Saturday, August 11, 2018

Katibu Mkuu Mambo ya Nje atembelea Chuo Kikuu cha Tiba cha Namibia

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda (kulia) akizungumza na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Namibia. Prof. Kenneth Kamwi Matengu (kushoto) alipomtembelea chuoni hapo mjini Windhoek, Namibia  tarehe  10 Agosti 2018. Wanaofatilia mazungumzo wa pili kulia ni Balozi wa Tanzania nchini Namibia mwenye makazi yake nchini Afrika Kusini Balozi Mhe.Sylivester Ambokile  na wa Pili kushoto ni Mkurugenzi msaidizi katika chuo hicho Bw. Evaristus Evaristus

Katika mazungumzo yao wawili hao wamejadili juu ya kuongeza maeneo ya ushirikiano na  kuanzishwa kwa programu za kujenga uwezo na kupeana uzoefu. Chuo Kikuu cha Namibia kinashirikiana na Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA), Chuo Kikuu cha Ardhi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na sasa  chuo hicho kina mpango wa kuanzisha mazungumzo ya ushirikiano na Chuo Kikuu cha Muhimbili. 

Mazungumzo yakiendelea, kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. James Lugaganya, Balozi wa Namibia nchini Tanzania, Mhe. Theresia Samaria.

Picha ya pamoja.
==================================

Baada ya mazungumzo Katibu Mkuu, Prof. Adolf Mkenda alitumia fursa hiyo kutembelea Chuo Kikuu cha Tiba cha Namibia ambacho ni Tawi la Chuo kikuu cha Namibia kilichopo mjini Windhoek, Namibia. 

Prof. Kenneth Matengu (wa kwanza kulia) akimwongoza Prof. Mkenda na ujumbe wake kutembelea chuo hicho.
Wa kwanza kushoto ni Mhadhiri katika chuo hicho akifafanua taratibu za masomo ya nadharia na vitendo zinavyoendeshwa katika chuo hicho.



Wakitembelea Maabara za kufundishia.

Wakitembelea vyumba vya semina kwa wanafunzi.
Baadhi ya majengo ya ofisi na madarasa katika Chuo kikuu cha Tiba cha Namibia.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.