Monday, August 25, 2014

Mhe. Mjenga akutana na uongozi wa banki ya UBL Dubai

Balozi Mdogo wa Tanzania-Dubai, Mhe. Omar Mjenga akiwa katika picha ya pamoja na watendaji wakuu wa benki ya UBL ya Dubai, Bw. Shaikh Muhammad Liaque, Makamu wa Rais wa UBL (kushoto) na Bw. Syed Abbas Bokhari walipomtembelea ofisini kwake leo.
Wakiwa katika mazungumzo, ambapo Mhe. Mjenga amewaomba kuangalia uwezekano wa kuajiri Watanzania kwenye Benki hiyo kuja kufanya kazi Dubai. Mwaka jana, UBL ilifungua ofisi ya Dar es Salaam kuwa ofisi ya Kanda ya Afrika. Aidha,wamegusia suala la kufungua matawi zaidi Arusha, Moshi, Mwanza, Mbeyana Matawi mengine zaidi Jijini Dar es salaam. Hii yote itafanikisha kuongeza nafasi za ajira kwa Watanzania. 

Sunday, August 24, 2014

Mhe. Membe Amwakilisha Rais Kikwete Michezo ya Shule Afrika Mashariki

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akitoa hotuba kwa niaba ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Uzinduzi wa mashindano ya michezo ya shule za Sekondari za Afrika Mashariki yajulikanayo kama (FEASSA) leo katika Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga (kulia) akifuatilia kwa makini hotuba kutoka kwa Waziri Membe. 
Viongozi mbalimbali wakifuatilia kwa makini hotuba iliyokuwa inatolewa na Waziri Membe kwaniaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard K. Membe akiwapungia mkono wanafunzi wa Shule za Sekondari kutoka Tanzania bara (hawapo pichani).
Wanafunzi wa Shule za Sekondari kutoka Tanzania ambao wanashiriki mashindano ya Shule za Sekondari za Afrika Mashariki wakiwa kwenye maandamano ya uzinduzi wa mashindano hayo leo katika Uwanja wa Taifa
Waziri Membe akipiga Mpira kuashiria kufunguliwa kwa mashindano hayo rasmi
Waziri Membe akisalimiana na wachezaji wa mpira wa miguu kutoka Shule ya Sekondari ya Makongo kabla ya kuanza mechi.
Waziri Membe akisalimiana pia na wachezaji wa shule ya Sekondari ya Mvara kutoka Uganda.
Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa Stars ya Tanzania Martinus Ignatus 'Mart Nooij' (mwenye kofia) naye akiangalia kwa makini mechi kati ya timu ya Makongo Sekondari na Mvara (hawapo pichani) katika Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam
Mechi ikiendelea
Waziri Membe akishangilia baada ya Makongo Sekondari kufunga goli.
Wachezaji wa Makongo Sekondari wakishangilia goli lao
Picha na Reginald Philip
 -------------------------------------------------------------------------------------------


Mhe. Membe Amwakilisha Rais Michezo ya Shule A. Mashariki



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), alimwakilisha Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kufungua Mashindano ya 13 ya Shirikisho la Vyama vya Michezo vya Shule za Sekondari za Afrika Madhariki (FEASSSA), jijini Dar es Salaam Jana.


Mashindano hayo yanahisisha timu za michezo mbali mbali za Shule 205 kutoka Kenya, Uganda, Sudani Kusini, Rwanda, Burundi, Zanzibar na Tanzania Bara, zenye washiriki 3,000.

Mashindano yatarindima kwenye Uwanja wa Taifa kwa siku 10.
Katika hotuba iliyosomwa na Mhe. Membe, Rais Kikwete alisema michezo hiyo ni moja ya mikakati ya utekelezaji wa itifaki ya utengamano wa Afrika Mashariki.
"Aidha, michezo hii ni kiashiria tosha cha azma madhubuti tuliyo nayo ya kuimarisha Umoja wetu," alisema.

Alizitaka Nchi za Afrika Mashariki kushirikiana kuendeleza michezo, akashauri Mashindano hayo yashirikishe pia Shule za msingi.

"Kwa niaba ya Marais wa Nchi za Afrika Mashariki, na kwa niaba ya Nchi yangu, napenda kuwahakikishia kuwa serikali za nchi zote zitaendelea kuwainga mkono na kuwezesha michezo hii kufanyika kila mwaka," alisema.

"Hafla hiyo ilihudhuriwa pia na Mhe. Hawa Ghasia, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa); Mhe. Dkt. Shukururu Kawambwa, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi; Dkt. Abdullah Juma Abdullah, Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mawaziri kutoka Sudani Kusini na Uganda.









Friday, August 22, 2014

Press Release

H.E Michael D. Higgins, President of Ireland

PRESS RELEASE

H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania, has sent a condolence message to H.E. Michael D. Higgins, President of the Republic of Ireland, following the demise of the former Irish Prime Minister H.E. Albert Reynolds on 21st August 2014.

 The message reads as follows:-

“H.E. Michael D. Higgins
  President of the Republic of Ireland
  Dublin
  IRELAND

Your Excellency,

I have received with great sorrow the sad news about the untimely passing away of the former Irish Prime Minister, the late H.E. Albert Reynolds.

I take this opportunity to extend my heartfelt condolences to you and through you to the family of the deceased, the Government and the people of Ireland during the whole mourning period.

The world will remember the late former Prime Minister Reynolds for his tireless efforts on peace keeping processes. It is my prayer that you remain strong during this difficult moment.

We pray to the Almighty God to rest his soul in eternal peace.
Please accept, Your Excellency, the assurances of my highest consideration”.

Issued by: The Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation, Dar es Salaam

22nd August 2014



Wednesday, August 20, 2014

Press Release

H.E János Áder, President of Hungary 

PRESS RELEASE

H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to His Excellency János Áder, President of Hungary on the occasion of the National Day of Hungary. The message reads as follows:-

“H.E. János Áder,
President of Hungary
Budapest
HUNGARY

Excellency and Dear Colleague,

On behalf of the people and Government of the United Republic of Tanzania and on my own behalf, I take this opportunity to convey my sincere congratulations to you, the Government and people of Hungary on the occasion of the National Day of your country.

This historic day offers us another opportunity to reaffirm our commitment to work together both bilaterally and multilaterally on matters of mutual interest and further enhance the relations between our two countries.

Please accept, Your Excellency, my best wishes for your continued good health and prosperity of the people of Hungary”.


Issued by the Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation, Dar es Salaam

20th August 2014


Tuesday, August 19, 2014

Africa Riled for Forgetting Nyerere

The Minister for Foreign Affairs and International Cooperation, Hon. Bernard K. Membe (MP) exchanging views with other Ministers including the Namibian Foreign Minister, Hon. Netumbo Nandi-Ndaitwah (second right) during the  Southern African Development Community (SADC) conference held in Zimbabwe of recent. 

Africa Riled for Forgetting Nyerere

The new generation of African leaders has been criticized for overlooking the contribution of Mwalimu Julius Nyerere,and other founding fathers, to the liberation of the continent.

The new Chairman of the Southern African Development Community (SADC), President Robert Mugabe, told the 34th Summit of the organization, that the region and Africa owed their success to  Mwalimu.

Speaking after taking over the chairmanship from President Arthur Mutharika of Malawi, Mr. Mugabe, whose liberation movement was hosted in Tanzania, lamented that little had been done to honour Mwalimu.

"They have done something for(Kwame) Nkrumah  and (Nelson) Mandela at the AU, but there is nothing for Mwalimu. No symbol," lamented President Mugabe, adding that it was Mwalimu Nyerere who bore the burden of African liberation.

"We must do something (for Mwalimu). Zimbabwe will do something," he promised.

The SADC Chairman also riled at the West for looking the other way as the Israel army massacred innocent civilians in Gaza "in the guise of fighting terrorists.

"Is Israel so precious that it can't be stopped? It is criminal for the world to keep quiet over such crime against humanity," he said.

He also called on the European Union and USA to lift economic sanctions against Zimbabwe after popular elections in his country. He said the sanctions had adverse effect on Zimbabwe's economy.

The two-day ordinary summit ends in Victoria Falls today. It was attended by President Jakaya Kikwete and the Heads of State and Government of South Africa, Malawi, Mozambique, Democratic Republic of Congo, Lesotho, Namibia, Zimbabwe, Madagascar, Mauritius and Seychelles. Angola, Botswana and Zambia were  represented by Vice-Presidents while the kingdom of Swaziland was represented by Prime Minister.

The Tanzanian delegation included the Minister for Foreign Affairs and International Cooperation, Hon. Bernard Membe, the Minister for Industry and Trade, Hon. Abdallah Kigoda and the Zanzibar Minister of state in the President's Office, Hon. Harun Ali Suleiman.

End

Tanzanian winner SADC Essay Competition


President Jakaya Mrisho Kikwete congratulates Neema Stephen a Tanzanian student from Nabote Secondary School in Njombe who won the first prize in  this year's Southern African Development Community (SADC)  Secondary Schools Essay Competition.
----------------------------------------------------------------------------------------------------------
Tanzanian Wins SADC Essay Competition as Zimbabwe decorates Mbita

Neema Stephen, a Form Three student at Nabote Secondary School in Njombe, has won the first prize in this year's Southern African Development Community (SADC)  Secondary Schools Essay Competition, beating Zimbabwe and Swaziland to second and third positions, respectively.

Neema was awarded a certificate and US$1,500. The second winner received $750 and the third prize was $500. Secondary schools in the region were asked to write an essay on the effects of climate change and discuss the remedy.

The prizes were presented to the winners by H.E. Prof. Arthur Peter Mutharika, President of the Republic of Malawi, in his capacity as the outgoing SADC Chairman, at the sideline of the SADC summit.

President Mutharika also presented prizes to winners of mass media competition, which eluded Tanzanians. The SADC Council of ministers has directed the secretariat of the organization to promote the competition among member states.

The competitions are coordinated by the Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation in collaboration with the relevant sectoral ministries.

Meanwhile, the Republic of Zimbabwe has bestowed its highest National Honour, the Royal Order of Munumutapa, on retired Brigadier General Hashim Mbita in recognition of his contribution to the liberation of the Southern African country.

H.E. Robert Mugabe, President of Zimbabwe, announced the decision during the opening of the 34th SADC Summit at Victoria Falls, after launching a nine-volume publication on the Southern Africa liberation struggles, coordinated by General Mbita.

President Mugabe said beside the medal, his government had awarded General Mbita, who was the Executive Secretary of the OAU Liberation Committee for 22 years, US$100,000.
General Mbita could not attend the ceremony due to ill health, and the medal and cheque were received on his behalf by his daughter, Shella.

The OAU Liberation Committee, which was based in Dar es Salaam, was  key in mobilizing arms and military supplies for liberation movements of the Southern Africa region. It was dissolved in 1994 after the defeat of apartheid in South Africa.

The only other non-Zimbabwean recipients of the honour are the Father of the Tanzanian Nation, Mwalimu Julius Nyerere, the first President of Mozambique, H.E. Samora Machel, the First President of Botswana, H.E. Sir Seretse Khama and H.E. Kenneth Kaunda, the first President of Zambia.

Monday, August 18, 2014

Kaimu Katibu Mkuu amkabidhi Hati ya Kiwanja Balozi wa Oman nchini

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya akimkabidhi Hati ya Kiwanja  Balozi wa Oman hapa nchini, Mhe. Soud Al Mohammed Al-Ruqaish  kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi za Ubalozi wa nchi hiyo hapa nchini. Makabidhiano hayo yalifanyika Wizarani tarehe 18 Agosti, 2014.

Balozi Yahya akizungumza na Balozi Al-Ruqaish kabla ya kumkabidhi hati hiyo ya kiwanja.
Mazungumzo yakiendelea.
Picha ya pamoja

Picha na Regiald Philip







Thursday, August 14, 2014

SADC Ministerial Conference starts in Zimbabwe

Minister for Foreign Affairs and International Cooperation, Hon. Bernard K. Membe (C) with Hon. Abdallah Kigoda (R), Minister for Industry and Trade and Ambassador Rajabu Gamaha (L), Acting Permanent Secretary in the Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation  during  the SADC Ministerial Conference held in Victoria Falls, Zimbabwe. Hon. Membe leads  Tanzanian delegation to the SADC Ministerial conference.

Hon. Membe in a  briefing meeting.



SADC MINISTERIAL CONFERENCE GETS UNDERWAY

The Minister for Foreign Affairs and International Cooperation, Hon. Bernard K. Membe, arrived in Victoria Falls, Zimbabwe, early today to lead the Tanzanian delegation to the SADC Ministerial conference.

Ministers from the 15 SADC member countries are meeting in the Zimbabwean resort town to prepare the agenda for the 34th SADC Summit on August 17 and 18, which is expected to be attended by H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania.

The Ministerial delegation includes Hon. Abdallah Kigoda, Minister for Industry and Trade.

The SADC Heads of State and government are scheduled to deliberate on a range of issues on regional cooperation, including review of the region's Industrial Strategic Development Programme.

They will also discuss establishment of a Regional Development Fund, which is proposed to have a seed capital of 1.2billion US dollars.

The Ministerial conference was preceded by a meeting of Senior Officials.
Ambassador Rajabu Gamaha, Acting Permanent Secretary in the Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation led the Tanzania delegation to the meeting.

SADC member countries are Tanzania, Botswana, Angola, Namibia, Mozambique, Malawi, Lesotho, Swaziland, Mauritius, Madagascar,Democratic Republic of Congo,South Africa, Zimbabwe and Zambia.

Ends


Rais Kikwete afungua rasmi Kongamano la Kwanza la Diaspora nchini


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akiingia Ukumbini kwa ajili ya ufunguzi  rasmi wa Kongamano la Kwanza la Diaspora hapa nchini lililoandaliwa kwa ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Taasisi ya Tanzania Diaspora Initiative (TDI). Kongamano hilo lililofanyika kwenye Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam limewakutanisha Watanzania wanaoishi nje ya nchi  kutoka nchi zaidi ya 17 ikiwemo Marekani, Uingereza, Canada, Cambodia, Zambia, Ujerumani, Ufaransa, Poland, Saudi Arabia, Afrika Kusini, China, Tunisia, Comoro na Finland.
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya pamoja na washiriki wengine wa mkutano wakimkaribisha Mhe. Rais Kikwete alipowasili kwa ajili ya kufungua Kongamano la Kwanza la Diaspora hapa nchini.
Mkurugenzi wa Idara ya  Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Mbelwa Kairuki pamaja na Bi. Premi Kibanga, Mwandishi Msaidizi wa Rais  wakati wa mapokezi ya Mhe. Rais Kikwete kwenye Kongamano la Diaspora.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akifungua rasmi Kongamano la Kwanza la Diaspora hapa nchini lililoandaliwa kwa ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Taasisi ya Tanzania Diaspora Initiative (TDI). Kongamano hilo lililofanyika kwenye Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam limewakutanisha Watanzania wanaoishi nje ya nchi  kutoka nchi zaidi ya 17 ikiwemo Marekani, Uingereza, Canada, Cambodia, Zambia, Ujerumani, Ufaransa, Poland, Saudi Arabia, Afrika Kusini, China, Tunisia, Comoro na Finland.
Kaimu Wakurugenzi wa Idara za Afrika na Ulaya na Marekani  katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bibi Victoria Mwakasege (kushoto) na Bi. Zuhura Bundala (wa pili kushoto) wakifuatilia hotuba ya Mhe. Rais Kikwete wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Kwanza la Diaspora. Anayefuata ni Bw. Yusuph Mndolwa, Afisa Mambo ya Nje kutoka Ubalozi wa Tanzania Sweden.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Tanzania Diaspora Initiative (TDI), Bw. Emmanuel Mwachullah nae akizungumza wakati wa Kongamano la Kwanza la Diaspora hapa nchini. Taasisi ya TDI imeshirikiana na Serikali katika kuandaa Kongamano hilo.
Bw. Caesar Waitara, Afisa Mambo ya Nje kutoka Ubalozi wa Tanzania Ujerumani akiwa na Bw. Peter Kazaura, Mwanadiaspora kutoka Ujerumani
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bibi. Rosemary Jairo akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakati wa Kongamano hilo.
Maafisa Mambo ya Nje wakinukuu hotuba ya Mhe. Rais Kikwete. Kulia ni Bw. Celestine Kakele na Bw. Deogratius Dotto.
Mshereheshaji wakati wa Kongamano hilo kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Bi. Suzane Mzee akiwajibika.
Maafisa Mambo ya Nje wakifuatilia hotuba ya Mhe. Rais.


Mhe. Rais Kikwete akizindua rasmi Tovuti ya Diaspora wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Kwanza la Diaspora. Wanaoshuhudia wengine ni Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda.
Mwonekano wa Tovuti hiyo inayoitwa www.tanzaniadiaspora.org   
Mhe. Rais Kikwete katika picha ya pamoja na Mhe. Pinda, Mama Jairo, Mkurugenzi wa Tanzania Diaspora Initiative na Mwakilishi wa Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) hapa nchini Bw. Damien Thuriaux
Mhe. Rais Kikwete na Mhe. Pinda katika picha ya pamoja na kundi la Wanadiaspora kutoka nchi za Ulaya
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy akibadilishana mawazo na mmoja wa wageni waalikwa mara baada ya ufunguzi rasmi wa Kongamano la Kwanza la Diaspora nchini.

Picha  na Reginald Philip








Wanafunzi wa Vyuo wapata semina kuhusu utendaji wa Umoja wa Mataifa Wizarani

Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy akitoa mada kuhusu  Utendaji kazi wa Idara yake na mfumo mzima wa utendaji kazi wa Umoja wa Mataifa na Uhusiano wa Mashirika ya Kimataifa na Tanzania katika semina kwa  Wanafunzi wa Chuo cha Diplomasia (CFR), Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) na Chuo Kukuu cha Dar es Salaam (UDSM), wanaofanya mafunzo kwa vitendo  Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Baadhi ya Wanafunzi hao wakimsikiliza Balozi Mushy (hayupo pichani)
Maafisa Mambo ya Nje kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa wakimsikiliza Balozi Mushy (hayupo pichani)
Semina ikiendelea

Picha na Reginald Philip

Wednesday, August 13, 2014

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais Kikwete, Mgeni Rasmi katika Mkutano wa Diaspora

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi katika mkutano wa Watanzania wanaoishi ughaibuni (Diaspora) ambao umepangwa kufanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam tarehe 14 na 15 Agosti 2014.

Mkutano huo ambao umeandaliwa kwa ushirikiano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Taasisi ya Diaspora Tanzania (Tanzania Diaspora Initiative-TDI), unalenga kuwahamasisha Watanazania wanaoishi ughaibuni wenye utaalamu na mitaji kurudi nchini au kuwekeza katika shughuli mbalimbali kwa madhumuni ya kukuza uchumi wa nchi.

Aidha, Mkutano huo ambao ni wa kwanza kufanyika nchini, wenye kaulimbiu “Unganisha, Shiriki, Toa taarifa na Wekeza” (Connect, Engage, Inform and Invest) utatoa nafasi kwa washiriki kutambua vyema fursa za uwekezaji na ajira zinazopatikana Tanzania.


Imetolewa na: Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Dar es Salaam

13 Agosti, 2014