Thursday, June 15, 2017

PUBLIC ANNOUNCEMENT


PUBLIC ANNOUNCEMENT

The Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation of the United Republic of Tanzania wishes to inform the General Public in need of Certificationof Documents to be used outside the country, that;

(1)From 1stJuly, 2017 all payments for Certification of Documents shall be made via CRDB bank account number0150275408200, Foreign Collection Account and the bank slip be submitted to the Ministry.

(2)It is stressed that, no cash payment will be accepted at the Ministry as per the previous practice except bank payment slip. Cost for certification remains unchanged,Tanzania Shillings Fifteen Thousands only (Tshs.15, 000/=) per copy.

(3)Before any document is brought to the Ministry for certification, it has to be first verified by the issuing authority for authentication.

(4)After complying with the directive provided under clause three (3) herein above, the applicant must write a letter to the Permanent Secretary, Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation requesting for certification of the documents. The said letter must be accompanied with copies of all the documents to be certified after being firstly verified by the issuing authority.

(5) IT IS REMINDED THAT, DOCUMENTS CERTIFICATION SERVICE IS AVAILABLE ONLY ON TUESDAY AND THURSDAY FROM 0900HRS TO 1100HRS.

ISSUED BY MINISTRY OF FOREIGN AFFAIRS

 AND EAST AFRICAN COOPERATION


Wednesday, June 14, 2017

Balozi Pindi Chana awasilisha Hati za Utambulisho

Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Mhe. Dkt. Pindi Hazara Chana akisalimiana na Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mhe. Uhuru Kenyatta kabla ya kuwasilisha Hati za Utambulisho kwenye Ikulu ya Eldoret tarehe 13 Juni 2017.

Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Mhe. Dkt. Pindi Hazara Chana wa pili kutoka kushoto akiwa katika picha ya pamoja na Rais wa Kenya (katikati) mara baada ya zoezi la kuwasilisha Hati za Utambulisho kukamilika.




Friday, June 9, 2017

Wizara ya Mambo ya Nje yafanya uzinduzi wa shindano la kubuni nembo mpya ya EAC

Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi akizungumza katika halfa ya uzinduzi wa shindano ya kubuni nembo mpya ya Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na Taasisi zake kwa vijana wenye umri kati ya miaka 18 hadi 35 wa Jumuiya hiyo, uliofanyika katika Ukumbi wa Nkurumah, chuo kikuu cha Dar es Salaam tarehe 09 Juni, 2017. Pembeni ni Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo cha Dar es Salaam, Profesa Curthbert Kimambo.

Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakifuatilia maelekezo ya vigezo vya shindano pamoja na zawadi zitakazotolewa kwa mshindi wa kwanza ambaye atapata dola za Kimarekani 25,000, wa pili dola  5,000 na wa tatu dola 2,500.

Sehemu nyingine ya Wanafunzi wakifuatilia maelekezo.

Picha ya pamoja uongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje, Chuo kikuu cha Dar es Salaam na Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Picha ya pamoja Viongozi na wanafunzi.

Siku ya Kongamano la Biashara ya Kilimo na Uwekezaji kati ya Tanzania na Uholanzi yafana



 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Siku ya Kongamano la Biashara ya Kilimo na Uwekezaji kati ya Tanzania na Uholanzi yafana

Katika kutekeleza Sera ya Diplomasia ya Uchumi, Ubalozi wa Tanzania kwa kushirikiana na Ubalozi wa Uholanzi uliopo Tanzania, Wizara ya Masuala ya Uchumi na Wizara ya Mambo ya Nje za Uholanzi na Taasisi ya Netherlands–African Business Council (NABC)kwa pamoja ziliandaa Kongamano la Biashara na Uwekezaji lililofanyika hapa The Hague, Uholanzi tarehe 31 Mei 2017. Lengo kuu la Kongamamo hilo, pamoja na kuendeleza na kukuza uhusiano mzuri uliopo kati ya Tanzania na Uholanzi, nikutangaza fursa mbalimbali za biashara na uwekezaji zilizopo nchini Tanzania hususan katika Sekta za Kilimo, Ufugaji, Uvuvi na Miundombinu ya Kilimo. Aidha, Kongamano hilo lililohudhuriwa na Wawakilishi wa Makampuni takriban mia moja (100) ni mwendelezo wa utekelezaji wa makubaliano yaliyofikiwa kwenye Mkataba kati ya Tanzania na Uholanzi kuhusu Uingizwaji wa Mbegu za Viazi kutoka Uholanzi uliosainiwa kwenye ziara ya Mhe. Martijn Van Dam, Waziri wa Kilimo wa Uholanzi nchini Tanzania tarehe 16 Juni 2016. Aidha, Kongamano hii lilitanguliwa na ziara ya ujumbe kutembelea maeneo mbalimbali ikiwemo mashamba yanayomilikiwa na wakulima na wafugaji binafsi nchini Tanzania pamoja na kupata fursa za kusikiliza mada mbalimbali zilizotolewa na wakulima/wafugaji na wakufunzi wa Chuo Kikuu cha Wageningen kinachohusika na kufanya tafiti za Kilimo na Ufugaji.
Ujumbe kutoka Tanzania uliongozwa na Mhe.Eng. Mathew Mtigumwe, Katibu Mkuu anayeshughulikia Kilimo kutoka Wizara ya Kilimo, Ufugaji na Uvuvi, akimwakilisha Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi.
Wajumbe wengine ni:
ü  Mhe. Yohana Budeba, Katibu Mkuu anayeshughulikia Uvuvi, Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi,
ü  Mhe. Irene F.M. Kasyanju, Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi,
ü  Bw. Twahir Nzallawahe, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Mazao, Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi,
ü  Bibi Anuciata Njombe, Mkurugenzi wa Uzalishaji wa Mifugo na Masoko, Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi,
ü  Bw. Geoffrey Kirenga, Mtendaji Mkuu wa Kituo cha kuendeleleza Kilimo Ukanda wa Kusini (SAGCOT),
ü  Bibi Jennifer Baarn, Naibu Mtendaji Mkuuwa Kituo cha kuendeleleza Kilimo Ukanda wa Kusini (SAGCOT),
ü  Professa Andrew Temu, Mkurugenzi wa Diligent Consulting Ltd na Mwanachama wa Bodi ya SAGCOT,
ü  Bibi Jacqueline Mkindi, Mtendaji Mkuu wa Tanzania Horticulture Association (TAHA),
ü  Bw. Hussein Sufiani Ally, Mkurugenzi wa AZAM Bakhresa Group,
ü  Bibi Mona Mahecha, Afisa Mambo ya Nje Mwandamizi, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
ü  Maafisa wa Ubalozi wa Tanzania Uholanzi Bw. Matiku Kimenya (MC), Bibi Naomi Z. Mpemba (CO) na Bibi Agnes K. Tengia (FS).
Kwa upande wa Serikali ya Uholanzi, ujumbe uliongozwa na Mhe. Bibi Marjolijn Sonnema, Katibu Mkuu anayeshughulikia masuala ya Kilimo, Wizara ya Masuala ya Uchumi ya Uholanzi ambaye pia anakaimu kama Naibu Waziri wa Kilimo. Wengine ni;
ü  Mhe. Jaap Fredericks, Balozi wa Uholanzi nchini Tanzania,
ü  Bw. Bert Rikken, Afisa anayeshughulikia Masuala ya Kilimo, Ubalozi wa Uholanzi nchini Tanzania/Kenya,
ü  Bibi Ingrid Korving, Afisa Sera Mwandamizi, Wizara ya Masuala ya Uchumi ya Uholanzi,
ü  Bibi Hennie Wellen, Mratibu Wageni wa Kimataifa, Wizara ya Masuala ya Uchumi ya Uholanzi,
ü  Bibi Theresia Mcha, Afisa Kilimo, Ubalozi wa Uholanzi nchini Tanzania.
Katika Kongamano hili, Viongozi wa Ujumbe wa Serikali ya Tanzania na Uholanzi walionesha dhamira ya kuendelea kushirikiana kwa pamoja kwa kusaini Barua (Letter of Intent) ya kuanzishwa kwa Kituo cha Kuendeleza Zao la Viazi nchini Tanzania (Centre for Development of the Potato Industry in Tanzania- CD PIT). Aidha, Makampuni takriban kumi (10) yanayojishughulisha na kilimo cha viazi, yalionesha utayari wa kuwa wanachama kwa kushirikiana na Serikali za nchi hizi mbili katika uanzishwaji wa Kituo hicho. Tukio hilo lilikamilishwa kwa Wawakilishi wa Makampuni hayo kuweka saini kwenye Kadi/Bango kuonesha utayari wao.
Kituo cha CD PIT kinatarajiwa kuanzishwa Mkoani Mbeya ambapo pamoja na kukuza maendeleo ya sekta binafsi na kutoa ajira, kitatoa mafunzo ya kujenga uwezo hususan katika uzalishaji na utafutaji masoko, kitaendesha tafiti mbalimbali za kilimo ikiwemo pia kukuza uhusiano wa kibiashara kati ya  Tanzania na Uholanzi. 
Ubalozi kwa upande wake umeridhishwa na mwitikio mkubwa uliooneshwa na wadau mbalimbali waliojitokeza kushiriki katika Kongamano hilo. Hii inadhihirisha kuzidi kuimarika kwa mahusiano mazuri yaliyopo kati ya nchi hizi mbili.
Pamoja na kubadilishana uzoefu, kujifunza na kufahamiana, Kongamano hilo liliwezesha wadau kupata fursa ya kujadili pia changamoto wanazokabiliana nazo katika shughuli mbalimbali za biashara na uwekezaji wanazoziendesha nchini Tanzania.
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
The Hague, Uholanzi, 09 Juni 2017
Mhe. Mathew Mtigumwe, Katibu Mkuu wa Wizara Kilimo, Mifugo na Uvuvi akisoma hotuba.
Mhe. Irene Kasyanju, Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi akisoma hotuba ya ufunguzi.

Mhe. Marjolijn Sonnema, Katibu Mkuu na Kaimu Naibu Waziri wa Kilimo wa Uholanzi  akisoma hotuba
Picha ya Pamoja ya Waheshimiwa Mabalozi wa Tanzania na Uhoalnzi na Makatibu Wakuu wa Kilimo na Uvuvi na Mkurugenzi wa TAHA.

Uwekaji saini wa makubaliano (letter of intent) ya kuanzishwa kwa kituo cha kuendeleza zao la viazi Tanzania


Thursday, June 8, 2017

Vijana wahamisishwa kushiriki mashindano ya kubuni nembo ya EAC

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika MasharikI, Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi akimsikiliza Afisa  Mkuu wa Uhusiano wa Sekrearieti ya Jumuiya ya Afrika Mshariki, Bw. Otrhieno Richard Owora (kushoto). Katika mazungumzo hayo, wawili hao walizungumzia maandalizi ya uzinduzi wa mashindano ya kubuni nembo mpya ya EAC yatakayowahusisha wanafunzi wa Vyuo Vikuu vilivyopo kwenye nchi wanachama wa Jumuiya hiyo. Uzinduzi huo utafanyika kwenye Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam tarehe 09 Juni 2017. 
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mindi Kasiga (wa kwanza kushoto), pamoja na Maafisa Habari wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, wa kwanza kulia ni Bw. Ally Kondo pamoja na Robi Bwiru wakinukuu mambo yaliyokuwa yakizungumzwa na Balozi Mwinyi pamoja na Bw. Owora.
Mazungumzo yakiendelea.
Balozi Mwinyi akipokea kitabu chenye mwongozo wa namna ya kushiriki mashindano hayo.
Picha ya pamoja.

Wednesday, June 7, 2017

Tanzania yashiriki Mkutano wa kujadili matumizi ya Bahari na rasilimali zake

Ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano wa utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu Na. 14 (Sustainable Development Goals-SDGs14)  maarufu kama Oceans Conference unaojadili matumizi endelevu ya bahari na rasilimali zilizomo baharini.

Waziri wa Kilimo, Nifugo na Uvuvi, Mhe. Charles Tzeba akiwasilisha hotuba kwa niaba ya Serikali ya Tanzania kwenye Mkutano wa Kimataifa wa kuweka mikakati ya utekelezaji wa SDG14 unaoendelea Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa New York, Marekan. Mkutano huo ni maalum kwa ajili ya kujadili kuhusu matumizi endelevu ya bahari na rasilimali zilizomo baharini kama sehemu ya utekelezaji wa lengo la 14 la malengo ya maendeleo endelevu






Monday, June 5, 2017

Wizara ya Mambo ya Nje yafanya usafi kwenye ufukwe wa Feri



Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki waadhimisha siku ya mazingira duniani kwa kufanya usafi kwenye ufukwe wa Bahari ya Hindi eneo la Feri jijini Dar es Salaam.  Wanaoenekana wakifanya usafi wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango, Bw. James Lugaganya akiwa pamoja na wafanya kazi wengine wa Wizara.
Mkurugenzi msaidizi Idara ya Utawala na Rasilimali watu Bw. Hamid Mbegu (kushoto) naye akifanya usafi
Sehemu nyingine ya watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakijumuika kwa pamoja katika kufanya usafi kwenye ufukwe wa bahari eneo la Feri.
wakisomba taka
Sehemu nyingine ya watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiendelea kufanya usafi
Usafi ukiendelea

Kaimu Mkurugenzi wa idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Jestas Nyamanga  akizungumza na waandishi wa Habari mara baada ya kumaliza zoezi la kufanya usafi kwenye ufukwe eneo la ferri



HOTUBA YA BALOZI DKT. AZIZ P. MLIMA, KATIBU MKUU WA WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI KATIKA SHUGHULI YA KUFANYA USAFI KWENYE UFUKWE WA BAHARI YA HINDI, ENEO LA KIVUKONI (FERRY), DAR ES SALAAM
TAREHE 05 JUNI 2017

Waheshimiwa Mabalozi, Wakurugenzi na Makaimu Wakurugenzi kutoka Wizarani,
Wawakilishi wa Mashirika na Taasisi za Umoja wa Mataifa kwenye tukio hili;
Uongozi wa Kata ya Kivukoni ukiongozwa na Mhe. Henry Massaba, Diwani wa Kata ya Kivukoni;
Uongozi wa Mtaa wa Kivukoni ukiongozwa na Ndugu Gasper Makame, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kivukoni;
Wafanyakazi wa Wizara na Taasisi zilizo chini ya Wizara;
Wananchi wote mlioshiriki;
Waandishi wa Habari;
Mabibi na Mabwana.

Awali ya yote, napenda kuwasilisha salamu kutoka kwa Mhe. Waziri, Dkt. Augustine P. Mahiga (Mb.), pamoja na Mhe. Naibu Waziri, Dkt. Susan A. Kolimba (Mb.). Wanawasalimu sana na walitamani wajumuike nasi kwenye zoezi hili, ila kutokana na kubanwa na majukumu mengine ya kitaifa wameshindwa. Lakini wamefurahishwa na hiki tulichokifanya na wanatupongeza sana.

Wizara inawashukuru sana wote mliojumuika nasi kwenye tukio hili muhimu la kusafisha mazingira ya ufukwe huu tunapoadhimisha Siku ya Mazingira Duniani.
Maadhimisho haya kidunia yanafanyika nchini Canada, na kwa hapa Tanzania, yanafanyika kitaifa huko Butiama, Mkoani Mara, chini ya kaulimbiu: “Hifadhi ya Mazingira: Muhimili kwa Tanzania ya Viwanda”.
Kaulimbiu hii inatukumbusha kuwa tunapoelekea kwenye Tanzania ya Viwanda na Uchumi wa Kati, hatuna budi kutunza mazingira, kwani rasilimali tunazozihitaji kutimiza azma yetu hii adhimu zinapatikana kwenye mazingira na mazingira ndiyo maisha yetu. Hivyo utajiri wetu wa kwanza ni mazingira.

Mabibi na Mabwana,
Tumechagua kufanya zoezi hili la usafi kwenye ufukwe wa bahari kwa sababu tunapozungumzia utunzaji wa mazingira, suala la utunzaji wa bahari linasahaulika. Hivyo, sisi tunaikumbusha jamii kuwa bahari nayo ni sehemu ya mazingira, ni urithi wetu, ni lazima tuitunze.

Kwa bahati, wakati sisi tunafanya zoezi hili, leo hii pia kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, huko New York, dunia inakutana kujadili namna ya kuhakikisha uhifadhi wa bahari na matumizi endelevu ya rasilimali zake, ukiwa ni Mkutano wa kwanza wa Umoja wa Mataifa kuhusu suala hili.
Hivyo, ndugu wananchi wenzangu, naomba tuone umuhimu wa kutunza bahari, tunaitegemea sana kwenye uchumi wetu na maisha yetu ya kila siku, tuache kuichafua kwani ikipoteza uhai ni hasara kwetu sote.

Mabibi na Mabwana,
Mtakubaliana nami kuwa, bila kufanya zoezi hili kwa ushirikiano, tusingefanya chochote cha msingi hapa. Basi, na hili liwe funzo wakati huu tunapotekeleza Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) na Makubaliano ya Paris ambayo yote yanasisisiza uhifadhi wa mazingira. Bila ushirikiano, itakuwa vigumu kutimiza azma hiyo ya Makuibaliano ya Paris na Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs). Dunia ni yetu sote, inatutunza sote, inatukirimia sote sawa sawa, basi sote tuna jukumu la kuitunza, tena kwa ushirikiano.

Mabibi na Mabwana, Wananchi Wote Mliopo Hapa,
Kabla sijamaliza kuzungumza, napenda kutumia nafasi hii kuishukuru Ofisi ya Umoja wa Mataifa hapa nchini; Uongozi wa Manispaa ya Ilala na Kata ya Kivukoni kwa misaada yao ya hali na mali katika kufanikisha zoezi hili. Tunawashukuru sana.

Asanteni sana kwa kunisikiliza!