 10 Machi 2023

Sehemu nyingine ya ujumbe wa Tanzania ikifuatilia mkutano huo

Sehemu nyingine ya ujumbe wa Tanzania ikifuatilia mkutano huo

Ujumbe wa Jamhuri ya Namibia katika Mkutano wa Tatu wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano (JCC) kati ya Tanzania na Namibia ngazi ya Maafisa Waandamizi wakifatilia hafla ya ufunguzi wa mkutano huo unaofanyika jijini Windhoek, Namibia tarehe 8 hadi 10 Machi 2023

 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.