Friday, July 3, 2015

Rais Kikwete aweka jiwe la msingi kuzindua ujenzi wa jengo la MICT

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete (mwenye tai nyejundu) akiwa pamoja na viongozi mbalimbali katika eneo la Lakilaki jijini Arusha linalojengwa jengo la taasisi ya Mechanism for International Criminal Tribunals (MICT) inayorithi shughuli za Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR). Mhe. Rais aliweka jiwe la msingi la ujenzi huo jijini Arusha tarehe 01 Julai 2015

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete wa tano kutoka kulia akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Serikali na viongozi wa Umoja wa Mataifa waliopo Arusha na waliomwakilisha Katibu Mkuu wa Umoja huo katika sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi


Balozi Irene Kasyanju, Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje (wa pili kulia), Bi. Tully Mwaipopo, Afisa wa Uabalozi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa pamoja na Amer Jandu wa pili kutoka kushoto na Bw. Samuel Akorimo, Afisa Mkuu wa MICT, Arusha wakiwa eneo la Lakilaki. Bw. Jandu ni mmiliki wa kampuni ya kitanzania iliyoshinda kandarasi ya kujenga jengo hilo.


Balozi Celestine Mushy, Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda wa kwanza kulia na Balozi Kasyanju wakiwa katika picha ya pamoja na wawakilishi wa Umoja wa Mataifa mbele ya jiwe la msingi lililowekwa na Rais Kikwete.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Balozi Hassan Simba Yahya wa pili kushoto, Balozi Kasyanju, Balozi Mushy na Bw. Akorimo wakikagua eneo la ujenzi kabla ya shughuli za uwekaji wa jiwe la msingi kuanza.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.