Saturday, November 5, 2011

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bw. John Haule akiwa kwenye mazungumzo leo na Maafisa wa Mambo ya Nje wa Wizara waliohitimu mafunzo ya wiki tatu ya diplomasia.

Baadhi ya Kaimu Wakurugunzi wa Wizara wakisikiliza hoja za Maafisa wa Mambo ya Nje wa Wizara walipofanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Wizara leo tarehe 5.11.2011

Katibu Mkuu wa Wizara Bw. John Haule akiandika baadhi ya hoja za Maafisa Mambo ya Nje wa Wizara alipokutana nao leo wizarani baada ya kuhitimu mafunzo ya diplomasia.


Kaimu Mkurugenzi Idara ya Asia na Australasia Bw. Rogatus Shao akifuatilia mazungumzo ya Katibu Mkuu kwenye mkutano huo. Kulia ni msaidizi wake kwenye idara hiyo Bi. Naimi Aziz 
Bw. Robert Kahendaguza, Afisa Mambo ya Nje Ubalozi wa Tanzania Pretoria Afrika Kusini, akizungumza kwa niaba ya Maafisa wengine changamoto na mafanikio ya maafisa hao baada ya mafunzo yao.  

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.