Monday, August 14, 2017

Waziri Mahiga akutana na Mjumbe Maalum kutoka Serikali ya Japan

Waziri wa Mambo wa Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Mjumbe Maalum wa Serikali ya Japan, Mhe. Ichiro Aisawa alipofika Wizarani hivi karibuni. Katika mazungumzo yao walizungumzia masuala mbalimbali yanayohusu ushirikiano kati ya nchi hizi mbili ikiwemo miradi ya maendeleo inayofadhiliwa na Japan.
Bw. Ichiro Aisawa nae akizungumza. Kushoto ni Balozi wa Japan nchini, Mhe. Masaharu Yoshida
Mhe. Mahiga akifafanua jambo wakati wa mazungumzo. Kulia ni Bi. Justa Nyange, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Waziri Mahiga akiagana na Bw. Ichiro Aisawa mara baada ya kumaliza mazungumzo yao.



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.