Thursday, July 30, 2015

Rais Museveni awasili nchini kuhudhuria Mkutano wa Jukwaa la Uongozi la Afrika

Rais wa Uganda, Mhe.Yoweri Kaguta Museveni akipokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Bw.Said Meck Sadiq mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius  Nyerere, tayari kwa kuhudhuria mkutano wa Jukwaa la Uongozi la Afrika unaofanyika Jijini Dar es Salaam tarehe 30 na 31 Agosti, 2015
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Zuhura Bundala akisalimiana na Rais Museveni baada ya kuwasili uwanjani hapo .

Mhe. Rais Museveni akikagua gwaride rasmi lililoandaliwa kwa ajili yake.
Rais Mstaafu, Mhe.Benjamin William Mkapa ambaye ni Mwenyeji wa mkutano huo akimpokea Rais Museveni katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam tayari kuanza kwa mkutano huo. 
Mhe. Mkapa akimkaribisha Rais Museveni tayari kuhutubia mkutano.
Rais  Museveni akihutubia mkutano huo.
 Mkutano huo ukiendelea.
Rais Museveni na Mhe. Mkapa wakiwa na baadhi ya  Viongozi wastaafu wa Afrika waliohudhuria mkutano huo akiwemo Mhe. Festus Mogae (wa kwanza kushoto), Rais Mstaafu wa Botswana, Mhe, Olusegun Obasanjo (wa pili kushoto), Rais Mstaafu wa Nigeria,  Mhe. Jerry Rawlings (wa tatu kutoka kulia), Rais Mstaafu wa Ghana, Mhe. Bakili Muluzi (wa pili kulia), Rais mstaafu wa Malawi na Mhe. Hifikepunye Pohamba (wa kwanza kulia), Rais Mstaafu wa Namibia.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.