Thursday, August 15, 2024

NAIBU WAZIRI CHUMI AFUNGUA KONGAMANO LA KISWAHILI

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Cosato Chumi akisisitiza jambo alipokuwa akifungua Kongamano la Kimataifa la Kiswahili lililoandaliwa na Chama cha Kiswahili Afrika Mashariki (CHAKAMA) linalofanyika katika Chuo Kikuu cha Dodoma

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Cosato Chumi (Mb.) amefungua Kongamano la Kimataifa la Kiswahili lililoandaliwa na Chama cha Kiswahili Afrika Mashariki (CHAKAMA) linalofanyika katika Chuo Kikuu cha Dodoma, akimwakilisha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Mahmoud Thabit Kombo. 

Kongamano hilo linaloongozwa na mada kuu isemayo "Lugha ya Kiswahili kwa Maendeleo Barani Afrika" linajumuisha Wataalam, Watafiti na wadau wa Kiswahili kutoka Nchi za Afrika Mashariki na sehemu mbalimbali duniani. 

Akifungua Kongamano hilo Waziri Chumi ameeleza kuwa kiswahili kimekuwa miongoni mwa lugha inayotuunganisha Waafrika hususan waliopo Kusini mwa Jangwa la Sahara, na hasa kutokana na mchango wake wakati wa harakati za kupigania uhuru. 

Akizungumzia nafasi ya Wizara katika kueneza lugha ya Kiswahili ulimwenguni Mhe. Chumi ameeleza Wizara kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa ndani na nje Nchi ilitoa mchango mkubwa katika kukifanya Kiswahili kuwa lugha ya kwanza Afrika kutambuliwa na Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO). 

Vilevile ameongeza kusema kuwa licha ya mchango huo, Wizara ya Mambo ya Nje inaendelea kukipa kipaumbele cha kipekee Kiswahili kupitia Sera Mpya ya Mambo ya Nje inayofanyiwa mapitio, hatua ambayo itachangia kubidhaisha lugha hiyo adhimu duniani hivyo kuongeza matumizi ya Kiswahili nje ya mipaka yetu. 

"Kwa sasa Wizara yetu ipo kwenye hatua za mwisho za mapitio ya Sera ya Mambo ya Nje ya Taifa letu. Kutokana na tathmini tuliyoifanya kwenye mapitio hayo, tumekubaliana kuongeza mawanda ya Diplomasia ya Uchumi kwa kujumuisha maeneo ambayo siyo ya jadi (traditional) ikiwemo masuala ya kubidhaisha Kiswahili" Alieleza Mhe. Chumi.

Aliongeza kusema kuwa Wizara kwa siku za usoni inatarajia kuongeza wigo wa upatikanaji wa fursa kwa waalimu wa Kiswahili na wakalimani sehemu mbalimbali duniani pamoja na uuzaji wa vitabu vya kiswahili.

Kwa upande wake, mratibu wa kongamano hilo Dkt. Zainabu Idd ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa kuendelea kuenzi na kukuza lugha ya Kiswahili ndani na nje ya mipaka ya nchi. 

Aidha, Dkt. Zainabu pamoja na kupongeza jitihada zinazofanywa na Serikali, ametoa wito kwa wadau mbalimbali kuendelea kutoa msukumo wa matumizi ya Kiswahili katika majukwaa na matukio mbalimbali ya kimataifa ikiwemo katika matamasha makubwa ya michezo kama vile AFCON, ili kukiongezea thamani na kuwavutia watu wengi zaidi duniani kutumia lugha hiyo adhimu.

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imefanikisha kuongeza wigo wa matumizi ya Lugha ya Kiswahili hususan katika Jumuiya za Kikanda ambapo tayari Jumuiya za SADC, EAC na AU zinatumia lugha hiyo katika kuendesha vikao mbalimbali. 

Vilevile Wizara inaendelea na mikakati ya kukuza na kubidhaisha Kiswahili ikiwemo kufungua madarasa ya kufundishia Kiswahili katika Balozi za Tanzania zilizopo sehemu mbalimbali duniani. 

CHAKAMA ni chama kinachoundwa na wahadhiri wanaofundisha Kiswahili katika Vyuo Vikuu vya Afrika Mashariki kikilenga kuunganisha wadau wa Kiswahili Kikanda na Kimataifa kupitia nyanja mbalimbali ikiwemo utafiti na kufanya mijadala fikirishi kuhusu lugha ya Kiswahili
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Cosato Chumi akitia saini kwenye kitabu cha wageni muda mfupi kabla ya ufunguzi wa Kongamano la Kimataifa la Kiswahili lililoandaliwa na Chama cha Kiswahili Afrika Mashariki (CHAKAMA) linalofanyika katika Chuo Kikuu cha Dodoma
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Cosato Chumi (Mb.) akisalimiana na Prof. Albino John Tenge Mkuu wa Ndaki ya Insia na Sayansi za Jamii, alipowasili katika Chuo Kikuu cha Dodoma kufungua Kongamano la Kimataifa la Kiswahili lililoandaliwa na Chama cha Kiswahili Afrika Mashariki (CHAKAMA) linalofanyika chuoni hapo.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Cosato Chumi akisisitiza jambo alipokuwa akifungua Kongamano la Kimataifa la Kiswahili lililoandaliwa na Chama cha Kiswahili Afrika Mashariki (CHAKAMA) linalofanyika katika Chuo Kikuu cha Dodoma
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Cosato Chumi (Mb.) akikabidhiwa cheti cha kutambua mchango wa Wizara katika kufanikisha kufanyika kwa Kongamano hilo na kukuza lugha Kiswahili.
Kongamano la Kimataifa la Kiswahili lililoandaliwa na Chama cha Kiswahili Afrika Mashariki likiendelea
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Cosato Chumi akifuatilia  hafla ya ufunguzi wa Kongamano la Kimataifa la Kiswahili lililoandaliwa na Chama cha Kiswahili Afrika Mashariki (CHAKAMA) linalofanyika katika Chuo Kikuu cha Dodom
Kongamano la Kimataifa la Kiswahili lililoandaliwa na Chama cha Kiswahili Afrika Mashariki likiendelea
Mkuu wa Ndaki ya Insia na Sayansi za Jamii Prof. Albino John Tenge akizungumza kwenye ufunguzi Kongamano la Kimataifa la Kiswahili lililoandaliwa CHAKAMA linalofanyika jijini Dodoma
Kongamano la Kimataifa la Kiswahili lililoandaliwa na Chama cha Kiswahili Afrika Mashariki likiendelea

PROF MKENDA AFUNGA MKUTNO WA ELIMU WA EAC JIJINI ARUSHA

 

Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Adolf Mkenda akizungumza wakati wa kufunga Mkutano wa kwanza wa Elimu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Maadhimisho ya mwaka wa elimu wa Umoja Afrika uliofanyika jijini Arusha tarehe 12-15 Agosti, 2024.

Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Adolf Mkenda akizungumza wakati wa kufunga Mkutano wa kwanza wa Elimu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Maadhimisho ya mwaka wa elimu wa Umoja Afrika uliofanyika jijini Arusha tarehe 12-15 Agosti, 2024.

Mwenyekiti wa Baraza la Kisekta na Waziri wa Elimu na Mafunzo wa Sudan Kusini Mhe. Awut Deng Achuil akizungumza wakati wa kufunga Mkutano wa kwanza wa Elimu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Maadhimisho ya mwaka wa elimu wa AU uliofanyika jijini Arusha tarehe 12-15 Agosti,2024.



 

washiriki wakifuatilia ufungaji wa  Mkutano wa kwanza wa Elimu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Maadhimisho ya mwaka wa elimu wa AU uliofanyika jijini Arusha tarehe 12-15 Agosti,2024.


washiriki wakifuatilia ufungaji wa  Mkutano wa kwanza wa Elimu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Maadhimisho ya mwaka wa elimu wa AU uliofanyika jijini Arusha tarehe 12-15 Agosti,2024.


washiriki wakifuatilia ufungaji wa  Mkutano wa kwanza wa Elimu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Maadhimisho ya mwaka wa elimu wa AU uliofanyika jijini Arusha tarehe 12-15 Agosti,2024.


Picha ya pamoja na Meza Kuu wakati wa ufungaji wa  Mkutano wa kwanza wa Elimu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Maadhimisho ya mwaka wa elimu wa AU uliofanyika jijini Arusha tarehe 12-15 Agosti,2024.

Picha ya pamoja na Meza Kuu wakati wa ufungaji wa  Mkutano wa kwanza wa Elimu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Maadhimisho ya mwaka wa elimu wa AU uliofanyika jijini Arusha tarehe 12-15 Agosti,2024.

 

Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Adolf Mkenda amefunga rasmi Mkutano wa kwanza wa Elimu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Maadhimisho ya mwaka wa elimu wa Umoja Afrika uliofanyika jijini Arusha. 

Akizungumza katika hafla hiyo Prof. Mkenda amezitaka nchi wanachama kuandaa mpango kazi utakaoonesha namna bora ya kutekeleza maazimio yaliyotokana na mkutano huo ili kuhakikisha yanafanyiwa kazi kwa ukamilifu.

Pia ametaka kuhakikisha mafanikio yote yaliyopatikana katika maadhimisho ya mwaka wa elimu wa AU yanasherehekewa na kutafakari jinsi ya kuwa na mifumo bora zaidi ya utoaji elimu kwa vijana na hivyo baada ya miaka miwili mkutano ujao uone matunda ya mkutano huo. 

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Kisekta na Waziri wa Elimu na Mafunzo wa Sudan Kusini Mhe. Awut Deng Achuil alıtoa wito wa kuchukua hatua na kujitoa zaidi ili kuhakikisha malengo na maazimio ya mkutano yanatekelezwa kwa vitendo na ameipongeza Tanzania kwa kuwa mwenyeji pamoja na Sekretarieti ya EAC na nchi wanachama kwa kuandaa mkutano huo kwa mafanikio makubwa. 

Mkutano huo wa kwanza na wa aina yake kufanyika katika ukanda wa Afrika Mashariki ulijumuisha wadau mbalimbali wa elimu kutoka Serikalini na sekta binafsi umejadili na kuweka mikakati mipya ya kukabiliana na fursa na changamoto zilizopo katika sekta ya elimu katika Jumuiya ya Afrika Mashariki na Bara la Afrika kwa ujumla. Kufanyika kwa mkutano huo ni utekekezaji wa maamuzi ya Mkutano wa 15 wa Baraza la Kisekta la Jumuiya ya Afrika Mashariki la Elimu, Sayansi na Teknolojia, Utamaduni na Michezo; na Umoja wa Afrika. 

Mkutano huo wa elimu na Maadhimisho uliwakutanisha Mawaziri wa Elimu kutoka Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Wageni mashuhuri wakiwemo Wawakilishi wa Nchi mbalimbali kama Jamhuri ya Watu wa China; Wakuu wa Mashirika na Taasisi za Kikanda na Kimataifa zinazojihusisha na agenda ya kuendeleza sekta ya elimu kama vile Umoja wa Ulaya (EU), Umoja wa Afrika (AU), Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF), Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi (ECOWAS), Taasisi ya Maendeleo ya Elimu Afrika (ADEA), Taasisi ya Haki Elimu, na Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ). 

Mkutano huo pia uliwakutanisha Wadau wa elimu zaidi ya 600 kutoka Nchi Wanachama, Taasisi za elimu, Mashirika yasiyo ya kiserikali, Sekta binafsi, Mashirika ya kimataifa, Asasi za kiraia waliokutana kutathmini, kubadilishana uzoefu wa mbinu bora za uendelezaji wa sekta ya elimu. Mkutano huo uliandaliwa na Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa kushirikiana na Nchi wanachama, taasisi zisizo za kiserikali , wadau wa maendeleo na bhana vya elimu katika Jumuiya ya Afrika Mashariki ulianza tarehe 12 hadi 15 Agosti 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan awasili Zimbabwe

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili Zimbabwe kwa ajilli ya kushiriki Mkutano wa 44 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) utakaofanyika tarehe 17 Agosti, 2024.


WAZIRI KOMBO AFANYA MAZUNGUMZO NA MAWAZIRI WA MAMBO YA NJE WA AFRIKA KUSINI NA MADAGASCAR


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Mahmoud Thabit Kombo (Mb.) amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Afrika Kusini, Mhe. Ronald Lamola na Waziri wa Mambo ya Nje wa Madagascar, Mhe. Dkt. Rasata Rafaravavitafika pembezoni mwa Mkutano wa Mawaziri wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) leo tarehe 14 Agosti, 2024 Harare, Zimbabwe.

 

Akizungumza na Mhe. Lamola, Waziri Kombo ameeleza kuwa Tanzania itaendelea kudumisha ushirikiano wa kihistoria na kindugu uliopo baina ya Tanzania na Afrika kusini ili kukuza sekta za kiuchumi ikiwemo biashara, utalii, uwekezaji, elimu, afya na maeneo mengine ya kimkakati kwa maslahi ya pande zote mbili.

 

Naye Mhe. Lamola ameeleza kuwa Afrika Kusini inaendelea kuthamini mchango wa Tanzania katika harakati za ukombozi wa Taifa hilo hivyo, ina nia ya dhati ya kuuenzi mchango huo kwa kukuza ushirikiano katika shughuli za kiuchumi, kijamii na kisiasa kwa ustawi wa wananchi wa mataifa hayo mawili.

 

 

Aidha, katika mazungumzo ya Mhe. Kombo na Mhe. Dkt. Rafaravavitafika wamejadili juu ya kuendelea kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia na kiuchumi na taifa hilo hususan katika sekta ya uchumi wa blue ambao Tanzania imeuwekea mkazo ili kukuza uchumi kupitia rasilimali za bahari zinazopatikana na kukuza biashara yake kimataifa.

HABARI KATIKA PICHA: Waziri Kombo alipokutana kwa mazungumzo na Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Afrika Kusini, Mhe. Ronald Lamola.







HABARI KATIKA PICHA: Waziri Kombo alipokutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Madagascar, Mhe. Dkt. Rasata Rafaravavitafika










Wednesday, August 14, 2024

WAZIRI KOMBO AFANYA KIKAO NA WATUMISHI WA UBALOZI WA TANZANIA NCHINI ZIMBABWE

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Mahmoud Thabit Kombo (Mb.) amefanya kikao na watumishi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Zimbabwe tarehe 14 Agosti, 2024.

 

Kikao hicho kilichofanyika pembezoni mwa mkutano wa Mawaziri wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kimejadili juu ya utekelezaji wa majukumu ya kidiplomasia yanayoendelea kutekelezwa na watumishi wa ubalozi huo.


“ Serikali ina imani nanyi ndio maana ikawaleta kutekeleza majukumu katika  kituo hiki, hivyo, ni vema mkajituma na kufanya kazi kwa tija ili kuweza kuleta matokeo makubwa kwa maslahi ya Taifa letu” alisema Waziri Kombo.


Pia, ameeleza kuwa Wizara inahitaji kuona Balozi za Tanzania nje zinatekeleza diplomasia ya uchumi kwa vitendo na kuwasilisha taarifa zenye matokeo hususan katika sekta za biashara, uwekezaji, na utalii. 


Aidha, Waziri Kombo ametembelea miradi mbalimbali ya maendeleo yenye umiliki wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Zimbabwe ikiwemo, nyumba za makazi za watumishi wa Ubalozi, nyumba za makazi za kibiashara, jengo la ofisi la ubalozi na kiwanja cha ubalozi huo chenye ukubwa wa ekari  saba (7).


Waziri Kombo amemueleza Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe kuwa ziara yake katika miradi hiyo imekuwa ya mafanikio kwa kuwa amejionea namna Ubalozi unavyojituma katika kutekeleza majukumu yake pamoja na jitihada za kukuza ushirikiano na nchi hiyo rafiki.


Vilevile, miradi hiyo kwa upande mwingine imeuwezesha ubalozi kupata nyumba kwa ajili ya watumishi wake na hivyo kuipunguzia Serikali gharama ya kupangisha nyumba na za uendeshaji kwa ujumla.


Hivyo, Waziri Kombo amesisitiza kuwa miongoni mwa masuala ambayo atayatilia mkazo katika utekelezaji majukumu yake ni pamoja na kuona Balozi za Tanzania nje zinaendeshwa kwa tija ili kuongeza pato la taifa.

====================================

HABARI KATIKA PICHA: Waziri Kombo akitembelea miradi ya maendeleo katika Ubalozi wa Tanzania nchini Zimbabwe.












WAZIRI KOMBO AFANYA MAZUNGUMZO NA RAIS WA BADEA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo amefanya mazungumzo na Rais wa Benki ya Kiarabu ya Maendeleo ya Kiuchumi Afrika (BADEA), Dkt. Sidi Ould Tah jijini Harare , Zimbabwe tarehe 13 Agosti, 2024. 

Mazungumzo hayo yamefanyika pembezoni mwa mkutano wa Mawaziri wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ambapo viongozi hao, wamejadili umuhimu wa kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Benki hiyo ambayo imekuwa ikitoa misaada ya kifedha, mikopo nafuu, na ufadhili kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo barani Afrika.

Aidha, Mhe. Balozi Kombo amemueleza Dkt. Tah kuwa Tanzania ipo tayari kushirikiana na wabia wa maendeleo kwa ustawi wa watu wake na Taifa kwa ujumla, hivyo ni matarajio yake kwamba mazungumzo hayo yatafungua maeneo mapya ya ushirikiano kwa manufaa ya pande zote mbili.

Hivyo, katika kuendelea kuimarisha Diplomasia ya Uchumi, Wizara itaendelea kusimamia taratibu za makubaliano ambazo BADEA itaingia na sekta husika ili kuhakikisha nchi yetu inanufaika vyema na fursa za ujenzi wa miundombinu ya kidigitali na upatikanaji wa mawasiliano ya kimtandao (Internet). 

Naye Dkt. Tah ameeleza kuwa Benki hiyo ina nia ya kufadhili nchini Tanzania ujenzi wa Kituo cha kwanza cha kuhifadhi taarifa zinazohusu masuala ya Akili Mnemba (Artificial Intelligence & Robotics) na kwamba kukamilika kwa taratibu za uanzishwaji wa mradi kutawezesha utekelezaji kuanza kwa wakati. Mazungumzo kuhusu suala hili yanaendelea. 

Viongozi wengine walioshiriki mazungungumzo hayo ni Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo na Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe, Mhe. IGP (RTD) Simon Sirro.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo akisalimiana na Rais wa Benki ya Kiarabu ya Maendeleo ya Kiuchumi Afrika (BADEA), Dkt. Sidi Ould Tah walipokutana kwa mazungumzo pembezoni mwa mkutano wa SADC unaoendelea jijini Harare , Zimbabwe tarehe 13 Agosti, 2024.
Mazungumzo yakiendelea
Mazungumzo yakiendelea
Picha ya pamoja
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo akisisitiza alipokuwa kwenye mazungumzo na Rais wa Benki ya Kiarabu ya Maendeleo ya Kiuchumi Afrika (BADEA), Dkt. Sidi Ould Tah jijini Harare, Zimbabwe tarehe 13 Agosti, 2024.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo (kushoto) na Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe, Mhe. IGP (RTD) Simon Sirro (kulia) wakifuatilia
Rais wa Benki ya Kiarabu ya Maendeleo ya Kiuchumi Afrika (BADEA), Dkt. Sidi Ould Tah akiwa kwenye mazungumzo na Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo yaliyofanyika jijini Harare, Zimbabwe

Tuesday, August 13, 2024

NAIBU WAZIRI LONDO AMTEMBELEA KATIBU MKUU JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Dennis Londo (Mb) akisalimiana na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Masharki (EAC) Mhe. Monica Nduva alipomtembelea Ofisini kwake jijini Arusha.

 

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Dennis Londo (Mb) akisaini kitabu cha wageni Ofisini kwa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Masharki (EAC) Mhe. Monica Nduva alipomtembelea  jijini Arusha .
 

 

mazungumzo yakiendelea

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Dennis Londo (Mb) katika picha na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Masharki (EAC) Mhe. Monica Nduva alipomtembelea Ofisini kwake jijini Arusha.
 
 NAIBU WAZIRI LONDO AMTEMBELEA KATIBU MKUU JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI


Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Dennis Londo (Mb) ametembelea Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Masharki (EAC) Mhe. Monica Nduva Ofisini kwake tarehe 13 Agosti 2024 jijini Arusha. 

Katika mazungumzo yao, Mhe. Londo alimuhakikishia Mhe. Nduva ushirikiano na kumuelezea kuwa Tanzania itashiriki katika masuala yote yanayohusu Jumuiya ya EAC kwa uzito unaostahili. 

Ziara hiyo ilikuwa na lengo la kujitambulisha na kufahamiana baada ya Mhe. Londo kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kufuatia mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri yaliyofanyika mwezi Julai 2024. 

Mhe. Londo aliongozana na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Stephen Mbundi.