Saturday, August 18, 2018

Mkuutano wa 38 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC umemalizika mjini Windhoek Namibia

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa hafla ya kufunga Mkutano wa 38 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) mjini Windhoek, Namibia tarehe 18 Agosti 2018.
Katika Mkutano huo Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan alisaini itifaki ya kazi na ajira, itifaki ya Kulinda Hakimiliki ya Wagunduzi wa aina Mpya za Mbegu za Mimea ya mwaka 2017.
Pia amesaini Tamko la nchi wanachama wa SADC la kutokomeza malaria katika ukanda wa SADC ifikapo mwaka 2030 na maboresho ya Katiba inayosimamia masuala ya Kamati ndogo ya Wakuu wa Polisi katika Organ.
Mhe. Samia Suluhu Hassan aliwasilisha salamu za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ambapo aliwashukuru wanachama wote kwa kuendelea kuiamini Tanzania katika nafasi za uongozi ndani ya Jumuiya hiyo pamoja na kuahidi kuendelea kushirikiana katika shughuli za maendeleo, siasa, ulinzi, na usalama.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (kushoto) akifuatilia tukio la utiwaji saini wa itifaki katika mkutano wa 38 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC uliomalizika tarehe 18 Agosti 2018 Windhoek, Namibia.
Mwenyekiti wa SADC na Rais wa Jamhuri ya Namibia, Mhe. Hage Geingob akihutubia katika hafla ya kufunga mkutano wa 38 wa  Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC uliofanyika mjini Windhoek, Namibia.

Katibu Mtendaji wa SADC. Dkt. Stergomena L. Tax akihutubia katika hafla ya kufunga mkutano wa  38 wa Wakuu wa Nchi na Serikali ambapo aliwapongeza viongozi wote walioteuliwa kushika nafasi mbalimbali na kuahidi ushirikiano katika utekelezaji wa agenda za SADC.


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda (kati) na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda wa Wizara ya Mambo  ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Innocent Shiyo (kulia) wakifuatilia mkutano.

Ujumbe kutoka Serikali ya Tanzania ukifuatilia utiwaji saini wa itifaki mbalimbali za ushirikiano.



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.