Tuesday, July 14, 2015
Monday, July 13, 2015
Press Release
Friday, July 10, 2015
Wizara ya Mambo ya Nje yamuaga Balozi wa Palestina
Balozi Simba akitoa neno la shukrani kwa Balozi wa Palestna nchini. |
Picha juu na chini ni Mabalozi wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Balozi Simba (Hayupo pichani) |
Balozi Jaish akitoa neno la shukrani kwa ushirikiano na upendo aliokuwa akipata kutoka Wizarani na kwa watanzania kwa ujumla. |
Balozi Jaish akiendelea kuongea. |
Naibu Katibu Mkuu, Balozi Simba akimpongeza Balozi Jaish mara baada ya kumaliza kuzungumza |
Balozi Jaishi akimkabidhi Balozi Simba zawadi ya Picha yenye mfano wa Nyumba ya Ibada (Msikiti) |
Naibu Kaitbu Mkuu Balozi Hassan Simba Yahya akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Palestina aliyemalimaliza muda wake wa uwakilishi nchini Tanzania. |
Picha na Reginald Philip
Thursday, July 9, 2015
MEMBE ASISITIZA UMUHIMU WA VIWANDA
Makamu wa Rais wa zamani wa Benki ya Dunia, Prof. Justin Yifu Lin akitoa mada yake juu ya uwanzishaji wa viwanda nchini Tanzania katika muadhara ulioandaliwa na Wizara ya Mambo ya Nje |
Balozi Simba akichangia mada katika muadhara uliokuwa ukiendelea |
Muhadhiri Chuo cha Diplomasia Bw. Innocent Shoo akiuliza swali |
Afisa Mambo ya Nje Bi. Felisita Rugambwa naye akiuliza swali katika muhadhara
|
Picha ya juu na chini ni watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje nao wakisikiliza mada kwa makini |
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Liberata Mulamula akizungumza jambo huku akisikilizwa na Prof. Lin (Kulia) na Mhe. Membe (Katikati). |
Kaimu Mkurugenzi, Idara ya Diaspora Bi. Rosemary Jairo akizungumza jambo kwa Prof. Lin (kushoto) na Katibu Mkuu Balozi Mulamula. |
Picha na Reginald Philip
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe, amesema upatikanaji wa gesi ni nyenzo muhimu ya uendelezaji wa viwanda vya kati ili kutengeneza ajira na kuharakisha maendeleo ya nchi.
Mhe. Membe alipongeza uamuzi wa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China kuichagua Tanzania kuwa miongoni mwa nchi tatu za Afrika itakapohamishia baadhi ya viwanda vyake, akazitaka taasisi za uwekezaji na uendelezaji wa viwanda kuweka mikakati madhubuti ya kutumia fursa hiyo kikamilifu.
Mhe. Waziri alisema hayo leo wakati wa mhadhara wa aliyekuwa Mchumi Mkuu na Makamu wa Rais Mwandamizi wa Benki ya Dunia, Prof. Justin Yifu Lin, kwenye Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere, jijini Dar Es Salaam, uliohudhuriwa na wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na wadau wengine.
Alisema uendelezaji wa viwanda lazima utiliwe mkazo katika mpango wa Tanzania kuingia uchumi wa kati 2025. "Tuache kukimbilia viwanda vikubwa vinavyohitaji mitaji mikubwa, ambayo hatuna.Tuchague viwanda vya kati vitakavyoajiri watu wengi kwa uwekezaji wa wastani."
Mhe. Membe alisema uendelezaji wa viwanda usambae nchi nzima ili kuvutia vijana kuishi vijijini badala ya kukimbilia mijini. "Sasa hivi nchi yetu ina viwanda takriban 3,000 lakini zaidi ya theluthi mbili viko Dar Es Salaam. Lazima umeme upelekwe vijijini kuleta uwiano wa maendeleo ya viwanda," alisisitiza.
Katika mhadhara wake, Prof. Lin alisema nchi nyingi zinazoendelea zilifanya maamuzi yasiyo sahihi kuhusu viwanda. "Nchi nyingi zilifuata kile kinachoitwa Muafaka wa Washington na kuanzisha viwanda vikubwa kwa maelekezo ya nchi tajiri, ambavyo viliwashinda kuendesha kwa kuwa vilihitaji uwekezaji mkubwa sana."
Alisema nchi za Asia zilizoendelea kwa haraka ni zile zilizoamua kuzingatia mazingira halisi na kwenda hatua kwa hatua katika kuanzisha viwanda. "Hii iliimarisha uchumi wao na kuukuza."
Prof. Lin alisema serikali zina wajibu wa kusimamia uendelezaji wa viwanda kwa kuweka sera sahihi, kuhimiza uwekezaji kwenye uzalishaji wa bidhaa zenye masoko ya uhakika na kusaidia sekta binafsi ishiriki kikamilifu.
Akiongelea Tanzania, Mchumi huyo wa Kichina alisema ingawa gharama za ajira ziko chini, gharama za uendeshaji ziko juu, hivyo hazivutii uwekezaji. Alisema moja ya sababu kubwa za Shilingi ya Tanzania kushuka thamani ni uuzaji mdogo wa bidhaa nchi za nje.
(mwisho)
Monday, July 6, 2015
Rais Kikwete aongoza Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi wa EAC kuhusu Burundi
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa
Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Mhe.Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na baadhi ya Wawakilishi wa Wakuu wa Nchi Wanachama wakiimba Wimbo wa Jumuiya hiyo tayari kwa kuanza Mkutano wao Dharura wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya hiyo uliofanyika Ikulu, Dar es Salaam tarehe 06 Julai, 2015.
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dkt.Richard Sezibera akisoma Maazimio yaliyofikiwa katika Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi wa EAC huku Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Rais Kikwete (wa tano kutoka kushoto waliokaa) pamoja na viongozi wengine wakisikiliza kwa makini. Pamoja na mambo mengine Wakuu wa Nchi wamemteua Rais Museveni kusimamia majadiliano ya makundi yanayopingana nchini Burundi na Uchaguzi wa Rais ufanyike tarehe 30 Julai, 2015 badala ya tarehe 15 Julai mwaka huu.
Katibu mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Liberata Mulamula (katikati) kwa pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afrika Mashariki, Bi.Joyce Mapunjo (kulia) pamoja na wajumbe wengine waliohudhuria mkutano huo wakiimba wimbo wa Jumuiya.
Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Mhe. Chirau Ali Mwakere pamoja na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Kenya, Mhe. Phyllis Kandie
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Zuhura Bundala akiwa na Wajumbe wengine kabla ya mkutano kuanza
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Zuhura Bundala akiwa na Wajumbe wengine kabla ya mkutano kuanza
Balozi wa Tanzania nchini Rwanda, Mhe.Ali Siwa (katikati) na Balozi wa Tanzania nchini Uganda, Mhe.Ladislaus Komba (kulia) wakati wa mkutano huo.
Afisa Mwandamizi kwenye Ubalozi wa Tanzania nchini Burundi, Bi. Victoria Mwakasege akiwa na Afisa Mwandamizi, Ofisi ya Rais wakisikiliza maazimio ya wakuu wa nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki yakisomwa.
Afisa Mwandamizi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bw.Mkumbwa Ally akijadiliana jambo na Afisa wa Mambo ya Nje, Bi.Samira Diria muda mfupi kabla ya mkutano huo kuanza.
Sehemu ya Wajumbe waliohudhuria mkutano huo uliofanyika Ikulu, Jijini Dar es Salaam.
Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Picha ya pamoja.
Picha na Reuben Mchome
==================================
Picha na Reuben Mchome
==================================
Wakuu
wa Nchi wa EAC wamteua Rais Museveni kusimamia majadiliano nchini Burundi
Mkutano wa Tatu wa
Dharura wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kujadili hali ya
kisisasa nchini Burundi umefanyika Jijini Dar es Salaam tarehe 06 Julai, 2015
chini ya Uenyekiti wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho
Kikwete.
Katika Mkutano huo
ambao umehudhuriwa pia na Rais wa Uganda, Mhe. Yoweri Kaguta Museveni na
Mawaziri wa Mambo ya Nje na wale wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki kutoka nchi
zote wanachama, umeazimia masuala mbalimbali kwa ajili ya kuhakikisha hali ya
kisiasa na utulivu nchini Burundi
inarejea.
Katika mkutano huo,
Wakuu wa Nchi wamemteua Rais wa Uganda, Mhe. Yoweri Kaguta Museveni kusimamia
majadiliano ya makundi yanayopingana nchini Burundi.
Pia wakuu hao wa nchi
wameitaka Serikali ya Burundi kuyanyang’anya silaha makundi yote nchini humo
kikiwemo kikundi kinachojiita Imbonera
Kure”. Aidha, wameomba Umoja wa Afrika (AU) usimamie zoezi hili kwa
kupeleka Timu ya Waangalizi wa Kijeshi ili kuhakikisha linafanikiwa.
Azimio jingine
ni kuvitaka vyombo vya usalama chini ya Sekretarieti ya Maziwa Makuu (ICGLR) kutafiti
na kuhakiki uwepo wa kikundi cha waasi cha FDLR nchini Burundi.
Aidha, Wakuu wa Nchi wameitaka
Serikali ya Burundi kuahirisha Uchaguzi wa Rais uliopangwa kufanyika tarehe 15 Julai, 2015 na sasa
ufanyike tarehe 30 Julai, 2015 ili kutoa muda kwa msuluhishi kusimamia
majadiliano kama ilivyopangwa.
Wakuu hao wa nchi pia
wametaka yeyote atakayeshinda nafasi ya Urais nchini Burundi kuunda Serikali ya
Umoja wa Kitaifa itakayojumuisha vyama vilivoshiriki kwenye Uchaguzi na vile
ambavyo havikushiriki.
Pia, Wakuu wa nchi
wameitaka Serikali ya Burundi kuheshimu Mkataba wa Amani na Maridhiano wa
Arusha wa mwaka 2000 na kutoifanyia marekebisho ya aina yoyote Katiba ya
Burundi.
Vilevile, Wakuu hao wa
nchi wameiomba AU kuidhinisha na kupitisha maamuzi haya ya EAC na kwamba
Jumuiya hiyo ya Afrika Mashariki itatuma Timu ya Waangalizi katika Uchaguzi wa
Rais nchini Burundi.
-Mwisho-
Rais Museni awasili nchini kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa EAC
Mhe. Rais Museveni akisilimiana na Wakuu wa Vyombo vya Usalama waliofika Uwanjani kumpokea. |
Mhe. Rais Museveni akiongozana na mwenyeji wake Waziri Membe mara baada ya kuwasili |
Mhe. Rais Museveni akikagua Gwaride la Heshima |
Rais Museveni kwa pamoja na Waziri Membe wakifuatilia burudani kutoka kwa moja ya kikundi kilichokuwepo uwanjani hapo kwa mapokezi |
Sunday, July 5, 2015
Mkutano wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa EAC wafunguliwa Jijini Dar es Salaam
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) Dkt. Richard Sezibera naye akizungumza wakati wa mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Afrika Mashariki |
Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa nao wakifuatilia kwa makini ufunguzi wa Mkutano huo |
Waziri wa Afrika Mashariki nchini Rwanda, Mhe. Valentine Rugwabiza (wa pili kushoto) pamoja na wajumbe wengine waliohudhuria Mkutano huo. |
Balozi wa Tanzana nchini Burundi Mhe. Rajab Gamah (Kushoto) akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uganda, Mhe. Henry Okello Oryem |
Maafisa Mambo ya Nje nao wakifuatilia kwa makini ufunguzi wa Mkutano wa Dharura wa Baraza la Mawaziri. Kutoka kushoto ni Bw. Ally Ubwa, Bi. Grace Martin na Bw. Mudrick Soraga |
Mkutano ukiendelea
Picha na Reginald Philip
|
Subscribe to:
Posts (Atom)