Thursday, July 16, 2015

Waziri Membe afuturisha Mashehe na watumishi wa Wizara

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,  Mhe. Bernard K. Membe akiwakaribisha  Mashehe pamoja na  Watumishi wa Wizara (hawapo pichani)   kabla  ya kushiriki  Futari aliyoiandaa kwa ajili yao nyumbani kwake Oysterbay Jijini Dar es Salaam  hivi karibuni.
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy (wa kwanza kulia), akiwa pamoja na Mashehe walioudhuria Futari hiyo
Waziri Membe akiendelea kuzungumza na kuwakarisha wageni wote nyumbani kwake
Mkurugenzi Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Nigel Msangi akitoa neno la shukrani kwa Mhe. Waziri Membe na Familia yake  kwa niaba ya Watumishi wa Wizara na Wageni wengine walioalikwa  kufuturu pamoja na Mhe. Membe nyumbani kwake
Mhe. Membe akiwa na Kadhi Mkuu walioshiriki futari hiyo
Sehemu ya Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje walioshiriki futari nyumbani kwa Mhe. Membe
Wageni waalikwa
Mke wa Waziri Membe, Mama Dorcas Membe (kushoto) akiwa na Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Irene Kasyanju wakati wa futari iliyoandaliwa na Familia ya Waziri Membe kwa Watumishi wa Wizara.
Sehemu ya Watumishi wa Wizara wakifuatilia hotuba wakati wa futari nyumbani kwa Mhe. Membe. Kutoka kulia ni Mkurugenzi wa APRM, Bibi Rehema Twalib, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Bi. Mindi Kasiga na Bi. Aisha Mandia.
Sehemu nyingine ya Watumishi wa Wizara wakifuatilia hotuba mbalimbali wakati wa futari hiyo
Watumishi wa Wizara wakiwa wametulia kabla ya kuanza kufuturu
Waziri Membe akimpongeza Kadhi Mkuu baada ya kuhutubia
Shehe  akitoa dua kabla ya kuanza kufuturu
Dua ikiendelea
Mhe. Membe akiwaongoza wageni wake kuchukua futari

Waziri Membe akiwa katika picha ya pamoja na Mashehe na Wageni wengine aliwaalika kufuturu pamoja nae.

Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.