Thursday, August 16, 2018

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan awasili mjini Windhoek, Namibia kushiriki mkutano wa 38 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amewasili leo tarehe 15 Agosti 2018 katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Hosea Kutako mjini Windhoek, Namibia ambapo atamwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) utakaofanyika tarehe 17 na 18 Agosti 2018. 
Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na mawaziri wa Serikali ya Namibia waliowasili kumpokea katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Hosea Kutako mjini Windhoek, Namibia. wa kwanza kulia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Christine !!Hoebes na wa kwanza kushoto ni Waziri wa Elimu ya juu, Mafunzo na Ubunifu, Mhe. Dkt Itah Kandjii-Murangi.

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Hosea Kutako mjini Windhoek,Namibia.

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Hosea Kutako mjini Windhoek,Namibia.

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango wa Serkali ya Mapinduzi Zanzibar, Bw. Ali Khamis Juma mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Hosea Kutako mjini Windhoek,Namibia.

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Namibia mwenye makazi yake nchini Afrika Kusini, Mhe. Sylivester Ambokile mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Hosea Kutako mjini Windhoek,Namibia.
Makamu wa Rais , Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana Naibu Mwanasheria Mkuu, Dkt. Evaristo Longopa mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Hosea Kutako mjini Windhoek, Namibia.

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Balozi wa Namibia nchini Tanzania, Mhe. Theresia Samaria mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Hosea Kutako mjini Windhoek,Namibia.
Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Bw. Edwin Mhede mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataiafa wa Hosea wa Kutako mjini Windhoek, Namibia.
Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Khatibu Kazungu mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Hosea Kutako mjini Windhoek,Namibia.

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na   Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Innocent Shiyo mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Hosea Kutako mjini Windhoek,Namibia.
Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Afisa Mambo ya Nje Mwandamizi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Agness Kayola mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Hosea Kutako mjini Windhoek,Namibia.
Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Afisa Mambo ya Nje, Bi. Zulekha Fundi mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Hosea Kutako mjini Windhoek,Namibia.

Wednesday, August 15, 2018

Ubalozi wa Tanzania nchini Korea waandaa kongamano kuhamasisha wawekezaji sekta ya afya

Mgeni Rasmi katika Kongamano la kuhamasisha uwekezaji katika viwanda vya madawa na vifaa tiba nchini Bw. Geoffrey Mwambe, Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji (TIC) akitoa hotuba ya ufunguzi, kwa niaba ya Mhe. Ummy Ally Mwalimu (Mb), Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto, wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.   

Picha ya pamoja meza kuu: Kutoka kushoto: Makamu Mwenyekiti wa Korea-Africa Foundation (KAF), Mkurugenzi Mtendaji wa TIC, Bw. Geoffrey Mwambe, Balozi wa Tanzania Korea Mhe. Matilda Swilla Masuka, “Congressman” KIM Gyu-hwan, Rais wa KAF, Balozi Yeon-ho CHOI, na mwisho kulia ni Katibu Mtendaji wa Chama cha watengenezaji madawa (TAPI), Bw. Abbasi S. Mohamed.

Balozi wa Tanzania nchini Korea Kusini, Mhe. Matilda Swilla Masuka akitoa neno la ukaribisho katika Kongamano hilo.


Rais wa “Korea-Africa Foundation” waandaaji wenza wa Kongamano hilo, Balozi CHOI, Yeon-ho, akitoa neno katika hafla ya ufunguzi.


“Congressman” na Katibu wa “National Assembly Forum for Africa’s New Era” katika Bunge la Jamhuri ya Korea, Mhe. KIM, Gyu-hwan akitoa salamu za pongezi katika Kongamano hilo.  

 
Picha ya Pamoja ikijumuisha meza kuu na watoa mada kutoka: TIC, TFDA, MSD, Korea Health Industry Development Institute (KHIDI) na “Korea Medical Devices Industrial Association”.

Add caption

Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa TIC Bw. Geoffrey Mwambe ulipokutana na Kampuni ya LS watengenezaji wakubwa wa Matrekta na vifaa vya kilimo nchini Korea Kusini wenye lengo la kupanua wigo wa biashara kwa kuwa na uwakilishi na pia kuwekeza kwenye kiwanda “Assembly Plant”. 

Sehemu ya ujumbe kutoka Tanzania wakiwa na mwenyeji wao Balozi Matilda Swilla Masuka, baada ya kufanikisha Kongamano hilo la aina yake na lililovutia makampuni ya madawa na vifaa tiba zaidi ya 100.

Ujumbe kutoka Tanzania ukiwa katika picha ya pamoja na Wana Diaspora ambao walishiriki kikamilifu katika Kongamano hilo la kuhamasisha wawekezaji katika viwanda vya madawa na vifaa tiba.

Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa TIC, Bw. Geoffrey Mwambe, ulipotembelea Kampuni ya kutengeneza Madawa ya Celltrion, na kujionea shughuli mbalimbali za kampuni hiyo. Celltrion ni kampuni maarufu na inashika Na.1 nchini Korea katika “ sekta ya Bio-pharmacy”. Wakati za ziara hiyo ujumbe wa Tanzania uliambatana na Balozi wa Tanzania Korea, Mhe. Matilda Swilla Masuka, na Rais wa “Korea-Afrika Foundation”, Balozi Yeon-ho CHOI

===================================================================
KONGAMANO LA BIASHARA NA UWEKEZAJI
KUHAMASISHA WADAU WA MADAWA NA VIFAA TIBA KUWEKEZA NCHINI TANZANIA LAFANYIKA SEOUL, KOREA

Ubalozi wa Tanzania uliopo Seoul nchini Korea kwa kushirikiana na “Korea-Africa Foundation” na “Korea Chamber of Commerce and Industry” uliandaa Kongamano la Biashara na Uwekezaji kwa wadau wa sekta ya Afya lililofanyika Seoul, Jamhuri ya Korea.  Kongamano hilo la aina yake, liliandaliwa ili kuunga mkono juhudi za Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuboresha sekta ya Afya.

Kongamano hilo lililenga kuhamasisha uanzishwaji wa viwanda vya madawa na vifaa tiba nchini Tanzania, lilihudhuriwa na makampuni zaidi ya 100, kutoka pande zote mbili ikijumuisha: Makampuni ya utengenezaji madawa na vifaa tiba; Vyuo Vikuu; Taasisi za utafiti; Hospitali; Vyama vya watengenezaji wa madawa na vifaa tiba; Makampuni kutoka katika sekta binafsi; na Diaspora wa Tanzania waliopo Seoul.


Wakati wa Kongamano hilo, mada mbalimbali ziliwasilishwa zikijumuisha: Fursa zilizopo Tanzania katika sekta ya utengenezaji wa madawa na vifaa tiba; Mazingira ya ufanyaji biashara na vivutio “incentives” vinavyotolewa na Serikali; Hali ya soko na uhitaji (Market Potentiality); Taratibu za kufuatwa katika uingizwaji wa bidhaa za madawa na uanzishwaji wa viwanda husika; na Utayari wa sekta binafsi katika kushirikiana na wenzao wa Korea katika biashara na ubia katika viwanda vya madawa na vifaa tiba.

Kongamano hilo lilijumuisha wadau kutoka Wizara na Taasisi za kuitendaji za hapa nchini ikiwa ni pamoja na  Wizara ya Afya; Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki; Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji; Kituo cha Uwekezaji (TIC); MSD; TFDA, na Chama cha wenye Viwanda vya Dawa Tanzania (Tanzania Association Pharmaceutical Industries-TAPI).


Kwa upande wa Korea wawakilishi walitoka  Vyama vya watengenezaji wa madawa na vifaa tiba walitoa mada iliyokuwa na lengo la kubadilishana uzoefu na upande wa Tanzania. Kongamano lilihitimishwa kwa B2B, ambapo makampuni na Taasisi zilikutana kujadiliana zaidi fursa, maeneo ya ushirikiano, na kupata ufafanuzi wa kina katika maeneo mbalimbali; na baadaye kutembelea Makampuni ya Madawa.       





Ziara ya Kikazi ya Chuo cha Diplomasia nchini India.


Chuo cha Diplomasia Tanzania (Center for Foreign Relation -CFR) wamefanya ziara ya kikazi nchini India kuanzia tarehe 13-15 Agosti 2018. Ziara hiyo imekuja kufuatia mwaliko wa Taasisi ya Mafunzo ya Kidiplomasia ya India (Foreign Service Institute-FSI), na ililenga kujua shughuli za FSI na taasisi zinazoshirikiana nazo, pamoja na kujadiliana juu ya uwezekano wa kuingia katika makubaliano ya ushirikiano. 
Wajumbe wa CFR waliongozwa na Balozi Ombeni Sefue, Katibu Mkuu Kiongozi (Mst.), ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi ya CFR. Wajumbe wengine walikuwa ni pamoja na Kaimu Mkuu wa cha  Diplomasia (CFR), Dr Bernard Achiula, Dr Lucy Shule wa CFR, Dr Richard Mbunda kutoka UDSM, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia (DAA), Bibi Justa Nyange. Kutoka ubalozi wa Tanzania nchini India, alikuwepo Balozi Baraka Luvanda na Bibi Natihaika Msuya, Afisa Mambo ya Nje.

 Aidha, wajumbe hao walipata fursa ya kutoa mihadhara katika Kituo cha Stadi za Masuala ya Afrika katika Chuo Kikuu cha Nehru, Taasisi ya Stadi za Masuala ya Ulinzi na Usalama (IDSA) pamoja na Taasisi ya Tafiti Mahususi kuhusu ushirikiano baina ya Nchi za Kusini (South Cooperation Research Information System-RIS).
Kwa ujumla, ziara hiyo imekuwa ya mafanikio makubwa ambapo taasisi wenyeji zimeonesha dhamira ya dhati ya kushirikiana na CFR katika kujenga uwezo wa wanadiplomasia wa Tanzania.
Balozi Ombeni Sefue akimkabidhi  Mkuu wa Taasisi ya Stadi za Masuala ya Afrika, Profesa Ajay Dubey zawadi ya Kinyago.


Newly elected Member of Parliament in Pakistan with African Origin.



Tanzeela Qambrani, an African- Pakistanis woman whose ancestors originate from Tanzania has been elected as a Member of Parliament in Pakistan. She was nominated by the Pakistan People Party (PPP).  Qambrani has been elected to a special seat for women in the provincial parliament in Sindh. She aims at eliminating the stigma attached to her community, known as the Habashi, Sibbi or Sheedi who are the descendants of the Bantu people from Africa.

Tuesday, August 14, 2018

Wajumbe wa Mauritius wa wasili nchini kuangalia maeneo ya Uwekezaji wa viwanda vya sukari.



Ujumbe wa Serikali ya Mauritius ukiongozwa na Balozi wao mwenye Makazi yake Mjini Maputo, Msumbiji Mhe. Jean Pierre Jhumun umewasili nchini kwa ajili ya kukamilisha taratibu za uwekezaji wa viwanda vya sukari.

Ukiwa nchini, ujumbe huo umepanga kukutana na Viongozi mbalimbali wakiwemo;  Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Waziri wa Kilimo, Waziri wa Mazingira (Ofisi ya Makamu wa Rais), Uongozi wa kituo cha Uwekezaji (TIC), Bodi ya Sukari pamoja na kuonana na Uongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Pichani, ni Balozi Jhumun (kushoto) na Bwana Gansam Boodram (kulia) , CEO wa Mauritius Sugar Board, pamoja Mhe. Balozi Ramadhan Mwinyi (kati) ambaye ni Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushikiano wa Afrika Mashariki

Aidha, Ujumbe huo unategemea kutembelea maeneo mbalimbali, ikiwemo mkoa wa Pwani, Wilaya ya Rufiji kwa ajili ya kuangalia maeneo ambayo wanategemea kuanza awamu ya kwanza ya uanzishaji wa kiwanda kikubwa cha kuzalisha sukari ambacho kinategemea zaidi ya wananchi 6000. 
Awamu ya pili ya Mradi huo (baada ya miaka mitano) inategemewa kufanyika Mkoani Kigoma ambapo sukari itakayozalishwa pia itasafirishwa na kuuzwa katika nchi za jirani.

Ziara hii inafuatia ombi la Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli alilotoa (mwezi Marchi, 2017) kwa Mhe. Balozi Jhumun kumtaka kusaidia kuleta wawekezaji watakaoanzisha Viwanda vya sukari hapa nchini, wakati Balozi huyo akiwasilisha Hati za Utambulisho, Ikulu Dar es Salaam.
Kaimu Katibu Mkuu Mhe Balozi. Ramadhan Mwinyi akikaribisha wageni hao.


Pichani ni Wajumbe wa Kituo cha Uwekezaji (TIC), pamoja na Balozi Jhumun akiwa na Bw. Boodram kutoka Mauritius (kulia, mwisho).





Monday, August 13, 2018

Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC wafunguliwa mjini Windhoek, Namibia

Mkutano wa siku mbili wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) umefunguliwa rasmi katika Hoteli ya Safari mjini Windhoek, Namibia tarehe 13 Agosti 2018.

Ujumbe wa Tanzania katika mkutano huu unaongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga ambaye ameambatana na viongozi waandamizi wa Serikali ya Tanzania ambao ni pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda; Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (anayesimamia masuala ya Ujenzi) Mhandisi Joseph Myamhanga, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dkt. Evaristo Longopa; Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Khatibu Kazungu na Naibu Katibu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Bw. Edwin Paul Mhede.

Mkutano huu ni sehemu ya mikutano ya awali ya maandalizi ya mkutano wa 18 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC utakaofanyika tarehe 17 na 18 Agosti 2018 mjini Windhoek, Namibia.  Mikutano mingine ya awali ni mkutano wa Makatibu Wakuu wa SADC uliofanyika tarehe 9 na 11 Agosti 2018 na Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Asasi ya Ushirikiano wa Siasa , Ulinzi na Usalama ya SADC (SADC Organ on Politics, Defence and Security) utakaofanyika tarehe 16 Agosti 2018 ambao utapitia na kujadili hali ya Siasa, Ulinzi na Usalama katika Kanda kwa kipindi cha Agosti 2017 hadi Agosti 2018. 

Mkutano  wa Asasi ya SADC ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama utahusisha nchi tatu za SADC Organ TROIKA na wajumbe wake ambao ni Angola (Mwenyekiti wa sasa wa Asasi ya SADC ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama), Zambia (Makamu Mwenyekiti wa Organ) na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (Mwenyekiti wa Organ aliyemaliza muda wa uenyekiti wa Asasi).

Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali utapokea, kujadili na kutolea maamuzi ya mapendekezo mbalimbali yanayotokana na mikutano ya kisekta na kamati za jumuiya kwa kipindi cha mwaka 2017/18. Pamoja na mambo mengine mkutano huu;

Utafanya uteuzi wa Mwenyekiti wa SADC na inatarajiwa kuwa Jamhuri ya  Namibia ambayo ni Makamu Mwenyekiti wa sasa itateuliwa kuwa  Mwenyekiti wa SADC kwa kipindi cha 2018/2019. Nafasi ya Makamu mwenyekiti itajazwa pia na nchi itakayoteuliwa ambayo itajulikana tarehe 17Agosti 2018.

Uteuzi wa Mwenyekiti wa Asasi ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC. Inatarajiwa kuwa Jamhuri ya Zambia, ambayo ni Makamu Mwenyekiti wa sasa itateuliwa kuwa Mwenyekiti kwa kipindi cha 2018/2019. Hivi sasa Tanzania ni Mwenyekiti anayemaliza muda wake kwenye Asasi ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC (SADC Organ on Politics, Defence and Security).


Mambo mengine yanayotarajiwa kujitokeza na kujadiliwa katika mkutano huu ni pamoja na;  masuala ya fedha; Utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Viwanda wa SADC  (Report on the operationazaition) na Maendeleo ya Viwanda;  Kutia saini itifaki mbalimbali ikiwa ni pamoja na itifaki ya Kulinda Hakimiliki ya Wagunduzi wa aina Mpya za Mbegu za Mimea ya mwaka 2017. Pia Mkutano huu utatoka na tamko la nchi wanachama wa SADC la kutokomeza malaria katika ukanda wa SADC ifikapo mwaka 2030. 



==========================================================

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa katika Mkutano wa siku mbili wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika unaofanyika tarehe 13 na 14 Agosti 2018 katika hoteli ya Safari mjini Windhoek, Namibia .

Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) Dkt. Stergomena L. Tax (mstari wa mbele kati) akiwa katika picha ya pamoja na Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya maendeleo ya Kusini mwa Afrika mara baada ya hafla ya ufunguzi wa mkutano huo mjini Windhoek, Namibia.

Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika, Dkt. Stergomena L. Tax akitoa hotuba ya ufunguzi wa mkutano wa Mawaziri wa SADC.

Katika hotuba yake aliwasilisha taarifa fupi ya mwaka ya utekelezaji ya Jumuiya hiyo pamoja na kuishukuru Serikali ya Afrika Kusini (Mwenyekiti aliyemaliza muda) kwa uongozi na usimamizi mzuri katika kipindi chote cha Agosti 2017 hadi Agosti 2018.

Mwenyekiti aliyemaliza muda wake na Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Afrika Kusini, Mhe Dkt. Lindiwe Sisulu (kushoto) akikabidhi nafasi ya uenyekiti kwa mwenyekiti mpya ambaye ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Namibia, Mhe. Netumbo Nandi-Ndaitwa. 

Mwenyekiti mpya wa Mawaziri wa SADC, Mhe. Nandi-Ndaitwa akihutubia mara baada ya  kupokea nafasi hiyo.
Katika hotuba yake alisistiza umuhimu wa kuwawezesha vijina kwa kuwa ndio nguzo kuu katika kuinua uchumi wa taifa lolote duniani sambamba na uwekezaji katika viwanda. Pamoja na hayo akaeleza malengo makuu ya kuanzishwa kwa jumuiya hiyo ni kuondoa umasikini na kuinua uchumi ndani ya kanda. 

Mkutano ukiendelea, walioketi nyuma ya Mhe. Waziri Mahiga kutoka kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Prof. Adolf Mkenda na Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Viwanda na Mawasiliano (anayeshughulikia masuala ya ujenzi) Mhandisi Joseph Nyamhanga.

Mkutano ukiendelea, Kutoka Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Khatibu Kazungu, Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Innocent Shiyo na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Bw. Edwin Mhede.

Wa kwanza kulia ni Balozi wa Tanzania nchini Namibia mwenye makazi yake nchini Afrika Kusini, Mhe. Sylivester Ambokile na wajumbe wengine wa Serikali ya Tanzania wakifuatilia ufunguzi wa mkutano.

Sehemu nyingine ya wajumbe kutoka Serikali ya Tanzania wakifuatilia mkutano. 

Balozi wa Namibia nchini Tanzania pamoja na wajumbe wengine wa mkutano huo wakifuatilia hafla ya ufunguzi.

Saturday, August 11, 2018

Katibu Mkuu Mambo ya Nje atembelea Chuo Kikuu cha Tiba cha Namibia

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda (kulia) akizungumza na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Namibia. Prof. Kenneth Kamwi Matengu (kushoto) alipomtembelea chuoni hapo mjini Windhoek, Namibia  tarehe  10 Agosti 2018. Wanaofatilia mazungumzo wa pili kulia ni Balozi wa Tanzania nchini Namibia mwenye makazi yake nchini Afrika Kusini Balozi Mhe.Sylivester Ambokile  na wa Pili kushoto ni Mkurugenzi msaidizi katika chuo hicho Bw. Evaristus Evaristus

Katika mazungumzo yao wawili hao wamejadili juu ya kuongeza maeneo ya ushirikiano na  kuanzishwa kwa programu za kujenga uwezo na kupeana uzoefu. Chuo Kikuu cha Namibia kinashirikiana na Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA), Chuo Kikuu cha Ardhi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na sasa  chuo hicho kina mpango wa kuanzisha mazungumzo ya ushirikiano na Chuo Kikuu cha Muhimbili. 

Mazungumzo yakiendelea, kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. James Lugaganya, Balozi wa Namibia nchini Tanzania, Mhe. Theresia Samaria.

Picha ya pamoja.
==================================

Baada ya mazungumzo Katibu Mkuu, Prof. Adolf Mkenda alitumia fursa hiyo kutembelea Chuo Kikuu cha Tiba cha Namibia ambacho ni Tawi la Chuo kikuu cha Namibia kilichopo mjini Windhoek, Namibia. 

Prof. Kenneth Matengu (wa kwanza kulia) akimwongoza Prof. Mkenda na ujumbe wake kutembelea chuo hicho.
Wa kwanza kushoto ni Mhadhiri katika chuo hicho akifafanua taratibu za masomo ya nadharia na vitendo zinavyoendeshwa katika chuo hicho.



Wakitembelea Maabara za kufundishia.

Wakitembelea vyumba vya semina kwa wanafunzi.
Baadhi ya majengo ya ofisi na madarasa katika Chuo kikuu cha Tiba cha Namibia.

Wizara ya Mambo ya Nje yahamasisha uwekezaji katika sekta ya Kilimo na Mifugo


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda amefanya mazungumzo na kampuni ya Burmeister & Partiners  (PTY) LTD ya nchini Namibia tarehe 10 Agosti 2018 mjini Windhoek, Namibia.

Akiongea na uongozi wa kampuni hiyo Prof. Mkenda alieleza Tanzania ina eneo kubwa la ardhi yenye rutuba  ambayo haitumiki na rasilimali watu ya kutosha hivyo ni fursa kwa mwekezaji mwenye nia thabiti kuwekeza nchini.

“Lengo la Serikali ni kupata mwekezaji aliye makini kama wewe nimeona una mradi mkubwa wa shamba la mifugo na vifaa vya kisasa kwa ajili ya machinjio nina imani ukija kuwekeza Tanzania hautajutia kabisa kwakuwa matumizi ya teknolojia ya kisasa katika miradi itaongeza thamani ya mazao na bidhaa zitakazozalishwa na kuwezesha kupatikana kwa soko la kimataifa” alisema Prof. Mkenda

Naye Mkurugenzi wa kampuni hiyo Mhandisi Hendrik Boshoff alieleza  kampuni imekuwa ikifanya kazi katika mataifa mbalimbali ambapo kampuni hiyo imefungua kampuni ya maziwa nchini Rwanda ambayo inauza na kusafirisha mataifa mengine pia imewekeza nchini Angola katika miradi ya uvuvi na imekuwa ikifanya vizuri katika biashara zake zote.

Pia alisema kampuni imebobea katika miradi ya ujenzi, nishati, miradi ya maji, usafiri, usanifu majengo, ujenzi wa majengo, miradi ya machinjio, mashamba ya mifugo na pia ipo katika mpango wa kuanzisha miradi ya viwanda vya dawa za binadamu ambapo utekelezaji wake utaanza mara baada ya kukamilisha mazungumzo na wataalamu kutoka nchini Cuba.

Prof. Mkenda alieleza miradi yote kutoka katika kampuni hiyo inatija kubwa kwa maendeleo ya taifa la Tanzania hivyo akaikaribisha kampuni hiyo kuja mapema nchini ili kuweza kujionea rasilimali zilizopo na kuainisha miradi watakayoweza kuanza nayo. Vilevile akaeleza  kampuni hiyo ina nafasi ya kutumia fursa za mji wa Dodoma katika uwekezaji kufuatia kuhama kwa mji wa Serikali kutoka Dar es Salaam.

Kampuni ya Burmeisters & Partiners (PTY) LTD ilianza kufanya kazi zake nchini Namibia mwaka 1984 na baadae kuwa miongoni mwa kampuni kubwa zilizowekeza nchini humo. Pia ni kampuni  hiyo inatoa huduma za  kihandisi na huduma za usimamizi wa miradi katika taaluma mbalimbali.


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda(kulia) akizungumza na mwakilishi wa kampuni ya Burmeister and Partners (PTY) LTD alipowatembela katika ofisi za kampuni hiyo iliyopo Windhoek, Namibia tarehe 10 Agosti 2018. Kulia kwa Katibu Mkuu ni  wajumbe walioambatana naye katika ziara hiyo, Mratibu wa Maendeleo na Ushirikiano wa Kimataifa katika Kilimo kutoka Wizara ya Kilimo Tanzania, Bi. Magreth Ndaba, Mkurugenzi wa Sera na Mipango katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa  Afrika Mashariki , Bw. James Lugaganya na Balozi wa Tanzania nchini Namibia, Mhe. Sylivester Ambokile.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Burmeister & Partners (PYT) LTD, Mhandisi Hendrik Boshoff akielezea usanifu wa miradi mbalimbali unaofanywa na kampuni ya Burmeister & patners (PTY) LTD.

Sehemu ya ofisi iliyosanifiwa na kampuni hiyo.

Mazungumzo yakiendelea.

Mwakilishi kutoka kampuni hiyo akiwasilisha miradi mbalimbali iliyosanifiwa na kampuni ya Burmeister & Partners (PTY) LTD

Prof. Mkenda akifafanua tunu na rasilimali zilizopo nchini ambazo ni fursa kwa uwekezaji.

Friday, August 10, 2018

Tanzania na Namibia kuimarisha ushirikiano katika sekta ya Elimu ya juu.

Serikali ya Tanzania imeonesha nia ya wazi ya kuongeza maeneo ya ushirikiano katika sekta ya elimu ya juu na Serikali ya Namibia ambapo ushirikiano huo utawezesha walimu na wanafunzi kuwa na progamu za kubadilishana kwa lengo la kupeana uzoefu na kujengeana uwezo.

Hayo yamesemwa wakati wa ziara ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf F. Mkenda katika chuo kikuu cha Namibia cha Sayansi na Teknolojia  Mjini Windhoek, Namibia tarehe 09 Agosti 2018.

Katika ziara hiyo Prof. Mkenda aliambatana na Balozi wa Tanzania nchini Namibia mwenye makazi yake mjini Pretoria nchini Afrika Kusini, Mhe. Balozi Sylivester Ambokile, Balozi wa Namibia nchini Tanzania, Mhe. Theresia Samaria na Mkurugenzi wa Sera na Mipango katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. James Lugaganya.

Lengo la ziara hiyo ni kujadili namna ya kuongeza ushirikiano katika sekta ya elimu ya juu kwenye masuala ya utafiti na ugunduzi katika taaluma za teknolojia zinazotolewa na vyuo vitakavyoingia makubaliano ya ushirikiano.

“Nimekuja tushirikishane mikakati mbalimbali tunayoweza kujiwekea ili kuvifanya vyuo vyetu viwe bora ndani ya kanda na Afrika kwa ujumla pia tujadili mbinu mpya za kielimu ambazo Tanzania na Namibia  zinaweza zikashirikiana,”alisema Prof. Mkenda

Pia akaeleza nchi nyingi za Afrika zinapata changamoto ya uwezo mdogo na uhaba wa rasilimali fedha katika kuhakikisha upatikanaji wa malazi kwa wanafunzi, upatikanaji wa elimu kwa vitendo na kwamba ni vema Tanzania na Namibia zikatumia fursa za ushirikiano wa elimu zinazosainiwa katika Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika.

Naye Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Namibia  cha Sayansi na Teknolojia, Dkt. Tjama Tjivikua alieleza kuwa hadi sasa chuo kimefanikiwa kuanzisha ushirikiano na taasisi, makampuni na viwanda mbalimbali nchini humo na hata nje ya nchi ili kuwawezesha wahitimu katika chuo hicho kupata nafasi ya elimu kwa vitendo.

“Jitihada hizi zimeshaanza kuleta matunda kwa kuwa kwa sasa wahitimu wa chuo hiki wamefanikiwa kupata ajira katika taasisi hizo na wengine walifanikiwa kupata ajira kabla ya kuhitimu muda wa mafunzo” alisema Dkt. Tjivikua

Vilevile chuo kinashirikiana na wadau mbalimbali ambapo alieleza Tanzania ni mmoja wa wadau kupitia chuo cha Sayansi ya Kilimo Sokoine(SUA) na chuo kikuu cha Ardhi, wadau wengine ni pamoja na Afrika Kusini,  Cameroon, Kenya, Botwana, Uswiss, na mashirika mengine ya kimataifa.

Balozi wa Tanzania nchini Namibia, Mhe. Sylivester Ambokile naye alisema kwa kuwa jumuiya ya wanamibia imezungukwa na jamii inayozungumza Kiswahili hivyo ni vema ushirikiano uliopo ukazidi kuimarishwa kwa kuingiza lugha ya Kiswahili katika idara za lugha za kigeni kwenye vyuo vikuu nchini Namibia.

“Katika hafla ya utambulisho wangu kwa Rais wa Jamhuri ya Namibia, Mhe. Hage Geingob niliwasilisha wazo la Kiswahili kuingizwa katika Idara za Lugha ya kigeni na lilipokelewa vizuri, hivyo kwa sasa ofisi za ubalozi zinafanya jitihada za kukumbushia katika sekta husika ili utekelezaji wake ukamilike mapema”. alisema Mhe. Balozi Ambokile

Nchini Namibia elimu ya juu imeanza mwaka 1979/1980 kutokana na kuchelewa huko kuliifanya Namibia kuhitaji Walimu wa taaluma mbalimbali kutoka mataifa mengine. Tanzania ni miongoni mwa nchi yenye walimu wengi katika vyuo vikuu ya Namibia. Pamoja na kuwepo kwa ushirikiano huo Chuo kikuu cha Namibia cha Sayansi na Teknolojia tangu kuanzishwa kwake mwaka 1992 kimekuwa kikishirikiana na Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) katika kupata wataalamu wazuri wa masuala ya mifugo ambao wamekuwa wakirejea baada ya masomo na kulitumikia taifa kwa tija.

====================================================

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda (kushoto) akijadili jambo na Makamu Mkuu wa chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Namibia, Dkt. Tjama Tjivikua mara baada ya kuwasili chuoni hapo kwa mazungumzo rasmi ya kikazi yaliyofanyika tarehe 09 Agosti 2018 mjini Windhoek, Namibia. Pembeni ni Balozi wa Tanzania nchini Namibia mwenye makazi yake nchini Afrika Kusini, Mhe. Sylivester Ambokile.
Katibu Mkuu, Prof. Mkenda akitembelea maeneo ya chuo kikuu cha Namibia cha Sayansi na Teknolojia ili kuweza kujionea uendeshaji wa vipindi vya masomo na mpangilio wa majengo kwa ajili ya madarasa na malazi ya wanafunzi.
Katibu Mkuu, Prof. Mkenda na ujumbe wake wakiwa katika mazungumzo na uongozi wa chuo, wa kwanza kulia ni Balozi wa Namibia nchini Tanzania, Mhe. Theresia Samaria, kulia kwa Prof. Mkenda ni Balozi wa Tanzania nchini Namibia, Mhe. Ambokile na pembeni yake ni Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango, Bw. James Lugaganya.



Mazungumzo yakiendelea.