Monday, July 20, 2015

Ujumbe wa Maafisa Waandamizi kutoka Nigeria watembelea Wizara ya Mambo

Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya akiukaribisha Ujumbe wa Maafisa Waandamizi kutoka Taasisi ya Taifa ya Mafunzo ya Sera na Stratejia ya Nigeria walipotembelea Wizarani  tarehe 20 Julai, 2015. Ujumbe huo upo nchini kwa ziara ya mafunzo ya siku 12 ambapo watatembelea Wizara na Taasisi mbalimbali za hapa nchini.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Zuhura Bundala akimkaribisha Kaimu Katibu Mkuu kuzungumza na ujumbe huo kutoka Nigeria.
 JUU NA CHINI:
Baadhi ya wajumbe wa msafara huo wakimsikiliza Kaimu Katibu Mkuu (hayupo pichani) wakati wa kikao hicho.

 Kaimu Katibu Mkuu, Balozi Simba akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa msafara huo Bw.Hamakim Jonny Godwin. 
Picha ya pamoja.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.