Friday, July 10, 2015

Wizara ya Mambo ya Nje yamuaga Balozi wa Palestina

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano  wa Kimataifa, Balozi Hassan Simba Yahya akimkabidhi picha yenye mchoro wa Mlima Kilimanjaro Balozi wa Palestina aliyemaliza muda wake wa uwakilishi nchini Tanzania, Mhe. Dkt. Nasri Abu Jaish. Makabidhiano hayo yalifanyika wakati wa hafla ya chakula cha mchana kilichoandaliwa kwa heshima yake na Wizara ya Mambo ya Nje.
Balozi Simba akitoa neno la shukrani kwa Balozi wa Palestna nchini.
Picha juu na chini ni Mabalozi wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Balozi Simba (Hayupo pichani)
Balozi Jaish akitoa neno la shukrani kwa ushirikiano na upendo aliokuwa akipata kutoka Wizarani na kwa watanzania kwa ujumla.  
Balozi Jaish akiendelea kuongea. 
Naibu Katibu Mkuu, Balozi Simba akimpongeza Balozi Jaish mara baada ya kumaliza kuzungumza
Balozi Jaishi akimkabidhi Balozi Simba zawadi ya Picha yenye mfano wa Nyumba ya Ibada (Msikiti)
Naibu Kaitbu Mkuu Balozi Hassan Simba Yahya akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Palestina aliyemalimaliza muda wake wa uwakilishi nchini Tanzania.
Balozi Simba (Wa tatu kutoka kushoto), Balozi Jaish (Wa nne Kutoka kulia), wakiwa katika picha ya pamoja na Balozi Joseph Sokoine (Wa pili Kutoka Kushoto), Kaimu Mkurugenzi Idara ya Mashariki ya Kati Bwa. Elibariki N. Maleko, wa kwanza, wapili na watatu ni Maafisa Mambo ya Nje.


Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.