Monday, July 6, 2015

Rais Museni awasili nchini kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa EAC

Rais wa Uganda, Mhe. Yoweri Kaguta Museveni akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere  Jijini Dar es Salaam. Mhe. Rais Museveni yupo nchini kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuhusu hali ya kisisasa nchini Burundi utakaofanyika Ikulu, Dar es Salaam tarehe 06 Julai, 2015.
Mhe. Rais Museveni akisilimiana na Wakuu wa Vyombo vya Usalama waliofika Uwanjani kumpokea.
Mhe. Rais Museveni akiongozana na mwenyeji wake Waziri Membe mara baada ya kuwasili
Mhe. Rais Museveni akikagua Gwaride la Heshima
Rais Museveni kwa pamoja na Waziri Membe wakifuatilia burudani kutoka kwa moja ya kikundi kilichokuwepo uwanjani hapo kwa mapokezi
Mhe. Rais Museveni akimsikiliza Mhe. Membe  katika mazungumzo mafupi kabla ya kuondoka Uwanjani hapo. Wengine katika picha ni Balozi wa Tanzania nchini Uganda, Mhe. Ladislaus Komba (kushoto), Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Mhe. Sofia Mjema (mwenye kitambaa kichwani) na Mwakilishi kutoka Ubalozi wa Uganda hapa nchini.

Picha na Reginald Philip


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.